KING MAJUTO AIBUKA TENA NA MBOTO

Mchekeshaji mkongwe nchini, Amri Athuman 'King Majuto' (Pichani) ameibuka tena na filamu iitwayo 'Tikisa' ambayo inaendelea kutikisa katika soko la filamu Tanzania.


Katika filamu hiyo iliyoandaliwa na Salma Jabu 'Nisha' na kuandikwa na kuongozwa na Leah Richard 'Lamata', King Majuto kama kawaida yake anavunja mbavu mwanzo mwisho akishirikiana na Haji Salum 'Mboto' na wakali wengine walioigiza pamoja.

Kwa mujibu wa Lamata, mbali na  Majuto na Mboto, filamu hiyo imewashirikisha pia Hemed Suleiman 'PHD', Chuchu Hans, Jacklyne Wolper na wengine.

"Ni bonge la filamu ambalo karibu waigizaji wote wametikisa kama lilivyo jina la filamu yenyewe, ni moja ya kazi nzuri nilizowahi kuziandika na kuziongoza baada ya kutoka na 'Poor Minds' na 'Pain Killer'," alisema Lamata.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI