Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LOGA AIPONDA FOWADI SIMBA, AZIDI KUMUANDAMA MWOMBEKI.

 Baada ya kupata ushindi finyu katika mechi yake ya kwanza katika Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic 'Loga', amesema ligi hiyo ni ngumu na timu ndogo ndizo zimekuwa kikwazo kwa klabu kongwe za hapa nchini, lakini akaweka wazi kuwa washambuliaji wake bado hawajaelewa darasa lake.

Simba juzi iliifunga Rhino Rangers ya mkoani Tabora bao 1-0 lililoiwezesha kufikisha pointi 27, hivyo kuendelea kukaa katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na wapinzani wao Yanga wakifuatiwa na Azam FC na Mbeya City.


Akizungumza juzi baada ya mechi, Loga, alisema mechi yao ilikuwa ngumu na ushindi huo finyu walioupata umethibitisha kwamba hakuna timu ya kuidharau katika ligi.
Loga alisema kikosi chake kilikutana na ushindani na kupoteza nafasi nyingi za kufunga ambazo walitengeneza katika mchezo huo.

"Ligi ina ushindani, ina changamoto na si rahisi, kila timu sasa ni kubwa, leo (juzi) nimethibitisha timu ndogo zinavyoendelea kuzisumbua timu kongwe. Jambo zuri nimefurahi ni kupata ushindi," alieleza kocha huyo raia wa Croatia.

Loga alisikitishwa pia na kitendo cha wachezaji wake kukosa nafasi za kufunga na kueleza kwamba hali hiyo inatokana na kikosi chake kutokuwa na washambuliaji wenye uzoefu.

Alisema anatarajia katika mechi ijayo kuwaanzisha Edward Christopher na Zahor Pazi.
Hata hivyo, wakati Loga akieleza hayo, mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe ndiye anayeongoza katika orodha ya wafungaji kwenye ligi hiyo.

AMCHAMBUA MWOMBEKI


Loga alisema hataweza kuvumilia kuona mchezaji anabaki uwanjani akifanya 'madudu' na si yale aliyoelekezwa katika benchi la ufundi kabla ya kuingia kucheza.

Kocha huyo alisema mchezaji anayecheza kwa kufuata maelekezo ataendelea kumpa nafasi kwa sababu malengo yake kila mechi ni kushinda.

"Sina ujamaa na mtu, wao ni wachezaji na mimi ni kocha, anayefanya vizuri atabaki uwanjani na atakayeharibu nitamtoa nje, hii ni katika kujenga uimara wa kikosi changu kwenye kila idara," Logarusic aliongeza.

Betram Mwombeki aliingia katika dakika ya 65 akichukua nafasi ya Tambwe lakini zikiwa zimebakia dakika nne mchezo kumalizika alimtoa nje kutokana na kuboronga, hivyo kumpisha kiungo, Henry Joseph.

Simba itaanza tena mazoezi leo kwa ajili ya kujiandaa na mechi yake dhidi ya JKT Oljoro itakayofanyika Februari Mosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa