SIMBA YAWAVUA MAGWANDA POLISI MORO



MABINGWA wa zamani wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Simba SC jana waliwavua magwanda Polisi Moro baada ya kuifunga magoli 2-1 kwenye uwanja wa Taifa jijini, Polisi Moro ambayo ilistahili ushindi mechi hiyo ili ijiwekee mazingira ya kubaki ligi kuu lakini ilijikuta inashindwa kuhimili mashambuliizi ya wachezaji wa Simba.
Kwa matokeo hayo sasa Polisi inasubiri miujiza tu ili kubaki ligi kuu, magoli ya Simba yalifungwa na Haruna Chanongo na Mrisho Ngassa, Hata hivyo Simba inajiandaa vilivyo kabla haijakutana na hasimu wake mkubwa Yanga Mei 18

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI