Klabu ya Yanga Princess imetambulisha kiungo mshambuliaji Lidya Akoth raia wa Kenya kuwa mchezaji wao kutokea klabu ya Kenya Police Bullets. Msimu uliopita katika raundi ya pili Lidya aliitumikia klabu ya Yanga Princess kwa mkopo wa miezi sita kutokea klabu ya Kenya Police Bullets. Sasa ni rasmi Lidya Akoth ni mali ya Yanga Princess kwa mkataba wa miaka miwili. Attacking mid ya Yanga Princess ; 1. Lidya Akoth 2. Precious Christopher 3. Adebis Ameerat 4. Riticia Nabbosa (ambaye pia anaweza kutumika kama namba 6).
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com