Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RIO FERDINAND ALIVYOTEMWA 'KIROHO MBAYA' MAN UNITED

BEKI Rio Ferdinand amemaliza maisha take ya soka Manchester United baada ya kuambiwa hatapewa Mkataba mpya.
 
Mkuu wa Old Trafford, Ed Woodward alimpa habari hizo za kusikitisha Ferdinand mwenye umri wa miaka 35 katika chumba cha kubadilishia nguo Jumapili wakati wa mchezo wa mwisho na Southampton. 
 
Wengi wamesikitishwa na kitendo cha Woodward kuamua kumuacha 'kiroho mbaya' Ferdinand baada ya miaka 12 ya kuitumikia klabu hiyo kwa moyo wake wote.

Champions: Ferdinand shows off the 2006/07 Premier League trophy with Cristiano Ronaldo
Kumbukumbu za furaha: Ferdinand akiwa ameshika taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2008 na Cristiano Ronaldo baada ya kuifunga Chelsea kwa penalti
New boy: Ferdinand shows off his United shirt with then manager Sir Alex Ferguson after joining from Leeds for £29.1million in July, 2002
Alipowasili: Ferdinand akikabidhiwa jezi ya United na mocha wakati huo, Sir Alex Ferguson baada ya kujiunga na timu hiyo akitokea Leeds kwa dau la uhamisho la Pauni Milioni 29.1 Julai mwaka 2002

FERDINAND MAN UNITED

Kusajiliwa: July 2, 2002
Ada: Pauni Milioni 29.1
Mechi alizocheza: 455
Mabao aliyofunga: 8
Mataji aliyoshinda: Ligi Kuu (2002/03, 2006/07, 2007/08, 2008/09, 2010/11, 2012/13), Ligi ya Mabingwa (2007/08), Kombe la Ligi (2005/06, 2008/09), Kombe la Dunia la Klabu (2008)
Katika taarifa aliyoweka kwenye tovuti yake binafsi usiku wa jana, Ferdinand amesema; "Mambo fulani yamenifanya nishindwe kusema kwaheri kwa namna amabyo ningependa,".
Na huku akiwa amekubali kumruhusu beki mwingine wa kati Nemanja Vidic kuondoka, mchezaji mwenzake wa zamani Ferdinand, Gary Neville ametweet: "Hivyo inaonekana kama Rio na Vida wameruhusiwa kuondoka!!!
Beki huyo wa zamani wa England amewaambia wenzake safe ya 1-1 juzi ndiyo ilikuwa mechi yake ya mwisho katika klabu hiyo wakiwa kwenye ndege kurejea kutoka St Mary na akawaomba wamsainie mpira abaki nao kama kumbukumbu yake.
Ferdinand, ambaye alikuwa mchezaji ghali kihistoria England wakati anasajiliwa United kutoka Leeds kwa dau la Pauni Milioni 29.1 Julai mwaka 2002, ameichezea timu hiyo mechi 455 lakini alionekana hafai chini ya David Moyes.
Hard man: Ferdinand is escorted from the pitch by Robin van Persie after being cut by a coin thrown from the crowd during a Manchester derby in 2012
Amemwaga damu: Ferdinand akisindikizwa kutoka uwanjani na Robin van Persie baada ya kuchanwa na sarafu iliyorushwa uwanjani na mashabiki wakati wa mechi ya mahasimu wa Jiji la Manchester mwaka 2012
On target: Ferdinand scores a rare goal against Liverpool in a 2-0 win at Old Trafford in 2006
Alikuwa anafunga pia: Ferdinand akifunga boa dhidi ya Liverpool katika ushindi wa 2-0 Uwanja wa Old Trafford mwaka 2006

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa