ARSENAL WAINGIA MKATABA MPYA MNONO NA PUMA

KLABU ya Arsenal imetangaza kuingia Mkataba wa muda mrefu wa udhamini wa vifaa vya michezo na kampuni ya Puma kuanzia Julai mwaka 2014.

Pamoja na hayo hakuna kiwango cha fedha cha udhamini huo kilichothibitishwa Jumatatu, ingawa dili hilo linatajwa kama kubwa zaidi katika historia ya uhusiani wa Puma na Arsenal.


Inafahima Washika Bunduki hao wanapokea kiasi cha Pauni Milioni 30 kwa mwaka kutoka kwa wadhamini wakuu, shirika la ndege la Emirates, na imeripotiwa dili hilo jipya litakuwa sawa na lile ambalo Puma walitoa wakati wanaiponya timu hiyo Nike, waliokuwa wadhamini wa Arsenal tangu 1994.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI