Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA KUANZA KUTETEA KAGAME J,PILI

MABINGWA watetezi wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), Yanga wanatarajia kuanza mazoezi Jumapili kwa ajili ya kujianda na michuano hiyo ambayo mwaka huu itafanyika nchini Sudan, Hata hivyo, mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara wataanza mazoezi bila ya nyota wake walioko kwenye kikosi cha timu ya taifa (Taifa Stars).

Akizungumza na MAMBO UWANJANI, Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, alisema kuwa tayari wameshawapa taarifa ya kuanza kwa mazoezi hayo wachezaji ambao hawako kwenye kikosi cha Taifa Stars na kuongeza kwamba kocha Mholanzi Ernie Brandts, atarejea nchini Jumapili akitokea kwao alikoenda kwa mapumziko.

Saleh alisema kwamba kocha alielekeza kuanza mazoezi siku hiyo akiamini kwamba nyota walioko Stars nao wanaendelea kujinoa na watakaporejea nchini wataimarisha kasi.

Alisema katika ripoti yake amehitaji mechi moja ya kirafiki kabla ya kuelekea Sudan katika mashindano hayo yatakayoshirikisha timu 13 za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

"Ila sijui itakuaje kwa wachezaji ambao mikataba yao imeisha na mpaka sasa hawajui hatma yao, ni ngumu mchezaji kufika mazoezini huku akiwa hana uhakika na ajira yake," alisema meneja huyo.

Katika mashindano ya Kombe la Kagame yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) na kufanyika kila mwaka, Yanga imepangwa kundi C na itaanza kampeni za kutetea ubingwa wake kwa kuivaa Express ya Uganda kwenye Uwanja wa Alfasher, Juni 20 saa nane mchana na watashuka tena dimbani Juni 22 mwaka huu kuikabili Ports ya Djibout. Watakamilisha mechi za hatua ya makundi Juni 25 kwa kuvaana na Vital'O kutoka Bujumbura, Burundi.

Wawakilishi wengine wa Bara,  Simba wako katika kundi A na wataanza kwa kuivaa El Mereikh Juni 21 kabla ya Juni 23 kuikabili APR ya Rwanda. Watamaliza dhidi ya Elman ya Somalia, Juni 26.

Mechi ya ufunguzi wa mashindano hayo itakayofanyika Juni 18 saa nane mchana itazikutania Tusker ya Kenya dhidi ya Super Falcon ya Zanzibar na saa 10:00 jioni wenyeji Al Hilal watachuana na Al Nasri.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa