Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANELKA KUTOCHEZA BRAZIL

Nicholas Anelka

Klabu cha Brazil Atletico Mineiro kimetangaza wamefutilia mbali mipango ya kumsaini straika wa Ufaransa, Nicolas Anelka.

Mkurugenzi wa timu hiyo Eduardo Maluf amesema kuwa Mineiro wameshindwa katika juhudi zao za kuwasiliana na mshambuliaji huyo aliyechezea Arsenal, Real Madrid, Paris Saint Germain na Chelsea na wamekata tama ya kusajili nyota huyo aliye na umri wa 35.

“Hakuna wakati tulifanikiwa kuzungumza naye,” vyombo vya habari vya Brazil vilinukuu Maluf akisema.

Miniero walidhibitishia AFP kuwa Anelka hatajiunga na gwiji wa Brazil, Ronaldinho, anayesakata kabumbu yake kwenye timu hiyo huku Maluf akiongeza watatuma malalamishi kwa shirkisho la soka duniani, FIFA, kuhusu straika huyo.


Mkurugenzi huyo anashikilia kuwa waliaafikiana na waakilishi wa Anelka lakini wakala wake, Cristian Cazini, aliwapasha habari kuwa mchezaji huyo hatawasili Brazil Jumamosi iliyopita kama ilivyopangiwa.
“Tuliamua kandarasi hiyo imebatilishwa kwani hatutasubiri hadi tarehe 19,” Maluf alifafanua.

Mwenyekiti wa Mineiro Alexandre Kalil alisema Aprili 5 kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Anelka atasaini huku wanahabari wa Brazil wakichapisha picha za mashabiki wa klabu hicho wakibeba mabango ya kumkaribisha straika huyo.

Anelka alisafiri Kuwait kuhudhuria kongamano la vijana wa dini ya Kiislamu badala ya kutua Brazil kukamilisha maagano kati yake na Miniero.

Maluf alifichua kuwa mkataba ulikuwa mezani ukingoja sahihi yake uliaafikia angelicheza nao hadi Desemba mwaka ujao.

Klabu cha Ligi ya Premier ya Uingereza, West Bromwich Albion kilimfuta Anelka mwezi uliopita kwa upotuvu wa nidhamu baada ya kuonekana kuonyesha ishara ya kupinga usemiti ‘quenelle’ baada ya kuwafungia bao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa