Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HUMUD SAFI SIMBA, KULAMBA MAMILIONI KUICHEZEA MSIMU UJAO

Kiungo mkabaji wa zamani Azam FC, Abdulhalim Humoud (Pichani) ameibukia Simba akisaka nafasi ya kusajiliwa kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Humoud aliyemaliza mkataba wake na Azam FC Mei, mwaka huu na kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa na klabu ya Jomo Cosmos, yuko kambi ya Simba iliyopo, Kigamboni, Dar es Salaam.
Akizungumza jana, Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are alithibitisha mchezaji huyo kuwepo kwenye kambi ya timu yake akisaka nafasi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi,  Agosti 24.
Itang’are alisema kuwa Kocha Abdallah Kibadeni ndiye aliyemtaka mchezaji huyo anayedaiwa kufuzu na klabu ya Jomo Cosmos.
“Kocha ndiye ametaka aje kambini kufanya mazoezi na timu ili aweze kujiridhisha na kiwango chake kabla ya kusaini mkataba,” alisema na kuongeza.
“Kamati ya Usajili Simba, tunasubiri kauli ya mwisho kutoka benchi la ufundi na kufanya naye makubaliano ya kusaini mkataba.”
Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni alisema jana kuwa, yuko kwenye kambi ya Simba kwa siku tano sasa akifanya mazoezi na wachezaji wenzake.
“Maendeleo yake ni mazuri ingawa siwezi kusema lolote kwa sasa. Ni mchezaji ambaye namjua vizuri, siyo mgeni kwangu. Pia najua aliwahi kuichezea Simba kipindi cha nyuma kabla ya Azam FC.” alisema Kibadeni.
Humoud alipofuatwa na gazeti hili baada ya kumaliza mazoezi alisema: “Sitaki kuzungumza lolote kwa sasa, ni mapema.”
Humoud alijiunga na Simba akitokea Mtibwa Sugar na kutolewa kwa mkopo na klabu hiyo kwenda Azam FC.
Wakati huohuo, mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Hussein Javu amejiunga na mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga na jana asubuhi alifanya mazoezi.
Javu aliyekuwa akitolewa macho na Simba, amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili mpaka mwaka 2015.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa