Ruka hadi kwenye maudhui makuu

VAN PERSIE AMTABIRIA MAKUBWA MOYES.

Robin van Persie amesema ana imani kwamba meneja wa Manchester United anayekabiliwa na shinikizo David Moyes atafana Old Trafford.

Moyes amekumbana na mwanzo mbaya wa ufanyakazi wake United kwani timu hiyo imehangaika katika juhudi zake za kutetea taji la Ligi ya Premia na pia ilibanduliwa kutoka kwa Kombe la FA raundi ya tatu.

United wako alama 11 nyuma ya viongozi Arsenal na wanakabiliwa na mlima katika juhudi zao za kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao.

Kumekuwa na uvumi kwamba Moyes ameshindwa kupata imani kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa United.

Na mahangaiko ya klabu hiyo katika juhudi zake za kudumisha viwango vya miaka ya Alex yamepelekea kushuka kwa thamani ya hisa za klabu katika Soko la Hisa la New York.


Lakini straika wa United Van Persie, ambaye amekosa sehemu kubwa ya msimu huu kutokana na jeraha la paja, ana imani kwamba Moyes atafanikiwa akipewa muda.

“Ninafikiri kwamba anahitaji muda sawa na watu wengine wote, hasa ukiwa mgeni katika klabu kubwa,” Van Persie aliambia gazeti la Guardian.

"Na kwa kweli, sidhani kwamba watu hawaelewi kwamba wanahitaji kumpa muda zaidi, na naongea kuhusu mashabiki na hata sisi.

“Atapata muda huo na kila mmoja anajua kwamba tutabadilisha mambo karibuni.

“Tulipoteza alama nyingi msimu huu, nyingi sana, lakini ikiwa unataka kupigania mataji yote, ni lazima ucheze vyema na ushinde mechi nyingi – lakini tunafanya kila tuwezalo kubadilisha hilo.

"Meneja ndiye kiongozi wetu katika hilo na anajaribu kadiri awezavyo na ninafikiri atabadilisha mambo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa