MAN CITY YACHAKAZWA NA ASTON VILLA

Yaya Toure wa Man City
Yaya Toure wa Man City
Manchester City wamekosa nafasi ya kuwa miongoni mwa viongozi wa ligi waliposhindwa na Aston Villa 3-2.

Goli la kwanza lilifungwa na City kupitia nyota wao Yaya Toure ambaye ametoa matumaini kwa City ya kuondoka na ushindi wa kwanza wa ugenini.
Goli hilo lakini halikukaa kwa muda mrefu kabla ya kukombolewa Karim El Ahmadi.
Edin Dzeko alifufua matumani ya City kwa kufunga bao la pili.Lakini nalo likasawazishwa na Leandro Bacuna kabla ya Andreas Weimann kufunga kazi kwa kufunga bao la 3.
Katika matokeo mengine ni kwamba Cardiff imepata ushindi ugenini wa mabao 2-1 dhidi ya Fulham,Hull ikainyuka West Ham goli 1-0 na Southampton kuibamiza Crystal Palace mabao 2-0.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI