Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUWAAGA BOCCO, MKUDE NI DHIHAKA AU MAPENZI

Na Prince Hoza Matua 

SEPTEMBA 10 klabu ya Simba SC inaadhimisha tamasha lake ya Simba Day katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, katika siku hiyo Wekundu wa Msimbazi watacheza mechi ya kirafiki na timu ya Police FC ya Kenya.

Police FC ni mabingwa wa nchi hiyo na watawakilisha taifa hilo katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika kama ilivyo kwa Simba SC ambao wamemaliza nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu bara msimu uliopita.

Katika tamasha hilo Simba SC watatumia nafasi hiyo ya kutambulisha jezi mpya, wachezaji wa kikosi chake cha msimu ujao na pia safi yake yote ikiwemo makocha.

Simba SC pia watatambulisha vikosi vyake vya timu za vijana kwa maana under-17 na under-20 pia timu ya wanawake, Simba Queens ambayo nayo imefanya usajili mkubwa kama ilivyo timu ya wanaume.

Kitu ambacho kinanifanya niandike makala hii ni kitendo cha klabu hiyo kuwaaga wachezaji wake wawili wa zamani wote wakiwa manahodha, John Raphael Bocco na Jonas Gelard Mkude.

Wachezaji hao waliichezea Simba kwa mafanikio makubwa lakini baadaye wakaachana na klabu hiyo na kutimkia vilabu vingine, Mkude yeye alidumu Simba misimu 13 na alijiunga Yanga SC ambao ni mahasimu wakuu wa Simba.

Na Bocco naye alidumu Simba misimu 8 na alitimkia JKT Tanzania, lakini uongozi wa Simba uliona umuhimu wa kuwapa heshima wachezaji hao na katika tamasha la Simba Day la mwaka huu wanawaaga rasmi.

Meneja wa Habari na mawasiliano Wa Klabu ya Simba SC Ahmed Ally amefunguka na kuthibitisha kuwa kwenye tamasha la Simba Day la mwaka huu itakuwa ni siku pia ya kuwaaga nyota wao wawili wa zamani wa kikosi hicho ambao ni Jonas Mkude na John Bocco.

Kwa ajili ya kutambua mchango wao ndani ya klabu hiyo ,huku pia akieleza kuwa mchezaji mwingine ambaye mashabiki wanamsubiri ataaagwa akimaliza pensheni yake japo hajataka kutaja jina lake.

"Tumeandaa utaratibu maalum wa kuwaaga wachezaji wetu vipenzi ambao waliitumikia Simba kwa muda mrefu lakini hatukupata bahati ya kuwaaga lakini niwaambie tumeshaongea nao na wamethibitisha watakuwepo Simba Day hii"
.
"Hapa namzungumzia John Bocco na Jonas Mkude  ambao walikaa Simba kwa muda mrefu lakini wakaondoka bila Kuagwa,  nitumie fursa hii kuwaambia kuwa Simba Day hii  itakuwa ni siku maalum ya kuwaaga wachezaji hawa", alisema Ahmed Ally.

Bila shaka tamasha la Simba Day lakuvutia sana kutokana na utofauti wake lakini mimi binafsi nashindwa kuwaelewa Simba SC kama wameamua kufanya tamasha hili na kuwaaga wachezaji hao Bocco na Mkude kwa mapenzi mema kwa wachezaji hao au wanawadhihaki.

Mapenzi mema kwao ni kwa sababu wameona umuhimu wao na ndio maana wamewaita na kuwaaga mbele ya halaiki ya wapenzi na mashabiki wa Simba ulimwenguni kote, najua Mkude aliipigania Simba tangu akicheza Simba B na baadaye timu ya wakubwa.

Lakini Bocco naye alicheza kwa mafanikio na ndio maana wakampa kitambaa cha unahodha, dhihaka inakuja kwa uongozi wa Simba kuwaaga sasa na si huko nyuma, Mkude aliachana na Simba msimu juzi, na Simba wamefanya matamasha mawili mpaka sasa.

Na Bocco aliachana na Simba msimu jana, na Simba wamefanya tamasha moja bila Bocco, Simba walipaswa kuwaaga wachezaji hao kwa wakati wao na si sasa, kuwaaga wachezaji hao ni dhihaka za waziwazj na si kuonesha mapenzi kama wenyewe wanavyodhani.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...