Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga haitanii, yaichapa Tabora United 4-0 kirafiki

TIMU ya Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa kirafiki leo Uwanja wa Gymkhana Jijini Dar es Salaam.

Mabao ya Yanga leo yamefungwa na kiungo Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua na washambuliaji Mzimbabwe Prince Dube Mpumelelo na Ange Celestin Ecua aliyesajiliwa dirisha hili kutoka Zoman FC ya kwao, Ivory Coast.

Huo unakuwa mchezo wa nne wa kujipima nguvu kwa Yanga katika maandalizi ya msimu mpya na kuendeleza rekodi ya ushindi.

Mechi tatu za awali ilishinda 3-1 dhidi ya Rayon Sports Jijini Kigali nchini Rwanda, 2-1 dhidi ya Fountain Gate na 4-0 dhidi ya wadogo zao, U20 zote Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.

Msimu Yanga ipo chini ya Benchi jipya kabisa la Ufundi Yanga chini ya Kocha Mkuu, Mfaransa Romain Folz na Msaidizi wake, Mspaniola Alejandro Manu Rodríguez Lázaro na Kocha wa Makipa, Majdi Mnasria.

Wengine ni Mtaalamu wa Viungo (Physiotherapist), Youssef Ammar wote kutoka Tunisia, Kocha wa Physic, Tshephang ‘Chyna’ Mokaila kutoka Botswana, Mchambuzi wa Video, Thula Bantu na Mkurugenzi wa Ufundi, Paul Matthews wote raia wa Afrika Kusini.

Yanga SC inatarajiwa kuuanza msimu kwa mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu, Simba SC Septemba 16 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam – baada ya tamasha lake la kutambulisha kikosi cha msimu mpya, Kilele cha Wiki ya Mwananchi Septemba 12.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...