Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2025

Dodoma Jiji yapigwa faini kisa kocha kihiyo

Klabu ya Dodoma Jiji imepigwa faini ya jumla ya TZS milioni 15 baada ya kucheza michezo ya Ligi Kuu bila kuwa na kocha mwenye sifa na ujuzi unaotakiwa. Adhabu hiyo imetokana na klabu hiyo kushiriki michezo mitatu tofauti, dhidi ya KMC, TRA United, na Coastal Union, ambapo kwa kila mchezo imepigwa faini ya TZS milioni tano.

Hatimaye mvaa hereni atambulishwa Simba

Klqbu ya Simba SC, imetambulisha Dimitar Pentev kuwa meneja mkuu akifanya kazi kama kocha mkuu lakini atasimama kama msaidizi kwakuwa hana vigezo. Inasemekana Pantey ana UEFA A ambayo haimfanyi kusimama benchi kama kocha mkuu ila ataelekeza timu kwenye mazoezi na wakati wa mechi Seleman Matola atasimama kama kocha mkuu.

Bacca afungiwa mechi tatu

Nyota wa klabu ya Yanga Ibrahim Bacca amefungiwa baada ya kuonesha mchezo usio wa kiungwana kwenye mechi ya Mbeya City dhidi ya Yanga SC. Katika hatua nyingine Waamuzi waliochezesha mchezo wa JKT Tanzania dhidi ya Azam FC na waamuzi wa mechi ya Mbeya City dhidi ya Yanga SC wamefungiwa zaidi ya michezo (3). Adhabu hizo zimetolewa baada ya Kikao cha kamati ya saa (72) kuketi hapo jana na kufanya Maamuzi hayo.

Muya kocha mpya Coastal Union

Kocha wa zamani wa Fountain Gate, Mohamed Muya,amejiunga rasmi na Coastal Union kama kocha mkuu akichukua nafasi ya Ally Mohamed Ameir aliyefutwa kazi. Coastal Union imeanza vibaya Ligi Kuu bara ikiwa imepoteza mechi mbili mfululizo na kushinda moja.

Yanga wamvuta Nabi mezani

Kocha wa zamani wa Yanga, Nassredine Nabi akiwa Jijini Dar Es Salaam hii leo amekutana na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Klabu ya Yanga,  Antony Mavunde na kufanya kikao cha masaa kadhaa na Kocha huyo. . Nabi kwa sasa hana timu baada ya kujiuzulu kufundisha Kaizer Chiefs.

Azam FC yaililia Bodi ya Ligi kwa JKT Tanzania

Uongozi wa Klabu ya Azam FC ya Dar es salaam umeiandikia barua bodi ya ligi ukilalamikia uamuzi mbovu kwenye mchezo wao dhidi ya JKT Tanzania uliopigwa jana Octoba 1,2025. Katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa sare ya kufungana bao moja kwa moja Azam FC imeyalalamikia matukio kadhaa ambayo hayakuamuliwa kwa usahihi. Barua hiyo imewasilishwa kwa mtendaji mkuu wa bodi ya ligi leo asubuhi.

Nabi azikacha Simba na Yanga

BAADA ya Kocha Nasreddine Nabi kuonekana nchini Tanzania kwa siku za hivi karibuni akihusishwa na klabu baadhi; hatimaye kocha mwenyewe amefafanua zaidi kuwa yupo nchini kwa masuala yake binafsi. “Nimeona watu wanasema nimekuja hapa kwa ajili ya Simba, wengine wanasema Yanga, hapana! Nipo hapa kwa safari yangu binafsi, nadhani hii ni mara ya tatu nakuja hapa," alisema Nabi Akaongeza; “Tanzania ni kama nyumbani ndio maana napenda sana kuja hapa, tangu nimefika sijakutana na kiongozi yeyote wa Simba wala Yanga, nikimaliza mambo yangu nitaondoka.”

Rasmi, Simba yamalizana na bishoo wa Gaborone, aaga

Kocha wa Gaborone Utd,raia wa Bulgaria Dimitar Pantev (49) ameaga rasmi ndani ya klabu hiyo. Simba wamekubali kumpa kila hitaji lake hivyo muda wowote kuanzia sasa atatua Dar es salaam ili kukamilisha dili lake.

WANAYANGA WANATAKA GUSA ACHIA TWENDE KWAO, FOLZ BADILIKA

Na Prince Hoza Matua WANAYANGA wanataka timu yao icheze mpira wa kupigiana pasi fupi fupi kwa staili ya kwenda mbele, hawataki mpira wa taratibu na kupigiana pasi za kurudi nyuma, wameshazoeshwa na makocha wao waliopita. Tunajua kabisa kwamba Wanayanga kupata ushindi kwao sio habari ngeni, wamezoeshwa na makocha waliopita, Yanga kushinda makombe ni jadi yao wala sio kitu kigeni, vitu ambavyo kwao ni vigeni ni pale timu yao inafungwa au kutoka sare. Kwa kifupi mashabiki wa Yanga sio watu wa mpira, hawajui kanuni za mpira, kwamba kuna matokeo aina tatu tu, kufungwa, kushinda na kutoka sare, lakini mashabiki wa Yanga wanajua tokeo moja tu la kushinda. Ikitokea timu yao imetoka sare, kocha ananyooshewa kidole, kama sare ya kwanza wanamvumilia kama ya pili wanampa kalipio kali na kama ya tatu wanamfungashia virago, kwa kifupi hawataki matokeo ya aina mbili yatokee. Lakini kwa sasa mashabiki wa Yanga wamebadilika kidogo, kushinda wamegeuza kama asilia yao, ila wanataka timu yao icheze kwa ku...

Roman Folz apewa mechi 3 Yanga

Uongozi wa klabu ya Yanga umeampa mechi tatu kocha mkuu wa klabu hiyo Romain Folz ili kubadilisha mwenendo wa klabu hiyo na kama si hivyo watamfuta kazi mara moja. Hata hivo kocha Folz hajaridhishwa na kitendo hiko kwani wameonekana hawana Imani naye hivo anaweza akaamua kuondoka zake ndani ya Jangwani.  Kama Romain Folz ataendelea kusalia Jangwani anatakiwa kufanya kazi ya zaida kukiandaa kikosi hiko kabla ya kurejea kwa Ligi baada ya mapumziko ya kimataifa.  Inakumbukwa kuwa hii imekuja kutokana na matokeo ya sare tasa ya 0-0 katika mchezo wao wa Ligi jioni ya Jana uliopigwa katika uwanja wa CCM Sokoine jijini Mbeya dhidi ya wenyeji wao Mbeya City kutoka huko huko jijini Mbeya.

Simba yailalua Namungo 3-0

Wekundu wa Msimbazi, Simba SC usiku huu imeilalua timu ya Namungo FC mabao 3-0 mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam. Ikiwa chini ya kocha msaidizi Seleman Matola, Simba ilitangulia kwa bao la Chamou Karaboue dakika ya 44 kabla ya Rushine De Reuck dakika ya 61 kufunga la pili wakiwa wote ni mabeki wa kati. Lakini mshambuliaji wa Wydad Casablanca, Seleman Mwalimu Gomez aliyepo Simba kwa mkopo, aliiandikia bao la tatu dakika ya 85, kwa matokeo hayo Simba inakaa kileleni ikiwa na pointi 6 na mechi mbili

Azam FC yashindwa kung' ang' ania bomba kwa JKT Tanzania

Timu ya Azam FC usiku huu imeshindwa kuutumia vema uwanja wa Meja Jenerali Isamuyo Mbweni  jijini Dar es Salaam baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 mchezo wa Ligi Kuu bara. Bao la Feisal Salum Abdallah maarufu Feitoto dakika ya 43 liliitanguliza kileleni lakini walishindwa kung' ang' ania bomba baada ya dakika ya 90 kijana wake wa zamani Paul Peter Kasunda kuisawazishia JKT Tanzania na kulazimisha sare na kuduwaa.

Mayele aendelea kutetema Pyramids

Mshambuliaji Fiston Mayele kaweka kamba mbili na kuisaidia Pyramids FC kuondoka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Wenyeji APR FC Katika mchezo wa CAFCL Pale Jukwaani Kulikuwa na mshikaji wake Jesus Moloko waliye cheza pamoja wakiwa Young Africans, Moloko alienda kumshuhudia PREDATOR FISTON MAYELE Akiifanya kazi yake naye akaifanya vyema pale Katika Dimba la Stade Régional Nyamirambo Baada ya Mchezo kumalizika FISTON MAYELE Alitambua uwepo wa Jesus Moloko na akaenda kumpatia jezi yake.  Jesus Moloko hivi sasa anaichezea AS Kigali ya Rwanda.

Pacome aitwa Ivory Coast, Ahoua atoswa

Kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ivory Coast "Elephant" wakati kiungo wa Simba SC, Jean Charles Ahoua ametoswa kwenye timu hiyo.

Nasreddine Nabi amekuja kutalii

Imefahamika kwamba kocha wa zamani wa Yanga SC, Nasreddine Nabi amekuja nchini kutalii tu na wala Hana mpango wa kujiunga na klabu ya Simba au Yanga. Taarifa za Nabi kuhitajika na Simba zilienea jana pale tu alipoonekana jijini Dar es Salaam, lakini mtu wa karibu na kocha huyo ambaye pia ameinoa Kaizer Chief ya Afrika Kusini amedai kwamba amekuja kupumzika na wala SI kujiunga na Simba.

Kapombe, Tshabalala nje Taifa Stars

KOCHA Hemed Suleiman 'Morocco' hajawamjumuisha mabeki wakongwe wa pembeni, Shomari Kapombe na Mohamed Hussein 'Tshabalala' kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kitakachoingia kambini Jumamosi, Oktoba 4, 2025 kujiandaa na mchezo wa Kufuzu Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Zambia.

Chama arudishwa Chipolopolo, kuivaa Stars kwa Mkapa

Kiungo mshambuliaji wa Singida Black Stars, Clatous Chama (34) ameitwa kwenye kikosi cha Zambia (Chipolopolo) kwaajili ya mechi mbili za kufuzu World Cup Vs Tanzania & Niger. Oktoba 8, Chama ataumana na Tanzania pale kwa Mkapa. Vilevile, Kennedy Musonda ameitwa kwenye kikosi hicho..

Simba yachenji gia angani, sasa yamtaka kocha wa Gaborone United

Simba SC wako kwenye mazungumzo na kocha wa Gaborone Utd, raia wa Bulgaria  Dimitar Pantev (49). Simba ni kama wamebadili gia angani, kwani wameachana na mpango wa kumchukua kocha wa zamani wa Al Ahly ya Misri na Orlando Pirates Jose Ribeiro na sasa wanamtaka kocha wa Gaborone United.

Gamondi kuiponza Singida Black Stars, kukatwa pointi

Inasemekana kwamba kocha Miguel Gamondi wa Singida Black Stars anaweza kuigharimu timu hiyo na kukatwa pointi sita ilizonazo kwakuwa ana adhabu ya kufungiwa na Bodi ya Ligi wakati anainoa Yanga SC. Mara ya mwisho,Miguel Gamondi anaondoka Tanzania alifungiwa mechi 3 na adhabu ya Tsh milioni 2,000,000. Kwa mujibu wa CEO wa Bodi ya Ligi,adhabu ya hela walikatwa Yanga,Lakini vipi kuhusu adhabu ya Gamondi? Amerudi na tumeona tayari mechi 2 za Ligi amekaa kama kocha mkuu wa Singida Black Stars,vipi BODI YA LIGI imesahau? Kanuni iko kimya? Nini kimefanya Gamondi kukaa benchi mechi 2 za Ligi Kuu Tanzania Bara huku akiwa na adhabu? Wapinzani waliofungwa na Singida Black Stars wakisimama na kuleta hili hoja,watapewa haki yao kikanuni? Tunatamani Bodi ya Ligi  itupe majibu sahihi kwenye Hili la Gamondi ili tusirudi tulipotoka.