Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUSHUKA TENA DIMBANI LEO NA MAFUNZO

Wakati Simba ikitarajia kucheza mechi ya kirafiki leo dhidi ya timu ya Mafunzo ya Zanzibar, kocha Patrick Phiri amesema anatarajia kupata kikosi cha kwanza baada ya Raphael Kiongera kuungana na wachezaji wenzake.

Hii itakuwa ni mechi ya pili ya kirafiki kwa kikosi hicho cha Phiri, baada ya ile ya awali dhidi ya Kilimani City ambayo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Akizungumza jana kwa njia ya simu mara baada ya mazoezi ya timu hiyo, Phiri alisema Kiongera anatarajia kuwasili mwishoni mwa wiki, huku kikosi cha kwanza ambacho kitaanza kucheza katika michuano ya Ligi Kuu ya Bara kitajulikana wiki moja kabla ya michuano hiyo kuanza.


Phiri alisema kwa sasa ni vigumu kutangaza kikosi cha kwanza kwa vile wachezaji wengine waliosajiliwa na timu hiyo bado hawajawasili kuungana na wenzao katika mazoezi. Ligi Kuu ya Bara itaanza Septemba 20.

Mzambia huyo alisema kwa sasa pamoja na mazoezi ataendelea kusaka mechi na kirafiki dhidi ya timu zitakazoshiriki Ligi Kuu, kwani zitasaidia kumpa picha ya kile anachopaswa kukitarajia kwenye ligi.

Alisema baada ya mechi ya leo dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar itakayopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, wanatarajia kucheza dhidi ya Mtibwa Sugar Septemba 6, huku wakiendelea kusubiri mechi ya kirafiki ya kimataifa.

Alisema katika mechi yao ya awali dhidi ya Kilimani City, licha ya kwamba walishinda, hakuridhika na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake.

"Bado nahitaji kiwango zaidi katika timu yangu, lengo langu ni kufanya vizuri msimu huu katika ligi kuu ya Bara," alisema Phiri.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa