Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BIN SLUM AICHIMBA MKWARA YANGA, ASISITIZA KIPIGO KIKO PALEPALE MKWAKWANI.

MKURUGENZI wa Ufundi wa Coastal Union ya Tanga, Nassor Bin Slum amesema Yanga SC itakiona cha moto kwa timu yake keshokutwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Akizungumza na mtandao huu Bin Slum amesema kwamba vijana wake wapo vizuri kuelekea mchezo huo na hakuna shaka Yanga itaacha pointi zote tatu Uwanja wa Mkwakwani Jumatano.

“Tunakubali msimu huu tumeshindwa kutimiza malengo yetu, siyo kwenye ubingwa tu, bali hata nafasi za nne za juu. Malengo yetu ya sasa ni kumaliza nafasi ya tano,”alisema Bin Slum.


Amesema ili wafanikiwe kumaliza katika nafasi hiyo, lazima wafanye vizuri katika mechi zilizobaki za Ligi Kuu na hawatakubali kuwa ngazi za timu nyingine kuelekea kwenye ubingwa.

“Coastal Union hatutakubali kamwe kufanywa daraja la timu nyingine zenye kutaka ubingwa, na anayetaka kuamini haya Jumatano tunacheza na Yanga, mtawaonea huruma,”alisema.

Coastal Union na Yanga SC ndizo timu pekee za Ligi Kuu zilizoweka kambi nje ya nchi kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi hiyo.

Wakati Yanga walikuwa Uturuki ambako walicheza mechi nne za kirafiki na kushinda mbili na kutoa sare mbili, Coastal walikuwa Oman ambako walicheza mechi nne pia na kushinda mbili, sare moja na kufungwa moja.
  
Katika mechi zao za ufunguzi za mzunguko wa pili Jumamosi, Yanga ilianza vyema kwa kuifunga Ashanti United mabao 2-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Coastal ililazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na JKT Oljoro Mkwakwani.

Yanga SC ambao ndio mabingwa watetezi wa Ligi Kuu, wapo kileleni mwa ligi hiyo kwa pointi zao 31, baada ya kucheza mechi 14, wakifuatiwa na Azam FC na Mbeya City zenye pointi 30 kila moja, wakati Coastal ni ya nane kwa pointi zake 17 baada ya mechi 14 pia.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa