Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2025

Kenya yaweka hai matumaini ya kutinga robo fainali

WENYEJI, Kenya ‘Harambee Stars’ wameweka hai matumaini ya kwenda Robo Fainali ya michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Morocco ‘Simba wa Atlasi’ katika mchezo wa Kundi A leo Uwanja wa Moi International Sports Centre, Nairobi. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliaji wa Tusker FC, Ryan Wesley Ogam dakika ya 42 akimtungua kipa wa Raja Athletic, maarufu kama Raja Casablanca. Lakini haukuwa ushindi mwepesi kwa wenyeji, kwani walilazimika kucheza pungufu kipindi chote cha pili baada ya kiungo wake wa ulinzi, Chrispine Erambo wa Tusker pia kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45’+4. Mchezo mwingine wa Kundi A leo Angola imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Zambia Uwanja wa Taifa wa Nyayo hapo hapo Nairobi. Mabao yote ya Palancas Negras yamefungwa na mshambuliaji wa Interclube, João Chingando Manha ‘Caporal’ dakika ya 79 na 86, wakati bao pekee la Chipolopolo limefungwa na beki wa Kabwe Warriors, Dominic Chanda dakika ya 73. Baad...

Pamba Jiji yaibomoa Mlandege FC

Klabu ya Pamba Jiji, imekamilisha usajili wa , Abdallah Idd Pina , kutoka Klabu ya Mlandege FC Kwa mkataba wa miaka miwili. Mshambuliaji huyo alikuwa mfungaji bora msimu 2024 katika ligi ya Zanzibar akiwa na mabao 21 , mbali na kufumania nyavu nyota huyo alikuwa na mchango mzuri sana katika Kikosi cha Pamba Jiji.

Rayvanny atoboa siri ya kutoka WCB

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Rayvanny, amefichua kwa mara ya kwanza kuwa alilipa kiasi cha shilingi bilioni 1.3 za Kitanzania ili kuondoka rasmi kwenye lebo ya WCB Wasafi, licha ya hakukuwa  na mkataba wowote wa kisheria wa rayvanny na lebo hiyo. Rayvanny alijiunga na WCB mwaka 2015 na kupitia lebo hiyo, alifanikiwa kujizolea umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania. Baada ya miaka kadhaa ya mafanikio, alianzisha lebo yake binafsi ya Next Level Music (NLM)

Masikini, Bruno Gomez atangaza kuacha soka

Aliyewahi kuwa kiungo wa Singida Black Stars Bruno Gomez (Barosso) ametangaza kuacha mpira kwa muda kutokana na maumivu ya Enka na goti yanayomsumbua kwa muda mrefu sasa. Bruno alianza kuumia Enka akiwa Tanzania na hata baada ya kuamua kurudi nyumbani Brazil aliendelee kucheza kwa kujilazimisha lakini kwa sasa imeshindikana kuendelea! “Kwa sasa sina timu, sina wakala wala mtu yoyote wa kunihudumia isipokuwa mimi, juhudi zangu na Imani yangu..!” - Sehemu ya Maneno ya kiungo huyo Raia wa Brazil.

Simba na Malongo kimeeleweka

Klabu ya Simba SC imempatia mkataba mlinzi , Hernest Malonga, aupitie aangalie kama ataridhika nao basi akubali kusaini katika Klabu hiyo. Taarifa za awali zinaeleza kuwa mazungumzo yamekuwa mazuri kati ya mchezaji na Klabu ya Simba SC, lakini pia nyota huyo ndie alikuwa chaguo la kocha Fadlu Davies ukimtoa Mligo ambaye tayari amesatambulishwa katika timu hiyo.

Kanoute kutua Azam FC

Kiungo wa kimataifa wa Mali Sadio Kanoute (Puttin)  ambaye amewahi kuwa Nyota wa Simba na JS Kabyle atawasili Tanzania Usiku wa leo tayari kujiunga na Azam Fc . Sadio Kanoute atawasili majira ya Saa tisa Usiku Tanzania tayari kukamilisha utaratibu wake wa kujiunga na Azam na kuingia kambini kule Arusha tayari kwa Msimu mpya akiwa na Azam Fc  . Ni rasmi Sadio Kanoute ni Mali ya Azam

Taifa Stars njia nyeupe robo fainali

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars usiku huu imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Madagascar mchezo wa kundi B kombe la mataifa Afrika kwa wachezaji wanaicheza ligi ya ndani maarufu CHAN. Licha kwamba Madagascar imeongoza kwa mchezo mzuri, yaani ball pozisheni, ilianza kupata bao la kwanza likifungwa na Clement Mzize dakika ya 13 kabla ya dakika ya 20 kufunga la pili. Bao pelee la Madagascar limefungwa na Razafi Mahatana dakika ya 34, Stars moja kwa moja inatinga robo fainali kwani mpaka sasa ni vinara wa kundi B ikiwa na pointi 9.

Simba kuhama kambi Misri

Timu ya Simba inatarajia kuhamisha kambi yake huko Misri kutoka mji wa Ismailia kwenda jijini Cairo kutokana na sababu mbalimbali zilizotajwa na benchi la ufundi la timu hiyo. Akizungumza katika mahojiano maalumu kupitia tovuti ya Simba, Kocha Mkuu Fadlu Davids amesema lengo la kuhamisha kambi kwenda Cairo ni kupata mechi nzuri za kirafiki zenye ushindani. “Tarehe 15 tutahamisha kambi kutoka Ismailia hadi Cairo, ambako tutacheza mechi za kirafiki zenye ushindani ili kujiandaa ipasavyo. Kadri tunavyocheza mechi za kirafiki, wachezaji wapya na wa zamani wanazidi kuzoeana. “Msimu uliopita tulikuwa vizuri kwenye Ligi Kuu, lakini kwenye Kombe la Shirikisho la CAF tulikosa ubora wa kutosha. Sasa tunapanda kiwango tunakwenda Ligi ya Mabingwa Afrika, tunahitaji kikosi chenye ushindani wa hali ya juu.  Hadi sasa Simba imeshafanya usajili wa wachezaji wapya saba, kati yao wanne ni wa kimataifa ambao ni Rushine De Reuck, Alassane Kante, Mohamed Bajaber na Jonathan Sowah wakati wengine watatu ...

Yanga yaichakaza Yanga

TIMU ya kwanza ya Yanga leo imeshinda mabao 4-0 dhidi ya timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Mabao ya Yanga A yote yamefungwa na wachezaji wapya, kiungo Lassine Kouma kutoka Stade Malien ya kwao, Mali, washambuliaji Muivory Coast, Ange Celestin Ecua kutoka Zoman FC ya kwao na Mkongo DR, Andy Bobwa Boyeli (24) kutoka Sekhukhune United FC ya Afrika Kusini na winga mzawa, Offen Francis Chikola kutoka Tabora United. Yanga imekamilisha wiki moja tangu ianze mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya Jijini Dar es Salaam na wiki ijayo inatarajiwa kwenda Rwanda kwa maandalizi zaidi pamoja na mechi za kirafiki.

Wakala wa Mzize awajia juu Yanga

Msimamizi wa Clement Mzize, Jasmine Razack amefunguka MENGI kutoka moyoni lakini kubwa kwamba Yanga hawataki kumuuza mchezaji huyo na kilichobaki wanaleta usumbufu kwa kuongeza dau kubwa Ili timu zinazomtaka zishindww. “Nimemchukua Clement Mzize wakati hana timu, Yanga walishamruhusu aondoke pale Under 20 ila Baba yake Mlezi pamoja na Kocha Zahera walikuja kuniomba sana nimchukue kumsimamia, hawajui namna gani Kijana ameteseka kufika alipo hapo, anategemewa na familia na yeye ndio kila kitu kwao, unadhani Yanga wamewekeza kiasi gani mpaka Mzize kufika hapo? Nafasi ya kuvunja Mkataba ipo ila kwasasa sitaki kumsumbua Kijana, acha alitumikie Taifa kwanza”  Jasmine Razack, Msimamizi wa Clement Mzize

Ratiba Ligi ya mabingwa Afrika hadharani

MABINGWA wa Tanzania, Yanga SC wataanza na Wiliete Benguela ya Angola katika Raundi ya Kwanza ya mchujo wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, wakati watani wao, Simba SC wataanza na Gaboron United ya Botswana – vigogo hao wote wakianzia ugenini. Katika droo ya michuano hiyo iliyopangwa mchana wa leo studio za Azam TV, Tabata TIOT, Dar es Salaam ikiongozwa na magwiji wa zamani wa Tanzania, Sunday Manara aliyewika na klabu ya Yanga na Abdallah Kibadeni wa Simba miaka ya 1970 – wawakilishi wa Zanzibar, Mlandege SC wataanzia ugenini na Insuarence ya Ethiopia. Mechi za kwanza zitachezwa wikiendi ya Septemba 19 na 21 na marudiano kati ya Septemba 26 na 28, mwaka 2025 – na washindi watafuzu katika Raundi ya Pili na ya mwisho wa kuingia hatua ya makundi ambayo mechi zake za kwanza zitachezwa kati ya Oktoba 17 na 19 na marudaino kati ya OKtoba 24 na 26. Katika Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC itaanzia nyumbani dhidi ya El Merreikh Bantiu ya Sudan Kusini, wakati Sing...

Wapinzani wa Yanga Ligi ya mabingwa Afrika hawa hapa....

Klabu ya Wiliete Sports Club ndio wapinzani wa Mabingwa wa NBCPL Klabu ya Yanga kwenye hatua ya awali CAFCL .  Wiliete imeanzishwa mwaka September 14, 2018 yaani ina miaka 6 tangia ianzishwe wana uwanja wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 35,000 ( Estàdio de Ombaka , Benguela ) … Wiliete walimaliza mshindi wa pili msimu uliopita kwenye ligi yao ya nyumbani .  Hawa Wiliete walipanda ligi kuu mwaka 2019 kutoka top division …. Jina la utani la hii miamba inaitwa Province .  Wiliete Sports Club hawana rekodi yeyote kwenye mashindano ya CAF ndio mara yao ya kwanza kushiriki CAF COMPETITION. 

Azam FC yamchukua kiboko ya Yanga

KLABU ya Azam imeendelea kuboresha benchi lake la Ufundi kwa kuajiri kocha mwingine Msaidizi, Anicet Kiazayidi Makiadi (33) ambaye anaungana na Mkongo mwenzake, Kocha Mkuu, Jean-Flotent Ibenge.  Anicet Kiazayidi Makiadi anajiunga na Azam FC baada ya kuiwezesha Aigles du Congo kutwaa ubingwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kama Kocha Mkuu. Kabla ya kujiunga na Aigles du Congo, Kiazayidi aliifundisha kwa miezi mitatu Tabora United akichukua nafasi ya Mkenya, Francis Kimanzi aliyeondolewa kwa matokeo mabaya. Ni wakati huo alijitengenezea umaarufu Tanzania baada ya kuiwezesha Tabora United kufanya vizuri ikiwemo kuwafunga mabingwa wa nchi, Yanga mabao 3-1 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Awali, Kiazayidi alikuwa Kocha Msaidizi wa timu za AS Vita Club chini ya Ibenge kati ya 2017 na 2019, Maniema Union chini ya Guy Lusadisu Basisila kati ya 2019 na 2021 na AS Simba kati ya 2022 na 2023 chini ya Mspaniola, Julio César Gómez.

Yanga yapiga tizi la hatari, kocha wa viungo balaa

Kocha wa mazoezi ya utimamu wa mwili (Physic), Tshephang ‘Chyna’ Mokaila raia wa Afrika Kusini akiwaongoza wachezaji wa Yanga leo kwenye mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.

Profesa Jay ammwagia sifa mke wake

Mwanamuziki wa Bongo Hip-hop, Joseph Haule [Prof Jay] amesema kipindi akiwa mgojwa mke wake aliuza kila kitu nilichokuwa nikimiliki awali. "Nadhani akitoka Mungu anafuata mke wangu, Wife alinipambania sana uhai wangu aliona bora auze kila kitu tulichokuwa tukimiliki ili mimi nipone."-Amefunguka Prof Jay.

Esperance yaingia vitani kumnasa Mzize

Klabu ya Espérance Sportive de Tunis ya Tunisia imetuma ofa kwaajili ya kumnasa mshambuliaji, Clement Mzize (28),  Yanga wamekataa ofa ya $600,000 iliyotolewa na Al Masry ya nchini Misri, naelezwa tena kuwa Yanga wapo tayari kupokea $800,000 hadi $900,000 kwa klabu zinazomuitaji Mzize, Esperance inatajwa kuwa kwenye ushindani mkali na Al Sadd SC ya Qatar katika kuwania saini ya Mzize.

Uchaguzi TFF, Karia kushiriki peke yake

RAIS Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace John Karia atagombea peke yake katika uchaguzi Mkuu wa shirikisho hilo Agosti 16, mwaka huu Jijini Tanga. Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Kiomoni Kibamba ametoa orodha ya mwisho wa wagombea leo kufuatia wagombea walienguliwa kuwania nafasi hiyo, Dh. Mshindi Msolla na Shijja Richard kushindwa rufaa yao. Wagombea wengine wote waliopitishwa ni wa nafasi za Ujumbe wa Kanda sita ambao wanaingia moja moja kwenye Kamati ya Kamati ya Utendaji.  Hao ni Lameck Nyambaya atakayechuana na CPA Hosseah Hopaje Lugani katika Kanda Namba 1 (Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtawra), Khalid Abdallah Mohamed anayegombea peke yake Kanda Namba 2 (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara), James Patrick Mhagama anayechuana na Evance Gerald Mgeusa na Cyprian Charles Kuyava Kanda Namba 3 (Ruvuma, Njombe, Mbeya, Songwe na Iringa). Wengine ni Mohamed Omar Aden anayegombea peke yake Kanda Namba 4 (Dodoma, Singida, Shinyanga na Simiyu), Vedast...

Yanga yala matapishi, yamrudisha kocha wa viungo waliomfurusha

Klabu ya Young Africans imetangaza kumrejesha mtaalamu wa tiba na viungo bwana Youssef Ammar ambaye hapo awali aliondoka kwenye klabu na nafasi yake kuchukuliwa na Sekhwela Seroto raia wa Afrika Kusini. Youssef Ammar kutoka Tunisia. Ni mtaalamu na mbobevu mkubwa kwenye masuala mazima ya tiba kwa wachezaji hivyo kurejea kwake klabuni kutaongeza uimara kwenye afya za wachezaji na kuwaepusha na majeraha ya mara kwa mara. Ni mbobevu. Katika hatua hiyo hiyo, Young Africans pia imemtambulisha mtaalamu wa video (Video Analyst), Thulani Thekiso ambaye ni raia wa Afrika Kusini. Mtaalamu huyu wa kuchambua video ambaye ametokea kwenye klabu ya Cape Town City ya Afrika kusini amekuja kuchukua nafasi ya Mpho Maruping ambaye ametimka klabuni hivi karibuni. Mwisho kabisa mabingwa Yanga wamemtambulisha kocha wa makipa aitwaye Majdi Mnasria kutoka Tunisia. Kocha huyu mwenye uwezo mkubwa wa kuwafundisha walinda milango ametua Yanga akitokea kwenye klabu ya Olympique Akbou ya Algeria.

Tshabalala aandika rekodi mpya

Mohamed Hussein, alifunga bao lake la kwanza akiwa na timu ya taifa agosti 2,2025 katika mchezo wa ufunguzi wa michuano ya CHAN dhidi ya Burkinafaso. Imemchukua zaidi ya michezo 40 ndani ya miaka takribani 10 kuifungia bao timu ya taifa ya Tanzania. Mohamed ambaye mara nyingi amekuwa akitumika eneo la ulinzi wa kushoto alianza kuitumikia timu ya taifa rasmi novemba 22,2015 katika mchezo dhidi ya Somalia katika michuano ya CECAFA. Huenda ukawa mwanzo mzuri kwa nyota huyu kuendelea kuifungia mabao muhimu timu ya taifa.

Emmanuel Okwi rasmi atua Police ya Rwanda

Uongozi wa klabu ya Police FC ya Rwanda , Imethibitisha kukamilisha usajili wa , Emmanuel Okwi , Kwa mkataba wa miaka miwili. Nyota huyo ambaye aliwahi fanya vizuri akiwa na Klabu ya Simba , Yanga na Vilabu kadha Uarabuni amechagua kucheza soka Nchini Rwanda Kwa misimu miwili.

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Yanga kukutana Septemba 7

MKUTANO Mkuu wa kawaida wa klabu ya Yanga utafanyika Jumapili ya Septemba 7 kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Taarifa ya Yanga iliyosainiwa na Rais wa klabu hiyo, Hersi Ally Said imesema kwamba Mkutano huo ni kwa mujibu wa Ibara ya 20 ya Katiba ya klabu hiyo ya mwaka 2021.

Mbwana Samatta ajiunga Le Havre ya Ufaransa

Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Mbwana Samatta (32) ameandika rekodi mpya baada ya kujiunga na Le Havre ya Ligi Kuu Ufaransa Ligue1. Samatta ambaye ameandika rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza Ligue1 msimu wa 2025/26 anajiunga na Le Havre kama Mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake wa miaka miwili na PAOK ya Ugiriki. Le Havre inakuwa Klabu yake ya sita Samatta kucheza soka katika ardhi ya Ulaya baada ya KRC Genk na Royal Antwerp za Ubelgiji, Aston Villa ya England, Fenerbahce ya Uturuki na PAOK ya Ugiriki.

Kenya, Angola nguvu sawa

WENYEJI, Kenya ‘Harambee Stars’ wametoa sare ya kufungana bao 1-1 na Angola ‘Palancas Negras’ katika mchezo wa Kundi A Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024 leo Uwanja wa Moi International Sports Centre, Nairobi. Mshambuliaji wa Petro Luanda, Jó Paciência alianza kuifungia bao Angola dakika ya saba, kabla ya kiungo mshambuliaji wa Gor Mahia kuisawazishia Kenya dakika ya 12 kwa penalti. Mchezo mwingine wa Kundi A leo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ‘The Leopards’ imeshinda 2-0 dhidi ya Zambia Chipolopolo’ Uwanja wa Taifa wa Nyayo hapo hapo Nairobi. Mabao ya DR Kongo yamefungwa na  winga wa kushoto wa FC Aigles RDC, Ibrahim Matobo Mubalu dakika ya 51 na mshambuliaji wa DR Congo FC Saint Eloi Lupopo, Malanga Horso Mwaku dakia ya 71.  Baada ya mechi za leo Kenya inapanda kileleni ikifikisha pointi nne katika mchezo wa pili na kuishushia nafasi ya pili  Morocco inayobaki na pointi tatu za mechi moja. DRC inaenda nafasi ya tatu ikiwa na pointi tatu pia baad...

Willy Onana ajiunga CS Sfaxien

Ni rasmi Winga Will Essomba Onana Leo hii Ametambulishwa kuwa mchezaji mpya wa Klabu ya Sc Faxien ya Tunisia kwa Mkataba Wa miaka 3, Onana amewahi kuzichezea Simba,Al Ahly Benghazi ya Libya na sasa atacheza ligi kuu Nchini Tunisia.

Msimamizi wa Mzize aigomea Yanga, adai mchezaji hauzwi kama ng' ombe mnadani

Msimamizi wa mchezaji wa Yanga SC Jasmin, Razack amedai Clement Mzize ambaye ni mteja wake hawezi kuuzwa kama ng' ombe mnadani isipokuwa wanatakiwa kumpa nafasi aamue. "Mchezaji hauzwi uzwi  tu kama Ng'ombe mnadani Kuna sheria na taratibu zake, Umesema Kuna Klabu Yanga wamekubali ofa lakini Mzize hajakubali kikubwa ni kufuata sheria na kanuni, Kama Klabu kwa Klabu wamekubaliana inabaki upande wa Mchezaji kwenye "Personal Terms" ila Hawezi kuuzwa tu kama Ng'ombe Mnadani", Mchezaji sio mtumwa ni ajira kama ulivyoajiriwa Wewe hapo. . "Sisi Mpaka sasa ofa rasmi tuliyoipokea kwaajili ya  Mchezaji huyo ni ofa kutoka Al masry ambayo mwisho wake ni Leo , Al Masry tuliongea na Sports Director wao pamoja na president wa Klabu lakini Bado hatujapata majibu kutoka Yanga" . "Mzize Bado anamkataba na Yanga aliongeza mwakajana tu mkataba wa miaka mitatu kwahiyo Bado anamkataba wa miaka mitatu na Yanga" . "Hizo ofa nyingine unazosema sijui Yanga...

Jentrix Shikangwa kurejeshwa Simba Queens

Baada ya Simba Queens kutangaza kuachana na mshambuliaji raia wa Kenya, Jentrix Shikangwa inadaiwa yupo njiani kurejeshwa kikosini kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) na michuano mingine ya ndani ya soka la wanawake. Hata hivyo, mmoja wa viongozi wa Simba Queens, amesema wameamua kumrejesha kikosini kutokana na uhitaji wake na kile alichokifanya ndani ya misimu mitatu. “Kulikuwa na changamoto kidogo ya uamuzi na ni kama tulikurupuka, lakini maoni ya mashabiki mitandaoni yametuamsha kwa sababu wao pia wanahusika na hii timu,” alisema kiongozi huyo na kuongeza: “Viongozi wakubwa waliuliza shida nini, tukasema mchezaji alitaka kiasi kikubwa cha pesa, wakasema mpatieni hiyo fedha kwa sababu ni mchezaji muhimu kwetu na amefanya makubwa.” Amesema Kiongozi huyo Julai 15 mwaka huu, Simba ilitangaza kuachana na mshambuliaji huyo wa zamani wa Vihiga Queens na timu ya taifa ya Kenya, Harambee Starlets, akiwa miongoni na nyota 13 walioitumikia msimu uliopita. Shikangwa ndani ya m...

Yanga yasaini mkataba wa bil 3.3 na Haier

Klabu ya Yanga SC imesaini mkataba na kampuni ya Haier wenye thamani ya shilingi bilioni 3.3 kwa muda wa miaka mitatu. Makubaliano ya mkataba huo yamefanyika leo na Haier imesaini mkataba huo na Yanga kwa mashindano ya ndani ambapo nembo ya Haier itakaa kwenye jezi za Yanga sehemu ya pembeni mbele.

JOB NDUGAI ATAKUMBUKWA KWA MENGI KWENYE MICHEZO

Na Prince Hoza ALIYEKUWA Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Kongwa, Job Yustino Ndugai amefariki Dunia August 06,2025 akiwa anaendelea kupatiwa matibabu Hospitalini baada ya kuugua ghafla. Ndugai amekuwa Spika wa Bunge tangu November 17,  2015 hadi Januari 06, 2022 alipojiuzulu na kuendelea kuwa Mbunge wa Kongwa  nafasi ambayo ameendelea kuitetea kwa kuchukua fomu tena mwaka huu ambapo ameshinda kwenye kura za maoni. Ndugai ambaye amezaliwa January 22,1960 alishinda kura za maoni za Ubunge wa Jimbo la Kongwa kwa kupata kura 5690. ALIHAKIKISHA TAIFA STARS INAFUZU FAINALI ZA AFCON MWAKA 2019 Ndugai tutamkumbuka kwenye tasnia ya michezo hasa alipokuwa Spika wa Jamhuri ya Muungano ambapo alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha soka la Tanzania linapiga hatua. Ikumbukwe marehemu Ndugai alikuwa sambamba na wabunge wenzake kuunda Kamati ya hamasa ambayo iliisaidia timu ya taifa kufuzu fainali za Afrika, mwaka 2019 Taifa Stars ilifuzu fainali za mataifa Afrika, AFCON zilizofanyika nc...

Mamelodi Sundown's yaikubalia Simba kwa Maena

Klabu ya Simba SC imepokea barua kutoka klabu ya Mamelodi Sundowns ya kukubali kumtoa kiungo wao Neo Maema kujiunga na Wekundu wa Msimbazi kuelekea msimu ujao na kila kitu kimekamilika Neo Maema atajiunga na Simba SC kwa mkopo wa mwaka mmoja akitokea Mamelodi Sundowns na atajiunga na Simba SC baada ya kurudi kutoka katika michuano ya CHAN 2024

Naibu Waziri wa michezo MwanaFA akikabidhi milioni 10 za goli la mama

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, ameikabidhi Taifa Stars kiasi cha Shilingi milioni 10 za goli la mama na kuungwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye ametoa kiasi cha shilingi Milioni 20 pamoja na mdau wa michezo, Azzim Dewji, ambaye ameahidi kiasi cha shilingi Milioni 25 kwa timu hiyo. Stars imejinyakulia fedha hizo baada ya ushindi wa goli 1 - 0, dhidi ya Mauritania, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, Agosti 06, 2025.

Tanzania njia nyeupe robo fainali kombe la CHAN

TANZANIA imeendeleza wimbi la ushindi katika Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mauritania katika mchezo wa Kundi B usiku wa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, beki wa kulia wa Simba SC, Shomari Salum Kapombe dakika ya 89 akimalizia krosi ya winga wa kushoto wa Azam FC, Iddi Suleiman Ali ‘Nado’. Kwa ushindi huo Taifa Stars inafikisha pointi sita kufuatia ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Burkina Faso Jumamosi hapo hapo Uwanja wa Mkapa. Mchezo mwingine wa Kundi B leo Burkina Faso imeshinda 4-2 dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) hapo hapo Uwanja wa Mkapa. Mabao ya Burkina Faso yamefungwa na Nasser Ouatarra dakika ya 11, Guiro  dakika ya 61 kwa penalti, Malo dakika ya 78 kwa penalti pia na Baguian  dakika ya 84, wakati ya CAR yamefungwa na Tchibinda  dakika ya 15 na Zoumara  dakika ya 90+5. Burkina Faso inasogea nafasi ya pili nyuma ya Taifa Stars...

Simba Queens yakamilisha usajili wa wachezaji 10 balaa

Klabu ya Simba Queens itaingia kambini tarehe 15 mwezi huu kwaajili ya maandalizi ya msimu mpya 2025/26. Hadi sasa Simba Queens imekamilisha usajili wa wachezaji ambao ni ; 1. Zainah Nadende (Uganda) 2. Elizabeth Nashoni (Tanzania) 3. Elizabeth Mkuki (Tanzania) 4. Ruth Aturo (Uganda) 5. Zawadi Usanase(Rwanda) 6. Cynthia Musungu (Kenya) 7. Fasila Adhiambo (Kenya) 8. Neema Mtunzi (Tanzania) 9. Asha Omary (Tanzania) 10. Magnifique Umutesiwase (Rwanda) huyu Kuna asilimia kubwa ya kuvunjiwa mkataba baada ya urejeo wa Jentrix Shikangwa. Wengine wawili Beki wa Kati ambaye ana uzoefu mkubwa toka Nigeria pamoja na kiungo mkabaji toka Cameroon (nitawaweka wazi hivi karibu). Kama nilivyowakataa mwaka jana baada ya kufanya tasmini yangu na kutoridhishwa na sajili walizofanya msimu uliopita hasa zile 3 toka Yanga Princess basi vivyo hivyo msimu huu nimekubali sajili za na niweke wazi tu kuwa Simba Queens msimu huu itakuwa ya moto mno.

Inonga huyooo Kuwait

Mlinzi wa zamani wa Simba SC, Hennock Inonga "Backer" ambaye pia ni mchezaji wa timu ya taifa ya DR Congo, amejiunga na klabu ya Kuwait FC ya nchini Kuwait. Inonga ambaye misimu miwili iliyopita alichezea klabu ya FAR Rabat ya Morocco, amesaini kandarasi ya miaka miwili hivyo ataichezea timu hiyo iliyopo mashariki ya kati. Inonga alihusishwa kujiunga na Yanga kwenye dirisha kubwa linaloendelea lakini wajumbe wa kamati ya usajili wa Yanga waligawana makundi wengine wakitaka asajiliwe na wengine wakikataa, lakini pia alihusishwa na Singida Black Stars kabla ya Kuwait FC kuamua kumchukua. Kila kitu kimekamilika msimu ujao Inonga atacheza Uarabuni

MJUE MZAMIRU YASSIN SOLEMBE

Mzamiru Yassin alikuja Simba 16/17, mwaka 2022 akaongeza mkataba wa miaka miwili hadi 2024, akaongeza tena miwili hadi 2026, msimu huu ukiisha Mzamiru anakuwa Free Agent. - Katika muda wote akiwa Simba SC, Mzamiru hajawahi kuwa mbaya bonge moja la Mido, ila lazima tukubali muda wake umeisha na hakuna kipya ataprove Simba, kuzingatia na umri, pia alishatumika. - Simba iliyocheza robo fainali mara nne, ubingwa wa ligi mfululizo huyu kiumbe alikuwepo tena alicheza kwa juhudi sana, kuna wakati lazima tukubali kila nabii na zama zake. - Zama za Mzamiru zinaelekea ukingoni, majeraha pia yamechangia, ila kwa umri wake 33+ na majeruhi aliyokuwa nayo, tukubali Mzamiru kazi imeisha, hakuna miujiza mipya kwake tena. - Kabakisha mwaka mmoja, wasiwasi ni kuwa hata anaweza asipate game time msimu huu, na msimu ujao akiwa free ukamkuta Namungo huko. - Kwa umri wa Mzamiru na mahitaji ya Fadlu, utamuanzisha Mzamiru, Kante? au Kagoma? wakae nje hapana. - Simba iliyopoteza ubingwa misimu minne haiwezi k...

Rasmi Tshabalala ni wa Yanga SC

KLABU ya Yanga imemtambulisha beki wa kushoto Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ anayejulikana pia kama Zimbwe Junior kwa jina lingine la utani kama mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao. Tshabalala anajiunga na Yanga kama Mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake Simba SC aliyoichezea kwa miaka 11 mfululizo. Hussein alijifunga na Simba SC mwaka 2014 akitokea Kagera Sugar ambako alicheza kwa msimu mmoja akitokea timu ya vijana ya Azam FC baada ya kuibukia klabu ya Friends Rangers ya Manzese. Anakuwa mchezaji wa tisa baada ya viungo Lassine Kouma kutoka Stade Malien ya kwao, Mali, Mguinea, Balla Mousa Conte kutoka CS Sfaxien ya Tunisia, Mohamed Doumbia raia wa Ivory Coast aliyekuwa mchezaji huru na washambuliaji Mkongo DR, Andy Bobwa Boyeli (24) kutoka Sekhukhune United FC ya Afrika Kusini na Muivory Coast, Ange Celestin Ecua kutoka Zoman FC ya kwao. Wengine ni wazawa, viungo wawili kutoka klabu za Ligi Kuu ya PBZ Zanzibar, Abdulnasir Mohamed Abdallah wa Mlandege na Nizar Abubakar Othman ...

Yanga yazindua jezi za mazoezi

Klabu ya Yanga SC imezindua jezi zake za mazoezi ambazo kama zinavyoonekana ni nzuri na zinavutia.

Mchezaji kipenzi wa Fadlu atambulishwa Simba

KLABU ya Simba SC imemtambulisha beki wa kushoto, Anthony Richard Mligo ambaye Agosti 6 atatimiza miaka 18 kutoka Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi kuwa mchezaji wake mpya kuelekea msimu ujao. Baada ya kukamilisha usajili wake, Mligo anapanda ndege leo kwenda mjini Ismailia nchini Misri kuungana na wezake kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya. Mligo ni mchezaji aliyeibukia klabu ya Geita Gold msimu wa 2023/2024, kabla ya kuhamia Namungo FC msimu uliopita ambako aliendelea kufanya vizuri na kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes’. Chipukizi huyo alikuwemo kwenye kikosi cha Tanzania kilichotwaa ubingwa wa Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati kwa vijana chini ya umri wa miaka 20, CECAFA U20 Oktoba mwaka jana nchini akiibukia mfungaji wa michuno hiyo. Chipukizi huyo alikuwepo pia kwenye kikosi hicho cha Ngorongoro Heroes kilichoshiriki Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) U20 nchini Misri. Anakuwa mchezaji mpya wa saba kutamb...