Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2013

CCM NAKO KWAFUKA MOSHI, NAPE APIGWA KOMBORA.

Picha
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa amejibu madai yaliyotolewa hivi karibuni na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kwamba ni mmoja wa mawaziri walioshindwa kazi, hivyo kustahili kung’olewa. Katika madai yake, Nape alisema Dk Kawambwa ameshindwa kusimamia vyema madai ya walimu na kwamba akiwa Waziri wa Miundombinu, aliingia mkataba na Kampuni ya ujenzi ya Progressive iliyopewa zabuni ya kujenga Barabara ya Namtumbo hadi Tunduru wakati mkandarasi huyo hana uwezo wa kuijenga. Nape alikaririwa akisema kwamba umefika wakati kwa waziri huyo na wenzake wa Fedha, Dk William Mgimwa; Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza; na Naibu wake, Adam Malima kuhojiwa na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho. Akijibu madai hayo Mjini Bagamoyo jana, Dk Kawambwa alisema anasubiri kwa hamu kuitwa CC kueleza tuhuma zinazomkabili huku akijigamba kuwa yeye ni mti wenye matunda ndiyo maana unapigwa mawe.

TUTATIBUA REKODI YA CHELSEA -YAYA TOURE.

Picha
KIUNGO Yaya Toure anaamini Manchester City inaweza kuvunja rekodi ya mabao ya msimu katika Ligi Kuu England msimu huu. Kiungo huyo wa nguvu amempa jeuri kocha Manuel Pellegrini juu ya uwezo wa kushambulia unaoleta matumaini ya taji kwa kusema rekodi ya Chelsea iko hatarini. Na baada ya timu ya Pellegrini kufikisha mabao 34 wakiifunga sita Spurs Jumapili, Toure amesema lengo ni kuvunja rekodi hiyo. Alipoulizwa kwamba inaezekana kuipiku rekodi ya Chelsea, alijibu: "Natumaini hivyo — tuna washambuliaji. Watu wawili mbele (Alvaro Negredo na Sergio Aguero ) hawa watu huwezi kuamini. Wanajiamini sana.

KILI STARS YATUA SALAMA NAIROBI.

Picha
BAADA ya safari ya takriban saa nne angani, hatimaye timu ya soka ya taifa ya Bara, Kilimanjaro Stars imeatua salama Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi, Kenya tayari kuwania taji la nne la Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge. Katika michuano hiyo inayoanza kutimua vumbi Novemba keshokutwa, Stars imepangwa Kundi B pamoja na Zambia, Burundi na Somalia na itafungua dimba na Chipolopolo Alhamisi Uwanja wa Machakos. Stars imetua hapa saa 2:45 usiku baada ya safari ndefu kidogo wakipitia Kigali, Rwanda kabla ya kutua Nairobi na iliwachukua saa nzima hadi kupanda basi kuelekea hotelini baada ya kukamilisha taratibu za kuingia nchini hapa za Idara ya Uhamiaji. Stars iliagwa jana mchana kwa hafla fupi kambini kwao katika hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam na kukabidhiwa bendera na Katibu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Henry Lihaya. Katika hafla hiyo, kocha wa Stars, Mdenmark Poulsen pamoja na kumtaja beki Kevin Yon

JANJA YA RAGE YABAINIKA, YADAIWA ANATUMIA MASHABIKI WA YANGA KUMLAKI.

Picha
Imefahamika kwamba mwenyekiti wa Simba ambaye hivi karibuni alisimamishwa na kamati ya utendaji Ismail Aden Rage, inasemekana amekuwa akitumia ujanja wakati wa mapokezi yake na kulakiwa na watu wengi wanaokwenda na vuvuela huku wakimbeba juu juu. Sasa imebainika kuwa mwenyekiti huyo wa Simba anatgumia kundi la mamluki ambao wengineo ni mashabiki wa kutupwa wa Yanga ambao hudiriki kuvaa jezi za Simba na kumuunga mkono, aidha ujanja huo umebainika na Simba wameandaa mpango rasmi wa kumng'oa Msimbazi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mjumbe mmoja wa kamati maalum ndani ta tawi moja maarufu jijini Dar es Salaam lkenye ushawishi mkubwa ndani ya klabu hiyo anasema kuwa ujanja wa Rage umejulikana hivi karibuni baada ya wapambe wake kuwakusanya mashabiki wa soka ambao wengine ni Yanga.

MAKALA: CHALENJI MTIHANI WA MWISHO KWA KIM POULSEN.

Picha
Na Prince Hoza TIMU ya taifa ya Tanzania bara maarufu Kilimanjaro Stars iliondoka jana kuelekea jijini Nairobi kushiriki fainali za mataifa Afrika mashariki na kati ambayo mwaka huu yanafanyika nchini Kenya, kikosi cha bara kiliondoka jana jioni na kuagwa kwa heshima zote. Tumehuhudia nahodha mpya wa timu hiyo akitangazwa badala ya aliyekuwa nahodha Juma Kaseja ambaye ametemwa katikia kikosi hicho kwa sababu hakuwa na timu timu msimu huu, Kelvin Yondani beki wa kutegemewa wa mabingwa wa soka nchini Yanga ndiye aliyechukua nafasi ya Kaseja kuongoza wachezxaji wenzake ndani na nje ya uwanja. Tuna imani kubwa kuwa timu hiyo inaweza kufanya vizuri hatimaye kurejea na kombe, Watanzania wamepoteza imani kwa timu yao hiyo hasa kutokana na matokeo mabaya iliyokuwa ikiyapata siku za hivi karibuni, kuwepo kwa wachezaji wawili wa kutumainiwa Mbwana Ally Samatta na Thomas Ulimwengu ambao wanaichezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kunaweza kuleta matumaini. Lakini pia huu

UMEISIKIA HII! MICHAEL JACKSON ALIKUWA KIKOJOZI.

Picha
Kwenye mahojiano yake ya kwanza mara baada ya kuachiwa toka gerezani kwa kuhusishwa na kifo cha nguli wa muziki wa pop duniani Michael Jackson, Dokta Conrad Murray alielezea kwenye mahojiano aliyofanya na The Mail kwamba, Michael hakuwa baba wa hata mtoto wake mmoja, aliathiriwa na madawa kiasi cha kufikia hatua ya kuhitajika kuwa anavaa condom sababu mkojo ulikuwa unatoka wenyewe kwenye uume wake. “Unataka kufahamu ni kwa kiasi gani mimi na Michael kwa vile tulikuwa karibu? Nilikuwa nikishukilia uume wake kila usiku. Nilikuwa namvalisha condom sababu mkojo wake ulikuwa ukitoka wenyewe. Michael alikuwa hajua namna ya kuvaa condom, hivyo ilinibidi niwe namvallisha. Kilikuwa ni kitu cha kipekee sana ila aliniamini mimi. Sikumuuwa Michael Jackson, aliathiriwa na madawa, Michael Jackson kwa bahati mbaya alimuuwa Michael Jackson, naamini aliamka na kuamua kufanya aliyozoea kufanya, akajidunga sindano haraka ambayo ilisababisha kumpeleka kwenye hali iliyomfika.’’ Alikuwa kwenye majanga mwi

KILIMANJARO STARS YAENDA KENYA, YONDANI NAHODHA MPYA.

Picha
KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Bara, Kilimanjaro Stars , Kim Pouslen amemtambulisha beki Kevin Yondan kuwa Nahodha mpya wa timu hiyo, anayechukua nafasi ya Juma Kaseja aliyeachwa kwenye kikosi hicho kinachoondoka jioni ya leo kwenda Nairobi, Kenya kushiriki michuano ya Kombe la Challenge inayoanza kutimua vumbi Novemba 27 mwaka huu. Stars imeagwa leo mchana kwa hafla fupi kambini kwao katika hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam na kukabidhiwa bendera na Katibu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Henry Lihaya. Kocha wa Stars, Mdenmark Poulsen amesema kwamba anakwenda Kenya kwa lengo moja kubwa kupigana kukata tiketi ya kucheza Robo Fainali kutoka kwenye Kundi lao B, na baada ya hapo mapambano mengine yatafuatia. Amesema anafurahi wachezaji wake wako tayari sana kwa ajili ya mashindano hayo na wamemuahidi kufanya vizuri.

JAHAZI LA MAN UNITED LAZIDI KUZAMA.

Picha
MCHEZAJI Kim Bo-kyung aliyetokea benchi alifunga bao dakika ya mwisho na kuinusuru Cardiff kuzama nyumbani kwa kulazimisha sare ya 2-2 dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu England, Manchester United. Wayne Rooney, ambaye alistahili kupewa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu mapema kwenye mchezo huo, aliifungia United bao la kuongoza dakika ya 15 kabla ya Fraizer Campbell kusawazisha dakika ya 33. Kona maridadi ya Rooney iliunganishiwa nyavuni na Patrice Evra dakika ya 45 na United ikaonekana kama itashinda, lakini Kim akaja kuharibu mambo mwanzoni mwa dakika nne za nyongeza akimalizia mpira wa adhabu wa Peter Whittingham.

PATA PICHA ZA MAZOEZI YA KLABU YA YANGA YALIYOANZA RASMI LEO.

Picha
Mabingwa wa soka nchini Yanga leo asubuhi wameanza mazoezi yao rasmi kwa ajili ya maandalizi yao ya mechi ya Ngao ya Hisani dhidi ya hasimu wao Simba mechi inayofahamika kama mtani jembe. Mabingwa hao wanaonolewa na Mholanzi Ernie Brandts wa,eanza mazoezi yao huku kipa wao mpya Juma Kaseja aliyesajiliwa hivi karibuni akitokea kwa mahasimu wao Simba alionekana kuwa furaha. Tayari mabingwa hao wameweka mikakati yao ya kutetea ubingwa wao walioutwaa msimu uliopita huku wakitaka kufika mbali katika ligi ya mabingwa barani Afrika. Pata picha zote za mazoezi kwa niaba ya BIN ZUBEIRY BLOG

YANGA YAMKATA MAINI KABURU, YAMALIZANA NA KELVIN YONDANI.

Picha
KLABU ya Yanga SC imemuongezea Mkataba wa miaka miwili beki wake Kevin Patrick Yondan, ambaye alikuwa ananyemelewa na klabu yake ya zamani, Simba SC. Yondan alisaini Mkataba huo juzi mjini Dar es Salaam na sasa atakuwa mali ya Yanga hadi Juni 2016. Juni mwakani, Yondan alikuwa anamaliza Mkataba wake wa awali Yanga SC wa miaka miwili na kwa ndoa mpya- maana yake kuna uwezekano mchezaji huyo bora wa Ligi Kuu msimu uliopita atamalizia soka yake Jangwani. Mambo yanamuendea vizuri Yondan tangu ajiunge na Yanga SC, kwani mbali na kushinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, pia leo ameteuliwa kuwa Nahodha wa kikosi cha Bara, Kilimanjaro Stars. Kocha wa Stars, Kim Pouslen amemtambulisha Yondan kuwa Nahodha mpya wa timu hiyo, anayechukua nafasi ya Juma Kaseja aliyeachwa kwenye kikosi hicho kinachoondoka jioni ya leo kwenda Nairobi, Kenya kushiriki michuano ya Kombe la Challenge inayoanza kutimua vumbi Novemba 27 mwaka huu.

RAGE AMTUNISHIA MISULI MALINZI, AMPA ULAJI WAMBURA.

Picha
Siku moja baada ya Shirikisho la Soka nchini (TFF), kumwagiza Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura wa klabu ndani ya siku 14 kuanzia juzi, Mbunge huyo wa Tabora Mjini amepuuza agizo hilo huku akikwea pipa na kwenda Uingereza. Juzi Rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema wameamua kutoa agizo hilo baada ya kubaini kuna mgogoro katika klabu baada ya kupokea barua mbili; moja kutoka Kamati ya Utendaji ikielezea kumsimamisha Rage, na nyingine kutoka kwa mwenyekiti huyo ikielezea kutotambua kusimamishwa kwake. Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Simba zilizopo mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam, Rage alisema 'maagizo ya uongozi mpya wa TFF hayatekelezeki'. Alisema TFF ilipaswa kutoa adhabu kwa 'wanamapinduzi' waliokutana Jumatatu jijini Dar es Salaam na kumsimamisha kinyume cha Katiba ya Simba Ibara za 22 na 28 (Muundo wa Kamati ya Utendaji ya Simba na mamlaka ya kuitisha Mkutano Mkuu wa Dharura) na Katiba

MKOLA MAN KUITANGAZA TANGA.

Picha
Staa anayechipukia kwenye kiwanda cha muziki bongo Christopher Mhenga ukipenda Mkola Man ameapa kuitangaza Tanga katika ramani ya muziki tofauti na wanamuziki wengine waliopata kutamba kupitia mkoa huo uliosifika kwa mengi. Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, Mkola Man amesema kuwa wanamuziki wengi waliopata kung'ara wanaotokea mkoa huo walishindwa kuitangaza vema baada ya kukimbilia jijini Dar es Salaam, lakini yeye ataendelea kuitangaza Tanga. Kwa sasa msanii huyo anatamba na wimbo wake mpya uitwao 'Kilevi Changu' na tayari umeanza kusikika baadhi kwenye vituo vya redio, ila mikakati yake ni kuendelea kubakia jijini Tanga na kutokimbilia Dar es Salaam. (Mkola Man wa pili kutoka kushoto, akiwa na wasanii wenzake jijini Tanga hivi karibuni) 'Unajua wanamuziki wengi waliopata kutikisa hapa nchini ambao wanatokea Tanga wameshindwa kuitangaza vema, hasa ukiangalia kundi la Wagosi wa Kaya wenyewe asili yao Tanga lakini walijikita Dar es Salaam, hivyo hivyo kw

WALCOT KUREJEA UWANJANI LEO.

Picha
Theo Walcott huenda akaichezea Arsenal siku ya leo ikiwa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha zaidi ya miezi miwili baada ya kupona kutokana na majeruhi ya tumbo. Walcott yumo katika kikosi cha kupambana na klabu yake ya zamani Southampton siku ya Jumaamosi. Walcott mwenye umri wa miaka 24-aliumia katika pambano la ligi dhidi ya Stoke September 22 baada ya kutegua maumivu aliyopata katika pambano la siku nne zilizotangulia dhidi ya Marseille. "hajachezea hata kikosi cha akiba lakini nitamjumuisha katika kikos ikamili cha Jumaamosi '' alisema kocha Arsene Wenger.

WAKATI SIMBA WAKIZOZANA NA RAGE, BIN KLEB APIGA BAO LA TATU.

Picha
Kukiwa na tetesi kwamba viongozi wa Simba wapo katika mpango wa kuwanyemelea beki Kelvin Yondani na kiungo Simon Msuva kwa ajili ya kuwasajili msimu ujao, uongozi wa Yanga umeanza mchakato wa kuwapa mikataba mipya wachezaji hao. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya klabu ya Yanga, Abdallah Bin Kleb alisema wameanza mchakato wa kuwasainisha mikataba mipya wachezaji hao. Bin Kleb alisema kuwa timu hiyo bado inahitaji huduma za wachezaji hao hivyo watawasainisha mikataba mipya muda mfupi kuanzia sasa ili waendelee kuitumikia Yanga. Mikataba ya Yondani, aliyesajili na Yanga akitokea Simba 2011, na Msuva aliyetoka Moro United inamalizika mwisho mwa msimu huu wa ligi kuu ya Bara.

MWISHO WA CHADEMA UMEFIKA, KABWE NA WENZAKE NJE.

Picha
Mgogoro ndani ya Chadema umezidi kupamba moto baada ya Kamati Kuu kuwavua uongozi Zitto Kabwe na Dk Kitila Mkumbo, huku Makamu Mwenyekiti Taifa, Said Arfi akiandika barua ya kujiuzulu. Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, wakati Dk Mkumbo amevuliwa ujumbe wa Kamati Kuu. Wawili hao wanatuhumiwa kukisaliti chama. Taarifa zilisema hoja ya kukisaliti chama pia ilimkumba Arfi akidaiwa kumwezesha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupita ubunge bila kupingwa, katika uchaguzi mkuu uliopita na ndiyo sababu ya kuamua kuachia ngazi nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa. Mbali ya kuwavua uongozi Zitto na Dk Mkumbo, pia Kamati Kuu imewapa siku 14 wajieleze kwa nini wasifukuzwe uanachama. Kwa uamuzi huo Zitto amebaki na wadhifa wa ubunge wake wa Kigoma Kaskazini na wadhifa mwingine kwenye Kamati ya Bunge. Zitto azungumza Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho, Zitto alisema, “Sina cha kueleza, kikao kilikwenda vizuri na taari

CARRICK AFUNGA NDOA MPYA MAN UNITED.

Picha
KIUNGO Michael Carrick amesaini Mkataba mpya Manchester United, ambao utamfanya adumu Old Trafford hadi mwaka 2015. Kiungo huyo kwa sasa yuko nje ya Uwanja kwa sababu ya majeruhi, lakini ameemelezea furaha yake kwa kuongeza Mkataba na mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England. Carrick amesema: "Ni babu kubwa kuongeza Mkataba wangu katika klabu hii kubwa. Hakika nafurahia soka yangu.

RAGE AMFUNIKA HANSPOPE UWANJA WA NDEGE, ATAMBA YEYE BADO MWENYEKITI SIMBA.

Picha
MWENYEKITI wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage aliwasili Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam jana usiku akitokea Sudan na kusema kwamba; “Mimi bado Mwenyekiti wa Simba SC,”. Rage aliwasili kwa ndege ya shirika la Kenya saa 1:40 usiku na kutokea mlango wa Watu maalum (VIP) ambako alilakiwa na wanachama zaidi ya 200, waliokuwa kwenye mabasi sita aina ya Coaster. “Umati huu uliokuja hapa ni kielelezo tosha sana kwamba kiasi gani wanachama wa Simba wana imani na Mwenyekiti wao, sasa leo sitasema mengi, nitakuwa na Mkutano na Waandishi wa Habari kesho saa saba mchana makao makuu ya klabu(Msimbazi),”alisema Rage. Alipoulizwa kuhusu kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika Jumatatu na kutangaza kumsimamisha, Rage alisema; “Kwa mujibu wa Katiba ya Simba, Kamati ya Utendaji haina uwezo wa kumsimamisha Mwenyekiti, usinimalizie utamu, njoo kesho mchana Msimbazi,”alisema. Watu zaidi ya 200 walifika Uwanja wa ndege tangu saa 11 na ushei jioni ya jana kumsubiri R

VILLA SQUAD YAZOA MASTAA WA SIMBA, YANGA.

Picha
Uongozi wa timu ya soka ya Villa Squad inayoshiriki ligi daraja la kwanza umetuma barua kwa Bandari ya Mombasa, Kenya kwa ajili ya kuomba kibali cha kumsajili kiungo Mohamed Banka anayetarajia kuichezea kwenye mzunguko wa pili. Banka anatarajia kuichezea Villa Squad katika mzunguko wa pili wa ligi hiyo unaotarajia kuanza Februari 8. Akizungumza jana, katibu wa Villa Squad Mbarouk Kasanda alisema barua hiyo wameituma jana kwa uongozi wa timu hiyo. "Tumetuma barua kwa ajili ya kuomba kibali cha Banka, tuna imani watatupatia," alisema Kasanda. Alisema Villa haijaanza mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mzunguko wa pili kutokana na wachezaji kuwa likizo lakini jitihada za kujiimarisha, ikiwa ni pamoja na usajili zinaendelea. Alisema kwa mujibu wa ratiba ya kocha mkuu wa timu hiyo, wachezaji wataanza mazoezi mwishoni mwa mwezi.

P-SQUARE KUWASHA MOTO DAR LEO.

Picha
Mapacha Peter na Paul Okoye wanaounda kundi la wanamuziki wawili la P-Square la Nigeria wameahidi kutoa shoo kali kwa mashabiki katika onyesho la leo kwenye viwanja vya Leaders Club, jijini, ikiwemo kutumbuiza kwa saa mbili mfululizo bila kupumzika. Kundi la P-Squere ambalo linatikisa ulimwengu kwa singo ya 'Pesonaly', limekuja nchini kwa mwaliko wa kituo cha televisheni cha EATV na East Africa Redio; chini ya udhamini mkuu wa Vodacom na kapmuni za Hennessy na Mastermind. Katika onyesho hilo, P-Square watasindikizwa na Lady Jaydee, Prof Jay, Jo Makini na Ben Pol ambao wote kwa pamoja jana waliahidi kutoa burudani ya kiwango cha juu katika kuchuana na wageni hao. Wakizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Peter alisema wamekuja nchini kutoa "shoo kali kwa mashabiki wa muziki na Watanzania wote kwa ujumla." P-Square wanathamini muziki wa Afrika na ndio maana wanajitahidi kila siku kupiga staili ya kiafrika, alisema Peter, kwa ajili ya kuendeleza muziki kwa Bara

FILAMU YA SIMBA YAZIDI KUNOGA: MZEE KINESI, HANSPOPE NAO WASIMAMISHWA.

Picha
MWENYEKITI aliyesimamishwa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage atarejea nchini Ijumaa na kulakiwa na mamia ya wanachama na ataitisha Mkutano Mkuu, ambao utafanyika Jumapili hii. Na katika Mkutano huo, Rage amepanga kuwasimamisha Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji na baada ya hapo atasafiri kwenda nje ya nchi. Wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliobaki Simba SC ni Joseph Itang’are ‘Kinesi’, Said Pamba, Ibrahim Masoud ‘Maestro’, Swedi Nkwabi na Zacharia Hans Poppe. Habari za kiuchunguzi, ambazo tumezipata zimesema kwamba, Rage amekwishawasiliana na wafuasi wake wa Dar es Salaam na wameandaa mapokezi makubwa kwake atakapokuwa anawasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Ijumaa. Baada ya hapo, Rage ataitisha Mkutano Mkuu wa dharula Jumapili na siku hiyo atawasimamisha Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji.

CRISTIANO RONALDO AKARIBIA TUZO YA BALLON D'OR

Picha
KATIKA usiku ambao Cristiano Ronaldo alifunga mabao matatu matamu, hat-trick iliyoipeleka Ureno Fainali zijazo za Kombe la Dunia mwakani, FIFA imeongeza muda wa kupiga kura za kuchagua mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, Ballon d’Or. Zoezi la upigaji kura lilifungwa Novemba 15, lakini Manahodha, Makocha Vyombo vya Habari ambavyo hazijawasilisha kura zao, wamepewa siku tisa zaidi kuwasilisha orodha zao za wachezaji watatu wa kwanza. FIFA, ambayo imethibitisha uamuzi wake leo asubuhi, pia imethibitisha kwamba wale ambao tayari wamekwishapiga kura wanaweza kurekebisha majina yao na kuwasilisha tena. Washindani: Nyota wa Barcelona, Lionel Messi (kushoto) amekwishashinda tuzo nne za Ballon d'Or na Franck Ribery wa Ufaransa na Bayern Munich (kulia) anapewa nafasi ya kufanya vizuri baada ya kushinda mataji matatu akiwa Bayern Munich.

POULSEN AITA SURA MPYA STARS.

Picha
KOCHA Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 23 watakaoshiriki michuano ya Kombe la CECAFA Challenge inayofanyika nchini Kenya kuanzia Novemba 27 mwaka huu. Kilimanjaro Stars iliyotwaa kombe hilo mara ya mwisho mwaka 2010 chini ya Kocha Jan Poulsen, na ambayo imepangwa kundi B katika michuano ya mwaka huu itacheza mechi yake ya kwanza Novemba 28 mwaka dhidi ya Zambia kwenye Uwanja wa Machakos. Wachezaji wanaounda kikosi hicho cha Tanzania Bara ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo Mapunda (Gor Mahia, Kenya) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Michael Pius (Ruvu Shooting) na Said Moradi (Azam). Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Ramadhan Singano (Simba) na Salum Abubakar (Azam). Safu ya ushambuliaji inaundwa na Elias Maguli (Ruvu Shooting), Faridi Musa (Azam), Joseph Kimwaga (A

DOLA 125,000 KUDHAMINI CHALENJI KENYA.

Picha
SERIKALI ya Kenya imetoa dola za Kimarekani 125,000 (zaidi ya Sh. Milioni 140) kudhamini michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge inayoanza wiki ijayo mjini Nairobi. Hili ni ongezeko la dola za Kimarekani 600,000 (zaidi ya Sh. Milioni 900) zinazotokana na mauzo ya haki za matangazo ya Televisheni yatakayohusu mechi zote 27 za mashindano hayo. Gavana wa Machakos, Alfred Mutua naye ametoa Sh. Milioni 5 za Kenya zaidi ya Sh. Milioni 11 za Tanzania kudhamini mashindano hayo, wakati wenzake kutoka Nairobi na Kisumu wametoa Sh Milioni 10 za Kenya, zaidi ya Sh. Milioni 22 za Tanzania. Kampuni ya Coca Cola pia imetoa Sh Milioni 6.5 za Kenya (Milioni 5 taslimu na vinywaji vyenye thamani ya Sh. Milioni 1.5), wakati kampuni ya Bima ya UAP itatoa Sh Milioni 5.5 za Kenya (Milioni 2.5 fedha taslimu nan a Milioni 3 kwa ajili ya bima za wachezaji na marefa wote) katika mashindano hayo.

BREAKING NEWZZ!!! BABU SEYA KUFIA JELA,KILICHOJIRI MAHAKAMANI HIKI HAPA

Picha
  Mwanamuziki Nguza Viking na mwanaye Johnson Nguza 'Papii Kocha'.   Ile hukumu ya rufaa ya mwanamuziki Nguza Viking na mwanaye Johnson Nguza 'Papii Kocha' imewarejesha jela maisha baada ya hoja za serikali za kukazia hukumu kuzidi zile za upande wa utetezi.   Babu Seya na Papii Kocha walihukumiwa kifungo cha maisha jela mwaka 2004 baada ya kupatikana na hatia ya kuwanajisi watoto wa Shule ya Msingi, Mashujaa, Sinza jijini Dar ambapo wamekuwa wakikata rufaa mara kwa mara lakini wakagonga mwamba. Hukumu hii ya rufaa ndiyo ya mwisho kusikilizwa.

MAKALA: HANSPOPE ILIBIDI AENDE NA RAGE.

Picha
Na Prince Hoza, 0772 954167 MWANZONI mwa wiki hii kamati ya utendaji ya klabu ya Simba ilitangaza kumsimamisha mwenyekiti wake Alhaj Ismail Aden Rage kwa madai ya kuiendesha Simba kama mali yake binafsi, pia ilitangaza kuwafuta kazi makocha wa timu hiyo Abdallah Kibadeni 'King' na msaidizi wake Jamhuri Kihwelo 'Julio'. Habari hizo zilionekana kushtua zaidi isitoshe wapenzi na mashabiki wa Simba walishuhudia usajili wa wachezaji wawili wa timu ya taifa ya Zanzibar Awadh Juma na Badru Ali, Usajili huo ulifanywa na mwenyekiti wa Simba Alhaj Rage. Hivyo kitimutimu kilichokuja kutokea kiliweza kumshangaza kila mpenda michezo nchini, licha ya mapinduzi hayo yaliyofanywa na kamati ya utendaji chino ya makamu mwenyekiti wa Simba Joseph Itang'are au mzee Kinesi yaliweza kuendana na mabadiliko mengine katika benchi la ufundi la timu hiyo. Kikubwa kilichopelekea Simba kuingia kwenye malumbano yanayopelekea kusimamishwa kwa mwenyekiti wake ni matokeo mabaya katika msima

MUME WA MAREHEMU NYAWANA YAMKUTA MAKUBWA.

Picha
Kaisi Musa Kaisi (Pichani) mume wa marehemu Nyawana ambaye alikuwa akitamba kwenye muziki wa taarabu hapa nchini hatimaye yamemkuta makubwa baada ya kutoswa na kundi la wanasalamu wenzake ambao kwa sasa wana umoja wao unaofahamika kwa jina la Umoja wa Wanasalamu mkoa wa Dar es Salaam na Pwani. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari hizi ambacho ni rafiki wa karibu na Kaisi Musa Kaisi ambaye ni mmoja kati ya wanasalamu maarufu hapa nchini kupitia vituo vya redio pamoja na magazeti alijikuta akitengwa na wenzake katika msiba wa marehemu mke wake aliyefariki kwa kuugua malaria. Taarifa kamili zinasema kuwa Kaisi amekuwa na tabia ya kutoudhuria misiba ya wanasalamu wenzake huku ikidaiwa umaarufu ndio umemfanya ajione staa, chanzo chetu kiliendelea kusema kuwa wanasalamu wamekuwa na utaratibu mzuri wa kuudhuria misiba ya wadau wao hata kama si maarufu. Kupitia afisa wao wa habari Salum Mfunga 'Rais wa mafukara Tz' amethibitisha habari hizo kuwa wanasalamu kwa pamoja wameamua

PHIRI KUIONGOZA ZIMBABWE MCHANA HUU KUTUA ARDHI YA BONGO.

Picha
KIKOSI cha Zimbabwe kinawasili leo mchana (Novemba 18 mwaka huu) kuikabili Taifa Stars katika mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)- FIFA Date itakayofanyika kesho (Novemba 19 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Msafara wa timu hiyo ukiwa na watu 30 utatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 8 kamili mchana kwa ndege ya Kenya Airways yenye mruko namba KQ 484 kupitia Nairobi. Kocha wa timu hiyo Ian Gorowa atazungumza na waandishi wa habari mara baada ya timu hiyo kutua JNIA. Kiongozi wa msafara wa timu ya Zimbabwe ni John Phiri. Wachezaji wanaounda kikosi hicho ni makipa; Frankson Busire, Maxwell Nyamupangedengu na Tapiwa Kapini. Mabeki ni Carrington Nyadombo, Felix Chindungwe, Innocent Mapuranga, Nkosana Siwela, Ocean Mushure na Patson Jaure. Viungo ni Isaac Masami, Kundakwashe Mahachi, Milton Neube, Misheck Mburayi, Obey Mwenehari na Silas Dylan Songani. Washambuliaji ni Gerald Ndlovu, Lot Chiungwa, Nqobizitha Masuku, Simba

IVO MAPUNDA ATEMWA GOR MAHIA

Picha
Tetesi za kutua kwa kipa wa zamani wa Moro United, Prisons na Yanga Ivo Mapunda ambaye anaichezea Gor Mahia ya Kenya katika klabu ya Simba huenda zikatimia baada ya kipa huyo kutokuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya Kenya. Ivo Mapunda anatajwa kuwemo katika kikosi cha Simba kinachojiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Tanzania bara, taarifa zilizothibitishwa na chanzo chetu cha habari zinasema kuwa kipa huyo mzoefu aliyeitwa kwenye timu ya taifa, Taifa Stars inayojiandaa kucheza na Zimbabwe kesho hatoongezewa mkataba mwingine na Gor Mahia. Kwa sasa Ivo anasugua benchi kama kipa namba mbili hivyo uongozi wa Gor Mahia umeamua kutomuongezea mkataba mwingine mchezaji huyo badala ya huu wa mwanzokumalizika rasmi, Ivo ameiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa Kenya lakini amejikuta katika wakati mgumu hasa anapoanzia benchi. Kulingana na taarifa hiyo inaweka wazi nafasi yake kubwa kutua kwenye ligi kuu ya bara na Simba inatajwa kama timu pekee

AJALI YA NDEGE YAUA 50 URUSI.

Picha
Ndege ya abiria imeanguka katika uwanja wa ndege katika mji wa Kazan, nchini Urusi na kuua watu wote 50 waliokuwa katika ndege hiyo.Ndege hiyo aina ya Boeing 737 iliruka kutoka mji wa Moscow na ilikuwa ikijaribu kutua lakini ikawaka moto saa moja usiku kwa saa za huko. Wizara ya matukio ya dharura imesema kulikuwa na abiria 44 na wafanyakazi sita wa ndege hiyo ya shirika la Tatarstan Airlines. Wachunguzi wanajaribu kuona kama kulikuwa na makosa ya kiufundi au huenda ya kibinadamu yaliyosababisha ajali hiyo. Afisa wa kamati ya uchunguzi Vladimir Markin ameiambia Televisheni moja nchini Urusi, Rossiya 24 TV, kwamba wataalam wanachunguza kubaini kama ajali hiyo imesababishwa na matumizi ya mafuta mabaya, au hali mbaya ya hewa. Mvua ilikuwa ikinyesha katika mji wa Kazan wakati ndege hiyo ilipoanguka. Kwa mujibu wa orodha rasmi ya wasafiri wa ndege hiyo, miongoni mwa waliokufa ni Irek Minnikhanov, mtoto wa kiume wa rais wa Jamhuri ya Tatarstan,nchini Urusi.

RAGE AMWEKA KANDO HANSPOPE SIMBA.

Picha
Mwenyekiti wa Simba SC Alhaj Ismail Aden Rage inaonekana kama ameamua kumweka kando mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu hiyo Zackaria Hanspope katika shughuri nzima za usajili kutoka na maneno yao kupishana huku vitendo vikionekana kufanywa na Rage badala ya Hanspope. Hivi karibuni Hanspope alisikika kwenye kituo kimoja cha redio akisema klabu yake haioni mchezaji wa kumuongeza katiia dirisha dogo hasa anayetokea hapa nchini kutokana na wote viwango vyao kufanana, pia amedai Simba haina mpango wa kusajili katika dirisha dogo. Tofauti na kauli yake Hanspope ambaye ndiye mwenye dhamana ya kushughurikia usajili katika klabu hiyo, ambapo mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage alionekana akiwasainisha wachezaji wawili Awadh Issa toka Mtibwa na Badru Ally wa Canal Suez ya Ligi Kuu ya Misri.

SIMBA YASAWAZISHA MBILI ZA YANGA.

Picha
Klabu ya Simba imezidi kujiimarisha kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara baada ya kusajili vifaa vipya viwili, Awadh Issa, kutoka Mtibwa Sugar ya Manungu, Morogoro na Ally Badru aliyekuwa anaichezea Canal Suez ya Misri, hivyo inakuwa kama imesawazisha baada ya watani zao kusajili wachezaji wawili pia. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema wachezaji hao kila mmoja amesaini mkataba wa miaka miwili na wanaamini uwapo wao utasaidia kukiimarisha kikosi chao ambacho kimemaliza mzunguko wa kwanza kikiwa katika nafasi ya nne. Mtawala alisema tayari klabu yao iko katika mazungumzo na timu nyingine za Ligi Kuu ya Bara ili kuwahamishia wachezaji wengine kwa mkopo. "Tuna nafasi moja lakini hilo si tatizo, kuna vijana wetu ambao bado wanahitaji uzoefu na kwetu Simba wamekosa nafasi ingawa ni wazuri, tutawapeleka kwa mkopo katika baadhi ya timu ambazo zimeonyesha nia ya kuwatumia," alieleza Mtawala.

CAMEROON YAIDUWAZA TUNISIA.

Picha
TIMU ya taifa ya Cameroon imekata tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuifumua kwa mabao 4-1 Tunisia jioni ya leo kwenye Uwanja wa Ahmadou Ahidjo mjini Yaounde, Cameroon. Mabao ya Pierre Webo dakika ya nne, Benjamin Moukandjo dakika ya 30 na mawili ya Jean Makoun dakika za 66 na 86 yametosha kuwahakikishia Simba Wasiofungika kucheza fainali hizo kwa mara ya saba. Bao pekee la Tunisia lilifungwa na Ahmed Akaichi dakika ya 50. Kocha wa Cameroon, Volker Finke alifanya mabadiliko matatu katika kikosi chake kutoka kile kilichotoa sare ya bila kufungana na Tunisia katika mchezo wa kwanza. Bennoit Assou-Ekotto, Stephane Mbia na Benjamin Moukandjo walianza kwenye kikosi cha kwanza badala ya Nyom, Nounkeu na Joel Matip. Samuel Eto’o alianza katika safu ya ushambuiaji pamoja na mkongwe Pierre Webo. Ruud Krol, naye kwa upande wake alibadilisha wachezaji wawili baada ya kushindwa kupata bao mjini Rades mwezi uliopita. Karim Haggui na Fakhreddine Ben Youssef walichukua nafasi za

UHURU SELEMAN ARUDISHWA SIMBA.

Picha
WINGA Uhuru Suleiman Mwambungu ameamua kurejea klabu yake ya Simba SC kumalizia Mkataba wake wa miezi saba kutoka Coastal Union ya Tanga alikopelekwa kwa mkopo mwanzoni mwa msimu. Uhuru aliyekwenda Coastal akitokea Azam FC alikocheza pia kwa mkopo kwa nusu msimu, amesema jana usiku kwamba tayari amekwishafuata taratibu za kumrejesha klabu yake. Amesema amekwishauarifu uongozi wa Coastal ambao umeandika barua ya kumrejesha Simba SC baada ya kuitumikia vizuri klabu hiyo katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu. “Kama utakumbuka nilitolewa kwa mkopo Simba SC kwenda Azam FC Desemba mwaka jana kwa sababu sikuwa fiti, nilikuwa nimetoka kwenye maumivu. Lakini namshukuru Mungu nimefika Azam nimepata malezi mazuri na nimecheza kidogo hadi nimefanikiwa kuwa fiti,”.

GERRARD AMPUUZA FERGUSON.

Picha
Nahodha wa Uingereza Steven Gerrard amepuuzilia mbali madai ya meneja wa zamani wa Manchester United Alex Ferguson kwamba kiungo huyo wa kati wa Liverpool si “mchezaji nyota.” Ferguson alitoa madai hayo kwenye tawasifu yake, ambayo ilichapishwa mwezi uliopita, lakini Gerrard anasema majaribio ya raia huyo wa Scotland ya kutaka kumnunua ni thibitisho tosha kwamba alithamini sana uwezo wake. “Sikizeni, ana haki ya kuwa na maoni yake,” Gerrard aliambia jarida la Jumanne la gazeti la Uingereza la Daily Mail. "Mimi ni shabiki wake; yeye ni mmoja wa mameneja bora zaidi duniani. Sipotezi usingizi kutokana na hilo. Katika maisha yangu ya soka, nimepokea pongezi kutoka kwa watu wa kila aina – yeye akiwa mmoja wao – na huwa nazipokea. “Nimepokea pongezi za kushangaza kutoka kwake na alijaribu kuninununua, wakati mmoja. Labda hata mara mbili. “Kwangu, la muhimu zaidi ni lile (meneja wa Liverpool) Brendan Rodgers na (meneja wa Uingereza) Roy Hodgson wanafikiria. Ninafikiri wamefurahishwa sa

MESSI AJA NA MAAJABU MAPYA.

Picha
Lionel Messi atafanya kila awezalo kuhakikisha anapona jeraha la misuli ya paja ambalo alipata Jumapili na ambalo litamfanya akae nje ya soka kwa kati ya wiki sita na nane, mchezaji huyo wa Argentina ambaye pia ndiye Mchezaji Bora wa Mwaka Duniani alisema Jumanne. Hayo ndiyo matamshi yake ya kwanza hadharani tangu aondoke kwenye mechi mapema wakati wa ushindi wa Barca wa 4-1 katika Real Betis. Messi alisema lengo lake kuu ni kurejea mchezoni mapema iwezekanavyo na kusaidia mabingwa hao wa Uhispania katika kutafuta kikombe. "Kama wengi wenu mjuavyo, wiki chache zijazo, nitakuwa nikifanya kila liwezekanalo nipone jeraha nililopata majuzi,” Messi alisema kwenye ukurasa wake wa Facebook. "Kwangu, ni masikitiko kwamba sitaweza kuchezea timu yangu kwa sasa,” akasema mchezaji huyo wa umri wa miaka 26. "Kwa sasa, la muhimu zaidi ni kupata nafuu vyema ili niweze kusaidia wachezaji wenzangu na kuwazawadi nyote kwa uungaji mkono ambao mmneipa kwa njia bora zaidi niwezayo, kucheza

USHABIKI WAMPONZA SHABIKI WA ARSENAL

Picha
Shabiki sugu wa klabu ya Arsenal katika wilaya ya Iganga, Mashariki mwa Uganda anatafuta nyumba mpya baada ya kupoteza nyumba yake kwenye dau aliyowekeana na mtu mwingine kuhusu mechi kati ya klabu mbili za Uingereza, Arsenal na Manchester United. Kabla ya miamba hao wawili kumenyana Jumapili katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza, Henry Dhabasani aliweka dau nyumba yake ya vyumba viwili kati yake na Rashid Yiga kwamba Arsenal wangeshinda mechi hiyo, gazeti la Observer la Uganda liliripoti. Kwa upande wake, Yiga aliweka dau gari lake ina ya Toyota Premio pamoja na mkewe kwamba Manchester United wangeshinda. “Wawili hao waliwekeana dau kwa maandishi, huku viongozi wa eneo hilo na mashabiki wakishuhudia mkataba huo,” gazeti hilo linasema. Dhabasani, ambaye ana wake watatu na watoto watano, alizirai mwishoni mwa mechi hiyo baada ya Arsenal kushindwa 1-0.

MCHAWI WA DIAMOND KUWABEBA NYOTA BONGO STAR SEARCH

Picha
Produza wa Hits mbalimbali za Bongo Fleva Sheddy Clever Aliyepewa nafasi ya kufanya Kazi na wasanii wawili wa Bongo Star Search 2013 ambao ni Emanueli na Mandela amepania kuwatoa kisanii wakali hao ambao wamekwisha anza mchongo wa kurecods Ngoma Moja moja kwa kila mtu ndani ya Studio za Burn Records pande za Tabata. “Mimi na wasanii wa Epiq Bongo Star Search Emanueli na Mandela katika Studio ya Burn Record tukifanya yetu”Alifunguka Sheddy Kwa wale ambao wanamtambua Sheddy Clever inajulikana kuwa ni mkali wa kutengeneza Ngoma za kuimba imba ambapo katika siku za karibuni alitengeneza Ngoma ya My Number 1 ya Diamond Platnum na Remix ya ngoma hiyo aliyopowe shavu Davido kutoka Nigeria.

IVO MAPUNDA AJIPELEKA SIMBA.

Picha
KIPA aliyerejeshwa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars baada ya miaka mitano, Ivo Mapunda amesema Mkataba wake na Gor Mahia ya Kenya unaisha mwezi ujao hivyo Simba SC ambao wanatafuta kipa kama wameridhishwa na uwezo wake, anawakaribisha kwa mazungumzo. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi baada ya mechi ya jana baina ya Taifa Stars na timu ya pili ya taifa, Future Young Taifa Stars iliyoshinda 1-0, Ivo alisema kwamba milango iko wazi kwamba Simba SC kumfuata kwa mazungumzo. “Ndiyo najua Simba SC wanatafuta kipa, mimi nasema kama wameridhishwa na uwezo wangu, waje tuzungumze na tukikubaliana nitawafanyia kazi nzuri,”alisema. Ivo aliidakia Stars kwa dakika 45 kipindi cha pili jana akimpokea Ally Mustafa ‘Barthez’ aliyefungwa bao hilo la Elias Maguril aliyeunganisha pasi ya Juma Luizio. Mapema juzi, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe alisema kwamba wanatafuta kipa atakayekwenda kuwa pamoja na makipa wazawa, Abuu Hashimu na Andrew Ntalla, kwa kuwa wan

STEWART HALL WA AZAM AULA TFF.

Picha
Kauli zinazotolewa na aliyekuwa kocha wa Azam FC, Stewart Hall kuhusu kuendelea kukaa nchini licha ya kumalizana na klabu hiyo, zimeanza kuzua maswali mengi huku baadhi ya wadau wa michezo wakidai Muingereza huyo ataingia katika uongozi mpya wa Shirikisho la Soka (TFF). Hall, kwa makubaliano na uongozi wa Azam, aliachana na Kikosi cha 'Wanalambalamba' mara tu baada ya mchezo wao wa mwisho wa kufunga mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom walioshikwa kwa sare ya mabao 3-3 dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wao wa Azam Complex uliopo nje kidogo mwa Jiji la Dar es Salaam. "Naondoka Azam baada ya kupata ofa kubwa hapa Tanzania, nakuahidi kwamba nitaendelea kuwa hapa. Ninachotaka kufanya ni kitu ambacho nilikuwa nakihitaji kukifanya kwa muda mrefu, lakini sasa nimekipata," alisema Hall katika mazungumzo yake ya moja ya vyombo vya habari nchini jana.

PHIRI KOCHA MPYA SIMBA.

Picha
Uongozi wa Klabu ya Simba umeanza mazungumzo na aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mzambia Patrick Phiri, ili kuchukua mikoba ya Abdallah Kibaden 'King', imeelezwa jana jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia, zinaeleza kuwa Phiri akipatikana atasaidiana na kocha mkuu wa timu ya vijana ya Simba (Simba B), Selemani Matola. Chanzo hicho kiliweka wazi kuwa, jana kwa nyakati tofauti viongozi wa Simba walianza mazungumzo na Phiri pamoja na nahodha wao wa zamani, Matola wakimtaka kuisimamia timu hiyo iliyomaliza mzunguko wa kwanza ikiwa katika nafasi ya nne. Taarifa hizo zilifafanua kuwa, kulikuwa na mipango ya kuajiri kocha kutoka Urusi lakini hali ya ukata ndani ya klabu hiyo na mafanikio aliyoyapata Matola kwa kuandaa vijana yalisitisha mikakati ya kumleta mzungu huyo.

VIDIC ATOLEWA HOSPITALI.

Picha
Nahodha wa Manchester United, Nemanja Vidic, ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya kuugua mtikiso kwenye mechi yao ya Jumapili dhidi ya Arsenal, taarifa ya klabu hicho imesema. Vidic aliondoka uwanjani muda mfupi kabla ya muda wa mapumziko baada ya kugongana na kipa wake, David de Gea. Mlinda ngome huyo wa Serbia alipelekwa hospitalini kwa uchunguzi baada ya kupagawa kutokana na ajali hilo. "Nemanja Vidic ameruhusiwa kwenda nyumbani baada ya kuugua mtikiso,” taarifa hiyo ilidhibitisha. Vidic hatarajiwi kucheza tena hadi Novemba 24 wakati United watakapo tembelea Cardiff kwenye Ligi Kuu ya Uingereza ijapokuwa hakuna muda umetengewa kurejea kwake mazoezini.

MSANII CHIPUKIZI ALIA NA MAPRODYUZA.

Picha
Msanii chipukizi wa miondoko ya kizazi kipya nchini anayefahamika kwa jina la Tozi Mchafu (Pichani) hatimaye amefunguka kulia na maprodyuza hasa kwa tabia zao za kuwabagua wanamuziki chipukizi na kuwakatisha tamaa ya kuendelea na muziki huo. Akizungumza na Mambo Uwanjani hivi karibuni, Mchafu amedai kwamba amepata shida sana kurekodi wimbo wake mpya na umejaribu kusota kwa prodyuza zaidi ya miezi nane au tisa sasa, msanii huyo ameshangaa kuona maprodyuza kuwababaikia wasanii wenye majina wakati na wao walianza kama wao. 'Mimi nashangaa sana, maprodyuza tena hawa wanaoanza kujulikana sasa wanaonyesha ubinafai mkubwa kwetu chipukizi, inafikia hatua tunakata tamaa, utakuta unakwenda studio kurekodi unapewa taratibu zote na kulipia gharama lakini siku hadi siku unapigwa kalenda', alisema na kuongeza. 'Mimi yamenikuta katika studio moja (Jina tunalo) ambapo nimesota karibu miezi minaje au tisa, inafikia hatua msanii chipukizi unavunjika moyo, lakini uvumilivu wangu umewe

ALIYEMUUNGA MKONO MORSI ATUPWA JELA YA SOKA MISRI.

Picha
Mchezaji soka mmoja katika moja ya vilabu maarufu nchini Misri ametupwa nje ya mechi za klabu hiyo baada ya kuonekana kumuunga mkono rais aliyeondolewa mamlakani Mohammed Morsi. Klabu ya Al Ahly, imesema kuwa Ahmed Abdul Zaher , hatashiriki mchuano wa FIFA wa klabu bingwa duniani baada ya kupiga saluti ya vidole vinne mnamo siku ya Jumapili. Mchezaji huyo alikuwa anasherehekea bao lake la mchuano wa mabingwa wa Afrika ambapo Al Ahly ilishinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Orlando Pirates wa Afrika Kusini. Ishara hio imekuwa ikitumika kama ishara ya kumuunga mkono bwana Morsi.

WENGER KUFUNGA PINGU NA MERTESACKER.

Picha
KLABU ya Arsenal inajiamini beki wake tegemeo, Per Mertesacker atasaini Mkataba mpya wa muda mrefu. Klabu hiyo imeanza mazungumzo na mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ujerumani juu ya vipengele vya Mkataba na inafahamika mazungumzo yanaendelea vizuri. Mertesacker amedhihirisha yeye ni mwamba wa safu ya ulinzi ya The Gunners akitengeneza ukuta mgumu wa mabeki wanne akicheza sambamba na Laurent Koscielny. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amebakiza miezi 18 katika Mkataba wake wa sasa, ambao unamfanya alipwe mshahara wa Pauni 65,000 kwa wiki na kocha Arsene Wenger anataka mustakabali wake ukamilishwe haraka iwezekanavyo.

ABEL DHAIRA ATEMWA RASMI SIMBA.

Picha
SIMBA SC inatafuta kipa mzuri wa kumsajili katika dirisha dogo, wakati huo huo inafikiria kuachana na kipa wake, Mganda, Abbel Dhaira ikibidi mapema iwezekanavyo au mwishoni mwa msimu. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema leo kwamba, kutokana na kanuni mpya ya usajili wa wachezaji wa kigeni msimu ujao ya wachezaji watatu kutoka watano, hawatahitaji kipa mgeni. Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), amesema kwamba kwa sababu hiyo lazima waachane na Dhaira mwishoni mwa msimu, au kama atapata timu hata sasa ambayo itakuwa tayari kuilipa Simba, watamuuza. Poppe amesema kwa sasa Simba SC tayari inasaka kipa atakayekwenda kuwa pamoja na makipa wa wazawa, Abuu Hasimu na Andrew Ntalla. “Niseme wazi, tunatafuta kipa. Huu ni mchakato makini sana na hatutaki kurudia kosa. Tunatafuta kipa mzawa, kwanza awe mwaminifu na mwenye uwezo mkubwa,”alisema. Kuhusu habari kwamba, klabu hiyo inabadilisha benchi la Ufundi, Poppe amesema kwamba huo si

KASEJA ATOBOA SIRI YA KUITEMA SIMBA.

Picha
Mlinda lango nambari moja nchini Juma Kaseja ametoboa siri ya kuikacha klabu yake ya zamani Simba na kumwaga wino kwa vijana wa Jangwani maarufu Yanga kwamba amefuata maslahi mazuri ambayo ilikuwa ngumu kupata angekuwa Simba. Akizungumza na Mtandao huu, Kaseja amesema kuwa Yanga ndio timu kubwa hapa nchini na inayolipa vizuri tofauti na klabu nyingine zilizomuhitaji msimu huu, anasema katika kipindi chake alichokaa bila kuwa na timu msimu huu timu nyingi zilimfuata lakini hakuna iliyofikia dau la Yanga. Aidha kipa huyo amewaondoa hofu mashabiki wa Simba na kuwaambia mpira kazi yake na asingeweza kuikacha ofa ya Yanga, amedai yeye ni mchezaji na mpira kazi yake hivyo hawezi kukaa ofa yoyote yenye maslahi mazuri kama aliyopewa na Yanga. Cha zaidi Kaseja amewataka mashabiki wa Yanga kumpa muda ili aweze kujifua na timu hiyo kabla hajashuka dimbani kuanza kuichezea kwa mara nyingine, Kaseja aliwahi kuichezea Yanga mwaka 2009 kwa msimu mmoja kisha kurejea katika klabu yake ya zamani

YANGA KUINGIA KAMBINI KUIWINDA SIMBA

Picha
Kikosi  cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga, kitaingia kambini Novemba 25 kujiandaa kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo na mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Simba utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Desemba 14, mwaka huu. Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, Kocha wa timu yao, Mholanzi Ernie Brandts aliyeondoka nchini mara tu baada ya raundi ya kwanza ya ligi hiyo kumalizika Novemba 7, mwaka huu, atarejea nchini Jumapili Novemba 24 tayari kuanza mazoezi na wachezaji wake Jumatatu ya Novemba 25. Simba na Yanga zitamenyana katika mchezo maalum wa Ngao ya Hisani ulioandaliwa na wadhamini wa klabu hizo kongwe nchini, Kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro ambao watatoa zawadi ya Sh. milioni 100 ambazo zimekuwa zikishindaniwa na masjhabiki wa klabu hizo kwa kunywa bia na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kwa simu (SMS). Kizuguto alisema mara baada ya mchezo huo, kikosi hicho kitaendelea na maandalizi kujiandaa

AL AHLY MABINGWA AFRIKA.

Picha
Klabu ya Al Ahly ya Misri imeshinda taji la klabu bingwa Afrika ilipoicharaza Orlando Pirates ya Afrika Kusini kwa mabao 2-0 katika mkondo wa pili na wa mechi ya mwisho mjini Cairo Jumapili. Ahly, waliojinyakulia kombe hilo kwa mara ya saba walipata alama 3-1 kwa ujumla. Kulikuwa na ripoti za vurugu kuzuka kati ya mamia ya wafuasi wa Ahly na polisi nchini Misri, kabla ya mchuano kuanza. Pindi vurugu zilipositishwa , mchezaji gwiji, Mohamed Aboutrika ndiye aliyeingiza bao la kwanza katika dakika ya 54. Ahmed Abdul Zaher aliingiza bao la pili kwa Ahly katika dakika 78. Hata hivyo mabingwa wa Misri walipungua kwa mtu mmoja na kusalia 10 dakika sita baada ya difenda Sherif Abdel Fadil kuondolewa uwanjani kwa kumfanyia masihara Daine Klate.