Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2015

VIDEO MPYA YA MKALI FIZO HII HAPA>>>

Picha
Msanii huyo mbali ya kuachia video hiyo anajipanga kwa ujio wake mpya baada ya kumalizika mwezi mutukufu Ramadhani.

HAMISI KIIZA ATUA RASMI SIMBA, HANSPOPPE ASHANGAA

Picha
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Hamis Kiiza, raia wa Uganda, juzi Jumamosi alitangaza rasmi kwamba amejiunga na Simba, jambo lililoshangiliwa na baadhi ya mashabiki wake. Kiiza alitangaza hayo kwenye sherehe ya harusi ya mchezaji mwenzake, Emmanuel Okwi iliyofanyika katika Ukumbi wa Uma uliopo Lugogo nje kidogo ya Jiji la Kampala, kufuatia ndoa takatifu aliyofunga na mkewe Nakalega Florence kwenye Kanisa la Lubaga Miracle Center linaloongozwa na Mchungaji Robert Kayanja.

HARUSI YA OKWI YAFANA

Picha
Harusi ya mshambuliaji wa Simba, Mganda Emmanuel Okwi imeacha historia nchini Uganda akitumia dola 80,000 ( Sh 160,000 Mil ) kwa ajiri ya kuifanikisha iliyofanyika Jumamosi jijini Kampala. Kiasi hicho kinatosha kabisa kukamilisha usajili wa timu zisizopungua tatu za Ligi Kuu Bara, lakini yeye alitumia fedha hizo kwa ajili ya sherehe, huku Gazeti hili lilikuwa Uganda na kushuhudia kila kitu kilivyokuwa kinaendelea wakati Okwi akimuoa Florence Nakalega. Mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Hamis Kiiza na Nabisubi Julian ndiyo walikuwa wasimamizi wao wa harusi hiyo, ilifungwa katika kanisa la Miracle Centre Cathedral lililopo Lubaga, Kampala.

MAKALA: Halifa Maliyaga: Msanii anayekuja juu bongo muvi

Picha
Na Prince Hoza ONGEZEKO la vijana katika tasnia ya sanaa hasa filamu limezidi  kukua kwa kasi, hii inadhihirisha kuwa vijana wengi hawana  ajira na sasa filamu zinaweza kuwaokoa. Halifa Yuda Maliyaga ( Pichani) ndiyo jina lake halisi, naye ameamua  kujikita kwenye tasnia hiyo lakini yeye anadai sanaa hiyo ipo  ndani ya damu ya ukoo wao kwani kaka yake Hemed Halifa  Maliyaga maarufu 'Mkwere' anatesa kwenye kundi la Mizengwe. Maliyaga aliingia rasmi kwenye sanaa baada ya kumaliza shule  ya msingi mwaka 2011 katika shule ya Mdaula Chalinze Pwani,  kundi lake la kwanza kushiriki nalo linaitwa Zinduko Arts  ambapo alidumu nalo hadi mwaka 2014. Maliyaga alijiunga na kundi la Nuru njema Arts Group mwaka  2014 ambapo anatamba nalo hadi sasa.

Carlos Tevez amerejea Boca Juniors

Picha
Mshambulizi wa Argentina na washindi wapili katika kombe la mabingwa mwaka huu Juventus Carlos Tevez amerejea katika klabu yake ya zamani ya Boca Juniors. Tevez, 31, alianzia huko huko Argentina katika Boca Juniors kabla ya kuondoka mwaka wa 2004 kwa ziara iliyomweka barani ulaya kwa kipindi cha miaka 9. Tevez ambaye alitamba Uingereza katika vilabu vya Manchester United, Manchester City na West Ham kabla ya kuhamia Italia kujiunga na mabingwa msimu huu Juventus .

Blatter: Sikujiuzulu kama rais wa FIFA

Picha
Rais wa shirikisho la soka duniani Sepp Blatter amekariri kuwa hakujiuzulu kama rais wa shirikisho hilo. Kiongozi huyo mswissi mwenye mri wa miaka 79 alikuwa amedhaniwa kujiondoa madarakani juni tarehe 2 kufuatia kashfa kubwa ya ufisadi ulaji rushwa na matumizi mabaya ya madaraka iliyokumba shirikisho lake lakini sasa anaonesha dalili za kubadili mtazamo huo. Blatter ambaye ameiongoza FIFA kwa miaka 17 alikuwa ametangaza kuwa atajiondoa mbele ya kamati kuu ili kufanyike uchunguzi wa kina katika FIFA lakini sasa ameikumbusha jarida moja la uswisi BLICK kuwa yeye ndiye rais wa FIFA na kuwa aliweka hatima yake mikononi mwa kamati kuu ya shirikisho katika mkutano wa dharura.

KAMARA AIGEUKA YANGA, AHAMIA SC VILLA, KUCHEZA TAIFA LEO

Picha
Siku chache baada ya kutemwa katika usajili Yanga, Lansana Kamara jana asubuhi mapema aliibuka katika mazoezi ya SC Villa ya Uganda na leo anataichezea timu hiyo dhidi ya Yanga kwenye mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa. Juzi Jumatano Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm bila kuficha alimuambia Kamara raia wa Sierra Leone, hana nafasi ya kusajiliwa katika kikosi chake kwa kuwa ana uwezo wa kawaida. Baada ya kuelezwa hayo, Kamara akiwa na wakala wake Gibby Kalule wakatimua zao na jana asubuhi walitinga katika mazoezi ya Villa kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Ubungo Plaza.

Arsenal wamnunua chipukizi nyota wa Romania

Picha
Nahodha wa timu ya taifa ya Romania ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 16 Vlad Dragomir amekataa ofa kutoka kwa mabingwa wa ligi ya kwao nyumbani Steaua Bucharest pamoja na timu kadha za ugenini na kuamua kujiunga na Arsenal kutoka ACS Poli Timisoara. "Nina furaha na natumai sitamvunja moyo mtu yeyote,” kiungo huyo wa kati, aliyetia saini mkataba wa miaka mitatu na klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza, aliambia vyombo vya habari Romania Jumatano. “Ofa ya Arsenal ilinipendeza zaidi, nilihisi kwamba huko ndiko nafaa kwenda.” Dragomir ndiye tineja wa pili kutoka Romania kujiunga na Ligi Kuu ya Uingereza mwezi huu baada ya Cristian Manea,

NGOMA KUKINUKISHA LEO TAIFA DHIDI YA SC VILLA YA UGANDA, PINDA KUSHUHUDIA JUKWAANI

Picha
Mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Donald Ngoma leo anatarajiwa kuiongoza safu ya ushambuliaji ya Yanga kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Sports Club Villa ya Uganda. Ngoma aliyetua nchini tangu mwanzoni mwa wiki ni miongoni mwa usajili mpya uliofanywa na Yanga kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake kitakachoshiriki mashindano ya Kombe la Kagame, klabu bingwa Afrika na Ligi Kuu msimu ujao.

SIMBA YATAMBULISHA KOCHA MPYA LEO, NI YULE ALIYEWAHI KUCHEZA LIGI YA UINGEREZA

Picha
Timu ya Simba imeingia makubaliano ya mkataba wa mwaka mmoja na kocha raia wa Uingereza, Dylan Kerr ya kukinoa kikosi hicho kwenye msimu ujao wa Ligi Kuu Bara. Kocha huyo, atatua kukinoa kikosi hicho ili kurithi kibarua cha Mserbia, Goran Kopunivoc aliyemaliza mkataba wa kukinoa kikosi hicho mwishoni mwa msimu uliopita wa ligi kuu. Rais wa timu hiyo, Evans Aveva alisema kuwa kocha huyo anatarajiwa kutua nchini wiki hii tayari kwa kuanza kibarua cha kukinoa kikosi hicho. Avea alisema, kocha huyo mara ya kutua nchini atazungumza na Waandishi wa habari na Jumatatu ya wiki ijayo ataanza kibarua rasmi cha kukinoa kikosi hicho chini ya kocha msaidizi, Selemani Matola.

NYAMBUI KOCHA WA RIADHA BRUNEI

Picha
Mshindi wa zamani wa medali ya fedha ya michuano ya Olimpiki, Suleiman Nyambui amepata kazi ya kuwa kocha mkuu wa Brunei. Nyambui, aliyeshinda medali ya Olimpiki mwaka 1980 wakati wa michuano ya Olimpiki ya majira ya joto nchini Moscow,amesema kuwa amepewa mkataba wa kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo kwa miaka miwili, ila atafanya kazi kwa miezi sita kuangalia mazingira.

UKATA WAMKWAMISHA MKOLA MAN KUTENGENEZA VIDEO YA MALAVIDAVI TIME

Picha
MSANII wa muziki wa kizazi kipya Mkola Man anayewakilisha kundi la Sakainge lenye maskani yake Hale mkoani Tanga ameelezea masikitiko yake ya kushindwa kutoa video ya wimbo wake mkali wa 'Malavidavi Time'. Mkola Man amesema kuwa ukata mkubwa uliomkumba ndio chanzo cha yeye kushindwa kutengeneza video ya wimbo wake wa 'Malavidavi time' ambao amemshirikisha mkali mwenzake kutoka kundi hilo hilo la Sakainge Yusa G. Akizungumza na gazeti hili, Mkola Man amesema kwa sasa hana fedha za kuweza kutengeneza video hasa baada ya kuachishwa kazi, hivyo anawaomba wafadhili wajitokeze kumsaidia ili aweze kutengeneza video ya wimbo huo pamoja na kuandaa kazi mpya. 'Muziki ni ajira tosha, ila kwa sasa sina kitu zamani nilikuwa

Adebayor asema yuko tayari kuchezea Togo

Picha
Emmanuel Adebayor Emmanuel Adebayor amemaliza kimya chake na kudai kuwa yuko tayari kuchezea Togo mechi ya kufuzu kwa Afcon dhidi ya Liberia Jumapili. Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Togo pamoja na wenzake wawili walikuwa wamekataa kujiunga na timu ya taifa iliyoitwa na kocha mpya Tom Saintfiet kwa maandalizi ya mechi yao ya kwanza ya kufuzu kwa Kombe la Taifa Bingwa Afrika bila kutoa sababu zozote.   Na straika huyo aliyepewa likizo na klabu yake ya Uingereza Tottenham ili akatatue matatizo ya kifamilia na kiakili kabla ya msimu kumalizika, amedokeza kuwa bado anajiandaa baada ya kutazama mechi ya kirafiki ambayo Togo walilazwa 0-1 na Ghana uwanja wa Accra Sports Stadium Jumatatu. “Bila shaka nimekuwa nikijiandaa kuwa sawa kucheza soka tena kwa sababu umekuwa muda mrefu sana tangu nicheze dakika 90 za soka,” fowadi huyo lalisema alipoulizwa ni kwa nini hakuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa uwanjani

AZAM FC WAENDELEA KUSISITIZA MESSI WATAMCHUKUA.

Picha
Makamu mwenyekiti wa klabu ya Azam FC Idrisa Nassor ameendelea kusisitiza kuwa watamchukua kiungo mshambuliaji wa Simba Ramadhan Singano 'Messi' aliye katika matatizo ya kimkataba. Juzi klabu ya Simba ilifanya kikao chake na kuamua kukaidi agizo la TFF na kuendelea kuutambua mkataba wao na Messi unaokwisha julai 16 2016, lakini Azam inaamini itafanikiwa kumnasa Messi ambae kwa sasa yuko huru kufuatia mkataba wake na Simba kufutwa na TFF. Akizungumza jana, Nassor amesema klabu yake inatamani kuwa na mchezaji Ramadhan Singano kwani ni mmoja kati ya viungo wa pembeni wanaofanya vizuri kwa sasa.

STARS YAIFUATA MISRI, TAYARI KWA MCHEZO WA AFCON

Picha
Baada ya mazoezi ya wiki moja nchini Ethiopia, timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Ijumaa jioni mjini Addis Ababa kuelekea nchini Misri tayari kwa mchezo wa kwanza wa kugombea kucheza fainali za AFCON za mwaka 2017 utakaochezwa siku ya jumapili. Mechi ya marudiano itachezwa Dar es Salaam, Tanzania baada ya wiki mbili.

KAMARA AFELI MAJARIBIO YANGA

Picha
Kiungo mpya wa Yanga, Msierra Leone Lansana Kamara amepewa mtihani mwingine na kocha Hans Pluijm akitakiwa kuhakikisha anajua kupiga mashuti ili kusajiliwa. Udhaifu wa kiungo huyo ulionekana pale kocha Hans Pluijm alipowapa zoezi maalumu kupima ufanisi wao kwenye upigaji mashuti, ambalo kiungo huyo mkabaji hakulimudu ipasavyo. Katika zoezi hilo, Pluijm alimtaka kila mchezaji kupiga mashuti 12 kuelekea kwenye lango ambalo lilikuwa na kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ aliyekuwa amesimama.

Recho atikisa 'Yuleyule ya PNC

Picha
Na Fikiri Salum WIMBO mpya wa mwanamuziki wa kizazi kipya nchini Panclas Ndaki Charles maarufu PNC uitwao 'Yuleyule' ambao tayari umeanza kukubalika kupitia vituo mbalimbali vya redio na runinga umeweza kumuibua video Queen mpya Rachel Njingo 'Recho', Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni PNC amesema video ya wimbo wake huo umeweza kumrudisha tena kwenye chati yake, PNC amesisitiza kuwa Recho ni bonge la video Queen na ameutendea haki wimbo huo. 'Sikutegemea kama wimbo wangu ungeweza kukubalika kiasi hicho lakini kila anayeutazama kupitia televisheni au mitandao ya kijamii hakusita kunipongeza', alisema PNC ambaye aliibukia mkoani Mwanza kabla hajajiunga na kundi la Tip top Connection lenye maskani yake Manzese Dar es Salaam. Aidha msanii huyo amedai anatarajia kuanza ziara za mikoani kwa lengo la kuutambulisha wimbo wake huo lakini pia atapeleka zawadi kwa mashabiki wake ambao walimmiss