Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CD YA JAY-Z AKICHAPWA NA WIFI YAZUA BALAA

Mitandao ya kijamii imewaka moto kufuatia kanda ya video iliyozuka ikionyesha dadake mwanamuziki wa kimataifa Beyonce Knowles , Solange Knowles akimchapa makonde mwanamuziki Jay-Z ambaye pia ni shemeji yake katika lifti.

Hoteli ambako kisa hicho kinadaiwa kutokea mjini New York, 'The Standard Hotel' ilisema kuwa inachunguza ambavyo kanda ya kisa kilichotokea ndani ya Lifti iliweza kusambazwa baada ya kanda hiyo ya video kuzuka katika mtandao mmoja wa udaku TMZ.


Hata hivyo kanda hiyo haikuwa na sauti bali ilionyesha tu kitendo cha dadake Beyonce akimpacha Jay-Z na hata kujaribu kumpiga teke mara mbili wakiwa ndani ya lifti hiyo pamoja na Beyonce na mlinzi mmoja wa Jay-Z aliyejaribu kumzuia Solange.

Kanda hiyo ilizuka baada ya Beyonce aliyekuwa ameambatana na mumewe Jay Z pamoja na Solange kuhudhuria tamasha la kifahari mjini New York tarehe tano Mei.
Dadake Beyonce Solange Knowles
Mlinzi wa Jay-Z anaonekana katika kanda hiyo akijaribu kumzuia Solange mwenye umri wa miaka 27 aliyeonekana kuwa na hasira mno kutomchapa Jay-Z amwenye umri wa miaka 44 akiwa amesimama kando ya mkewe wa miaka sita Beyonce.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, taarifa kutoka kwa maafisa wa hoteli ambamo kisanga hicho kilitokea walielezea kukasirishwa na mtu ambaye aliisambaza kanda hiyo kwenye internet na hata kutishia kumchukulia hatua pindi atakapojulikana.

"tumeshtushwa sana na kukasirishwa na mtu aliyekiuka sheria zetu za faragha ambazo wageni wetu wanathamini sana, '' ilisema taarifa kutoka kwa wakuu wa hoteli hiyo.

"tunachunguza hali hiyo na pia yeyote atakayepatikana na hatia ataadhibiwa vikali.''
Wasimamizi wa Beyonce walikataa kuzingumzia kisa hicho.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa