Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BREKING NEWS: NGASA AKUMBANA NA ADHABU NYINGINE TFF

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeshindwa kutambua rufani ya Yanga kupinga adhabu ya Mrisho Ngassa kufungiwa mechi sita na kulipa faini ya Sh45 milioni, pamoja na ile ya kutaka mechi yao dhidi ya Mbeya City irudiwe.


Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya TFF chini ya Mwenyekiti Alex Mgongolwa ilimfungia Ngassa baada ya kubaini winga huyo alisaini mkataba wa mwaka mmoja Simba kabla ya kutua Yanga.

Kamati hiyo ilimfungia mechi sita na kulipa faini Sh15 milioni na kuwarudishia Simba Sh30 milioni.

Yanga iliandika barua kwa TFF kukata rufaa ya kupinga adhabu hiyo ingawa kwa sasa shirikisho hilo limewajibu halitambui barua hiyo ni ya kamati ipi ya rufani.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura ameliambia gazeti hili jana jijini Dar es Salaam: “Nafikiri Kamati za Rufani TFF ni nyingi, wao Yanga katika barua yao hawajaeleza wamekata rufaa hiyo kwenye kamati gani.

“Tulichowajibu ni kwamba hatutambui kuwa barua hiyo ya kukata rufaa wameiandikia kamati gani ya rufani TFF,” alisema Wambura.

Naye Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema: “TFF wametujibu kwa maandishi kwamba hawajui rufaa waipeleke kwenye kamati ipi. Ni jambo ambalo limetushangaza kwa kweli.

“Kwa sasa sina cha kukueleza zaidi, naomba usubiri uongozi ukutane kwa ajili ya kulizungumzia hilo,” alisema Baraka.

Mechi kutorudiwa

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeiweka pembeni rufani iliyowasilishwa na Yanga kutaka mchezo dhidi yao na Mbeya City uliofanyika mwishoni mwa wiki  kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya urudiwe.

Uongozi wa Yanga ulifikia hatua hiyo ya kupeleka rufaa TFF, baada ya vuguru zilizotokea kabla ya kuanza kwa mechi na watu wanaodhaniwa kuwa ni mashabiki wa Mbeya City kulipiga mawe basi la Yanga na kumsababisha majeraha dereva wa basi hilo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa