Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM FC YAVURUGA MAPATO YA SIMBA NA YANGA

Kuibukia kwa mafanikio kwa timu ya Azam FC na kufanya vibaya kwa miamba ya soka nchini kumeanza kuzipa machungu ya kiuchumi timu za Simba na Yanga, ambazo katika mechi iliyopita baina ya watani hao wa jadi ziliingiza mapato kiduchu ya Sh. milioni 130, ambayo ni madogo zaidi kupatikana katika miaka ya karibuni tangu ulipojengwa uwanja mpya wa Taifa 2007.

Katika taarifa ya uongozi wa Simba iliyotolewa mwanzoni mwa wiki kuhusu tathimini yao kwa msimu huu, katibu mkuu wa klabu hiyo ya Msimbazi, Ezekiel Kamwaga alisema walikuwa wakiambulia mgawo wa mapato wa hadi Sh.300,000 katika baadhi ya mechi zao ikiwamo dhidi ya Ashanti United ambayo walilala 1-0.


Mechi baina ya Simba na Yanga ambayo kwa kawaida huwa na mashamsham tele nchi nzima, ya kufungia msimu huu ya Aprili 19, 2014 iligeuka kuwa kama mechi ya "ndondo" ikichezwa huku Azam ikiwa tayari imeshatwaa ubingwa wa bara kwa mara ya kwanza tangu ilipopanda daraja 2008.

Mashabiki wachache mno walihudhuria kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mechi hiyo iliyokosa mvuto huku shamrashamra zikitawala "upande wa pili" kwenye uwanja wa Azam Complex ambako Azam walikuwa wakikabidhiwa kombe lao na kuwashuhudia mashabiki wote walioingia siku hiyo wakipewa chakula na vinywaji bure.

Mapato ya Sh. milioni 130 yaliyozishuhudia timu hizo kila moja ikiambulia mgawo wa Sh. milioni 30, yalikuwa ni pigo kiuchumi kwa timu hizo zinazotegemea kwa kiasi kikubwa mapato makubwa ya mechi baina yao kwa ajili ya "kuzibia mashimo" mengi katika kujiendesha kila msimu.

Kufikia sasa, rekodi ya mapato ya mechi baina ya Simba na Yanga ni ya raundi ya kwanza msimu huu iliyomalizika kwa sare ya 3-3 ambayo iliingiza Sh. milioni 500.7.

Rekodi ya awali ya mapato ya mechi baina ya miamba hao wawili wa soka nchini ilikuwa ni Sh. milioni 500.4, iliyopatikana katika mechi ya kufungia msimu uliopita ambayo Yanga ilishinda 2-0 Mei 18, 2013.

Kushuka kwa mapato katika mechi za Simba na zile za Yanga msimu huu kumechangiwa na kiwango kisichoridhishwa cha timu hizo zinazopendwa na mashabiki wengi zaidi nchini ambazo zitalazimika kujipanga zaidi msimu ujao ili kuwarejesha mashabiki wao viwanjani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa