Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wachezaji wageni Ligi Kuu kubanwa

Dar es Salaam. Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema litakutana na klabu za Ligi Kuu kuzikumbusha azimio la mwaka jana la mjini Bagamoyo kuhusu wachezaji wa kigeni.

Azimio hilo lilipitisha sheria inayokataza klabu za Ligi Kuu kusajili zaidi ya wachezaji watatu kutoka nje ya nchi.
Pamoja na sababu mbalimbali za kupitisha azimio hilo, dhamira kuu ilikuwa kuwapa fursa wachezaji wa ndani kuonyesha vipaji vyao kwenye michuano ya ligi.
Kwa sasa, klabu zinaruhusiwa kusajili siyo zaidi ya wachezaji watano kufikia msimu uliomalizika, lakini kama azimio hilo litaungwa mkono na klabu, basi msimu wa 2013/14 utashuhudia wachezaji wachache wa kigeni.
Klabu za Simba, Yanga na Azam ndizo zinaoongoza kusajili wachezaji wa kigeni kulinganisha na timu zingine zinazoshiriki ligi hiyo.
Mtendaji Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alikaririwa na mtandao wa soka nchini Uganda, akisema mchakato huo unaendelea kufanyiwa kazi na watakutana na viongozi wa klabu kujadili.
“Ni sheria mpya ya Azimio la Bagamoyo. Ni vyema sheria zilizowekwa na sisi wenyewe zikaheshimika. Tutakutana na klabu kujadili azimio hili,” alisema Osiah.
Kabla hata ya kufanyika kwa kikao hicho, klabu hizo zenye utamaduni wa kusajili wachezaji wa kigeni, zilionyesha kutoridhika nalo.
Katika msimu uliopita klabu ya Azam ilikuwa na wachezaji wa kimataifa kutoka Kenya, Joackins Atudo na Humphrey Mieno, Brian Umony kutoka Uganda na wachezaji wawili kutoka Ivory Coast, Kipre Tchetche na Michael Bolou.
Kwa upande wa Yanga, Haruna Niyonzima kutoka Rwanda, Mganda Hamis Kiiza na Didier Kavumbagu wa Burundi na Mbuyu Twite, huku Simba ikiwa na Abel Dhaira, Musa Mudde, Felix Sunzu na Komabil Keita.
Pamoja na tahadhari hiyo, klabu hizo zimeendelea na zoezi la kusajili wachezaji wa kigeni bila kufikiria uwepo wa azimio la Bagamoyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa