Ruka hadi kwenye maudhui makuu

EMMANUEL OKWI ANUKIA MSIMBAZI

MGANDA Emmenuel Okwi aliyesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili na nusu kukipiga Yanga kabla na shirikisho la kandanda nchini TFF kuingilia kati kuhoji usajili wake kama una baraka zozote kutoka Fifa, Imebainika kuwa mchezaji huyo atarejeshwa katika klabu yake ya zamani ya Simba endapo klabu ya Etoile Du Sahel ya Tunisia itashiondwa kuilipa Simba SC pesa zake dolaza Kimarekani 300,000.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ambaye ni rafiki wa karibu na mjumbe mmoja wa kamati ya sheria, hadhi za wachezaji wa TFF amedai kuwa barua iliyoandikwa na TFF kwenda Fifa ilikuwa na nmaaguizo mawili tu.


Agizo la kwanza ni kutaka kujua kama kweli Okwi ana uhalali wa kukipiga Yanga, wakati la pili likitaka klabu ya Simba ilipwe pesa zake za usajili ama sivyo Simba irejeshewe mchezaji wake harafu imuuze kwa timu nyingine kama itataka au aendelee kuichezea.

Endapo Fifa itaamua kupitisha mapendekezo hayo mawili ya TFF basi mchezaji huyo atarejea katika klabu yake ya zamani ya Simba na kuifanya Yanga ichanganyikiwe, Yanga ilitangaza kumnunua Okwi kutoka klabu ya SC Villa ya Uganda ambayo nayo ilipewa kwa mkataba wa miezi sita na Fifa baada ya klabu yake ya Etile Du Sahel kushindwa kumlipa mshahara wa miezi mitatu.

Hata hivyo chanzo hicho cha habari kimesema kwamba bado Fifa inaendelea kupitia mapingamizi matatu ya mchezaji huyo na ikijiridhisha itatoa tamko, 'Inawezekana akaruhusiwa kuicheza Yanga au kumrejesha katika klabu yake ya zamani', kilisema chanzo hicho.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa