Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Morocco mabingwa CHAN

TIMU ya taifa Morocco imefanikitwa kutwaa Kombe la Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Madagascar usiku huu Uwanja wa Moi International Sports Centre, Kasarani, Nairobi nchini Kenya.
Ilikuwa mechi ya funga nikufunge, kabla ya mshambuliaji wa mabingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika, RS Berkane – Oussama Lamlioui kufunga bao la ushindi dakika ya 82.

Hilo lilikuwa bao lake la pili kwa Lamlioui kwenye mchezo huo kufuatia kufunga lingine dakika ya 44 ambalo lilielekea kuwa la ushindi – kabla ya winga wa COSFAP Antananarivo, Toky Niaina Rakotondraibe kuisawazishia Madagascar dakika ya 68.

Madagascar ndio waliouanza vizuri mchezo huo na kupata bao la kuongoza kupita kwa mshambuliaji wa Fosa Juniors FC, Felicite Manohantsoa dakika ya tisa, kabla ya winga wa Renaissance de Berkane, Youssef Mehri kuisawazishia Morocco dakika ya 27.

Hilo linakuwa taji la tatu la CHAN kwa Morocco baada ya awali kulibeba katika mwaka 2018 na 2020, hivyo kuweka rekodi ya kuwa timu iliyotwaa mara nyingi Zaidi ubingwa wa michuano hiyo, ikifuatiwa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) waliobeba mara mbili, 2009 na 2016, wakati timu nyingine zilizowahi kutwaa taji la michuano hyo lililoanzishwa mwaka 2009 ni Tunisia mwaka 2011, Libya mwaka 2014 na Senegal mwaka 2022.

Aidha, Oussama Lamlioui ameibuka mfungaji wa michuano hiyo kwa mabao yake sita, huku nyota mwingine wa Morocco, kiungo wa ulinzi wa AS FAR Rabat, Mohamed Rabie Hrimat akibeba Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashindano na Kipa wa Teungueth FC, Marc Diouf akishinda Tuzo ya Kipa Bora na timu yake ya taifa, Senegal ikishinda Tuzo ya Mchezo wa Kiungwana.

Kwa ubingwa huo, Morocco wamezawadiwa fedha, Dola za Kimarekani Milioni 3.5 huku Madagascar wakiondoka na Dola Milioni 1.2 kwa kumaliza nafasi ya Pili.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...