Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AKINA MBIYAVANGA WAONDOLEWA TENA NA KIBADEN SIMBA

Kocha mpya wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Abdallah 'King' Kibadeni
 
Wakati kocha mpya wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Abdallah 'King' Kibadeni akiahidi kuanza kurejesha heshima ya kikosi hicho katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), tayari amewapiga 'panga' wachezaji wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao walikuwa wakifanya majaribio.

Wachezaji hao ambao Kibadeni na wasaidizi wake hawajaridhishwa na viwango vyao ni Fabrice Baloko, Fabian Tshiyaz, Patrick Milambo na Joe Fills.

Akizungumza na mtandao huu Kibadeni ambaye aliiongoza Simba kufikia fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993, alisema kuwa bado amewapa nafasi wachezaji wengine wawili, kiungo mkabaji kutoka Ivory Coast, Kouakou Martial na beki anayetoka Nigeria, Youssouf Gabra.

Aliongeza kuwa bado milango iko wazi katika kuangalia wachezaji wa kuwasajili na jana jioni zaidi ya nyota watatu kutoka klabu za Prisons, JKT Ruvu na JKT Oljoro, walitarajia kuanza mazoezi chini ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba.

Kocha huyo alisema kwamba anataka kufanya usajili kwa umakini ili kuhakikisha msimu ujao Simba inafanya vizuri na anarejesha imani kwa mashabiki wake.

Kocha huyo mkongwe alisema kuwa kikosi hicho ambacho kiko katika mabadiliko kinahitaji muda ili kuweza 'kusimama' na kucheza kama timu hasa kufuatia uamuzi uliofanyika wa kujenga upya timu yenye mchanganyiko wa wachezaji chipukizi na wazoefu.

"Timu hii ina wachezaji wakubwa ambao wanatakiwa kuelimishwa na kubadilishwa kidogo na wachezaji vijana nao wanahitaji kuelimishwa ili kujua nini wanatakiwa kufanya kukabiliana na ushindani," alisema kocha huyo.

Aliongeza kwamba kikubwa anachokiangalia yeye ni wachezaji kuwa na nidhamu huku akisisitiza kutowarudisha wachezaji waliosimamishwa kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Simba tayari imeshawasajili Issa Rashid kutoka Mtibwa, Zahor Pazi (Azam), Andrew Ntalla (Kagera Sugar), Ibrahim Twaha (Coastal Union) na Mganda Samuel Ssenkoomi wa URA ya Uganda.

Wakati huo huo, Simba inatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa Juni 12 mwaka huu dhidi ya Sofapaka inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka ya Kenya.

Mratibu wa mchezo huo,George Wakuganda, alisema kuwa mchezo huo utatumiwa na Simba kutambulisha wachezaji wapya.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa