Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OSCAR AIBEBA CHELSEA IKIIADHIBU STOKE.

Bao maridadi kutoka Oscar liliiongoza Chelsea kuwalaza Stoke City 1-0 katika raundi ya nne ya kombe la FA jana Jumapili.

Kiungo huyo wa Brazil ambaye alichukua nafasi ya Juan Mata, aliyesajiliwa na Manchester United, kama kielelezo cha mashambulizi, alitia kimiani kutokana na mkwaju wa adhabu.

Ubora wa bao lake nyota huyo lilidhihirisha sababu iliyomfanya meneja Jose Mourinho kuekeza imani naye na kumruhusu Mata kuondoka Stamford Bridge siku mbili zilizopita.


Chelsea walipoteza nafasi kadhaa za kuadhibu Stoke huku wakipata ulingo wa lango mara mbili lakini hatimaye, wageni wao hawakutishia kulazimisha wenyeji mechi ya marudiano.

“Bao moja kwa bila haitoshi kuonesha jinsi tulivyocheza na kumiliki mechi. La muhimu ni kushinda na kuepuka mchuano wa marudio kwani hatuhitaji mechi ya ziada,” Mourinho aliambia runinga ya ITV.

Meneja wa Stoke, Mark Hughes, alilalamikia uamuzi wa mkwaju wa adhabu dhidi ya Erik Pieters baada ya kukabiliana na straika, Samuel Eto’o, ambao Oscar alifunika wavuni lakini aliinuliwa moya na jinsi vijana wake walivyo cheza.

“Hatukubuni nafasi wazi. Ilikuwa ngumu kwetu lakini ninafurahia yale tuliyoyafanya. Hatukuzama nah ii ni ishara ya mazuri,” aliendelea.

Wachezaji wenye uzoefu miongoni mwao nahodha John Terry na kipa Petr Cech walipumzishwa ingawa Eto’o alipewa nafasi ya kuanza na Mourinho huku Demba Ba, aliyetarajiwa kuorodheshwa akibaki kwenye benchi.

Ni bidii za nyota huyo wa Cameroon aliyefunga matatu dhidi ya United wiki iliyopita ambazo zilifungua ngome ya Stoke na kumruhusu Oscar kuibuka shujaa katika dakika ya 27 pale alipochezewa vibaya na Pietersen.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa