Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA AZAM AWATAJA WACHAWI WAKE.........

Kocha Stewart Hall (Pichani) amesema alimuacha nje ya kikosi cha kwanza cha Azam mfungaji bora wa ligi msimu uliopita, Kipre Tchetche na kiungo bora yosso Salum Aboubakar 'Sure Boy', katika mechi waliyoshinda 3-2 dhidi ya mabingwa Yanga, kwa sababu nyota hao wanaonekana wameridhika na mafanikio ya msimu uliopita na hawajitumi.


"Kuwa na mafanikio msimu uliopita hakukuhakikishii mafanikio msimu huu," alisema Hall.
Muingereza huyo aliongeza kuwa sare tatu katika mechi nne zilimfadhaisha na aliona kuna tatizo kikosini kwamba baadhi ya wachezaji wanaotegemewa hawajitumi.

"Ndiyo maana nikaamua kuwachezesha yosso na nikawaacha nje Kipre Tchetche na Sure Boy. Wanapaswa kujituma ili kuendelea kupata namba kikosini. Niliwaanzisha vijana kwa sababu najua wana usongo wa kupata mafanikio, wanajituma. Huwezi kucheza kama huna bidii," alisema Hall.

Imani yake kwa yosso ilimlipa Hall, ambaye aliwashuhudia wachezaji waliopandishwa kutoka timu yao ya vijana, winga Farid Musa na mshambuliaji Joseph Kimwaga waking'aa.

Kimwaga (18), ambaye aliingia katika uwanjani katika dakika ya 72 kuchukua nafasi ya yosso mwenzake, Musa, aliifungia Azam goli la ushindi katika dakika ya mwisho ya mchezo.

Matokeo hayo yalizima uteja wa Azam wa mechi nne mfululizo kutoka kwa Yanga, ambayo ilitawala kiasi kikubwa cha mechi ya juzi.

Hall pia aliisifu Yanga kuwa ilicheza vizuri zaidi yao akisema kwamba "timu bora" haikushinda juzi baada ya kuwashuhudia mabingwa hao watetezi wakikosa bahati baada ya mashuti yao  mawili kugonga mwamba, huku kipa wa Wanalambalamba, Aishi Manula akifanya kazi ya ziada kuzuia "mvua" ya magoli langoni mwa Azam.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa