Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WENGER ASHANGAZWA NA MTANDAO WA KLABU YA MAN CITY



Meneja wa Arsenal Arsene Wenger Jumapili alieleza kushangazwa kwake na mpangilio ambao umewezesha kiungo wa kati wa zamani wa Chelsea Frank Lampard kujiunga na klabu ya Manchester City kwa mkopo kutoka kwa ‘klabu-dada’ ya New York City.

Pamoja na kuhamia kwa Lampard uwanja wa Etihad, New York pia wamemkopesha straika wa Uhispania David Villa kwa Melbourne City.

Klabu zote tatu zinamilikiwa na City Football Group, kampuni inayomilikiwa na wamiliki wa City, Abu Dhabi United Group.

Wenger, ambaye timu yake itakabiliana na City wikendi ijayo kupigania Community Shield, alidokeza kwamba ushirika huo huenda ukawapa mabingwa hao wa Ligi ya Premia nafuu wasiyofaa.


Alipoulizwa kuhusu kuhama kwa Lampard, alijibu: “Inanishangaza. Ni kama hizi klabu za ‘City’ zitalisha klabu kuu, Man City. Nilisikia wanataka kununua klabu tano kote duniani.

“Ninafahamu sheria vyema. Walinunua klabu (New York City) kwa $100 milioni (euro 74 milioni) Marekani ya kucheza msimu ujao.

"Kwa sasa, wachezaji wanaowanunua hawawezi wakacheza hadi mwaka ujao, kwa hivyo wanawasajili katika klabu hizo na wanaweza kuwatoa nje kwa mkopo.

“Ni njia ya kukwepa sheria (za shirikisho linalosimamia soka Ulaya Uefa) za uchezaji haki kifedha? Sijui.”

Alipouliza kama Arsenal ingependa kuanzisha mtandao wake kama huo wa klabu, alijibu: “Tunafurahia kutumia pesa tunazotengeneza kuendesha klabu yetu. Hatuna pesa nyingi za ziada za kununua klabu nyingine.”

Wenger alikuwa akihutubu katika kikao cha wanahabari baada ya timu yake kushindwa 1-0 na Monaco katika dimba la kirafiki la Kombe la Emirates katika uwanja wa Emirates wao Arsenal.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa