Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2025

Singida Black Stars nao wahamia Zanzibar

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza kuchagua kuutumia uwanja wa New Amaan-Zanzibar kwenye mechi zao za nyumbani kwenye mechi za hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika 2025/26. Singida Black Stars imefuzu hatua ya Makundi ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza, na sasa inasubiri droo ya kupanga makundi itakayofanyika Johannesburg, South Africa Jumatatu ijayo Novemba 03,2025

Ndayiragije avunja mkataba Police FC

Kocha raia wa Burundi Étienne Ndayiragije amekatisha Mkataba Wake na Police FC ya Nchini Kenya Baada ya kuifundisha klabu hiyo kwa Miezi 11. Étienne Ndayiragije alijiunga na Klabu hiyo Mwishoni Mwa Mwezi Novemba ambapo aliikuta ikiwa nafasi ya mwisho katika michezo nane iliyokuwa imecheza kwenye Ligi Kuu ya Kenya. Kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo ilishinda Kombe la Ligi Kuu Kenya na kuiwakilisha nchi katika Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika. Katika Michuano ya klabu Bingwa Afrika, walitolewa na Al Hilal SC ya Sudan katika raundi ya pili. Inaelezwa kuwa Étienne Ndayiragije kuna timu ambayo iko inawinda saini yake ili aweze kuwa Kocha Mkuu ingawa bado haijawekwa wazi ni Klabu ipi. Etienne Ndayiragije

Makocha wa Simba na Yanga matawi ya juu Algeria

Klabu 4 za Algeria zimefanikiwa kuingia hatua ya Makundi ya mashindano ya CAF CAF Champions League zilizoingi ni MC Alger inayonolewa na Rulani Mokwena, JS Kabylie inayonolewa na Josef Zinnbauer. CAF Confederation Cup zilizofuzu ni CR Belouizdad inayonolewa na Sead Ramović aliyewahi kuinoa Yanga na timu ya USM Alger inayonolewa na Abdelhak Benchikha ambaye aliwahi kuinoa Simba SC.

Yanga yailaza Mtibwa Sugar

MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Pongezi kwa wafungaji wa mabao ya leo – wachezaji wapya, beki Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ aliyesajiliwa kjutoka kwa watani, Simba SC dakika ya 38 na kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Chad, Célestin Ecua aliyesajiliwa kutoka Zoman FC ya Ivory Coast dakika ya 83. Baada ya mchezo huo, Tshabalala ambaye anafahamika pia kwa jina lingine la utani, Zimbwe Junior alikabidhiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi kwa kiwango kizuri alichokionyesha leo. Kwa ushindi wa leo, Yanga inafikisha pointi saba katika mchezo wa tatu baada ya kuichapa Pamba Jiji mabao 3-0 kwenye mchezo wa kwanza na sare ya bila mabao na Mbeya City kwenye mchezo uliofuata Jijini Mbeya. Kwa upande wao Mtibwa Sugar waliorejea Ligi Kuu msimu huu baada ya msimu mmoja wa kucheza Championship wanabaki na pointi zao tano za mechi tano ...

Azam FC yahamia New Amaan Zanzibar

KLABU ya Azam FC imeamua kuutumia Uwanja wa New Amaan Complex kwa ajili ya mechi zake za hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika baada ya Uwanja wao wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. “Mashabiki wetu na wakazi wa Zanzibar kwa ujumla tunawaletea burudani ya mechi zetu za Kombe la Shirikisho Afrika zilizobakia kwa msimu huu 2025/26, baada ya kuuchagua Uwanja wa New Amaan Complex kama uwanja wetu wa nyumbani,” imesema taarifa ya Azam FC leo na kuongeza; “Zanzibar tunakuja kuanzia hatua ya makundi, kaeni tayari kutupokea! Hii ni zamu ya Azam.

Twiga Stars yafuzu fainali za kombe la mataifa Afrika Morocco 2026

TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars leo imefanikiwa kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa Afrika Wanawake 2026 nchini Morocco baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji, Ethiopia jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Dire Dawa mjini Dire Dawa katika mchezo wa marudiano wa Raundi ya Pili na ya mwisho ya mchujo. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo mshambuliaji wa Trabzonspor ya Uturuki, Diana Lucas Msewa na kwa matokeo hayo Tanzania inafuzu WAFCON ya mwakani kwa ushindi wa jumla wa 3-0 kufuatia ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam – mabao ya washambuliaji Aisha Juma Mnunka wa Simba Queens dakika ya 23 na Jamila Rajab Mnunduka wa JKT Queens dakika ya 56. Inakuwa mara ya tatu kwa Twiga Stars kufuzu Fainali za WAFCON baada ya mwaka 2010 nchini Afrika Kusini na 2024 nchini Morocco na mara zote walitolewa katika hatua ya makundi.

Pamba Jiji yapewa ushindi wa mezani Ligi Kuu bara

Klabu ya Pamba Jiji imepewa alama tatu na magoli matatu baada ya mchezo wao dhidi ya Dodoma Jiji kushindwa kuendelea ukichezwa dakika 6 tu. Mchezo huo ulindwa kuendelea kutokana na umeme kukatika dakika ya 6, hivyo kamati ya uendeshaji na usimamizi wa ligi ya bodi ya ligi kuu (TPLB) imewapata Pamba alama tatu na magoli matatu kwa kosa la wenyeji (Dodoma Jiji) kushindwa kuuandaa mchezo vyema.

Shujaa wa Eloi Lupopo dhidi ya Orlando Pirates

Ushujaa wa Simon Omossola ulivyoipeleka Saint Eloi Lupopo katika hatua ya Makundi ya ligi ya mabingwa ya CAF. Kipa huyo wa Cameroon aliye imara katika goli, aliokoa penalti mbili baada ya sare ya 3-3 na Orlando Pirates mwishoni mwa mchezo wa kawaida. Timu ya DR Congo ilishinda 5-4...

Niffer akamatwa kwa kuhamasisha maandamano ya Oktoba 29

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema kwamba Leo, Tarehe 27,10,2025 majira ya saa 9 mchana eneo la Sinza Kumekucha limemkamata na linamuhoji Mwanamitandao na Mjasiriamali maarufu Jenifer Bilikwiza Jovin (Niffer) mwenye umri wa miaka 26 mkazi Masaki Peninsula Kinondoni kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu na kuharibu miundombinu katika maeneo mbalimbali jijini hasa siku za kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025. Pia taarifa ya Jeshi imesema kwamba hatua zaidi za kisheria zinaendelea kuzingatiwa dhidi ya mtuhumiwa.

Raja Casablanca kumng' oa Maema Msimbazi

Kocha mkuu wa klabu ya Raja CA, ambaye amewahi kuinoa Simba SC ya Tanzania , Fadlu Davids anaripotiwa kuihitaji saini ya kiungo wa klabu yake hiyo ya zamani Neo Maema. Ikumbukwe Fadlu ndiye aliyependekeza usajili wa mchezaji huyo ndani ya Simba SC.

Kocha mpya Yanga aanza kazi

Kocha mpya wa mabingwa wa soka Tanzania bara Mreno Pedro Goncalves ameanza kazi yake ya kuwanoa mastaa wa timu hiyo inayojiandaa na mchezo wake wa Ligi Kuu bara dhidi ya Mtibwa Sugar. Pedro Goncalves amechukua mikoba ya Ramon Folz aliyefulushwa hivi karibuni wakati timu ikishiriki Ligi ya mabingwa Afrika raundi ya kwanza ambapo katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Silver Strickers ilifungwa bao 1-0 mjini Lilongwe.

JKT Queens na TP Mazembe zapangwa kundi moja Ligi ya mabingwa

TIMU ya JKT Queens ya Tanzania imepangwa Kundi B pamoja na mabingwa watetezi, TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Gaborone United ya Eswatini katika Ligi ya Mabingwa Wanawake Afrika 2025. Katika droo iliyopangwa leo makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Jijini Cairo nchini Misri – mabingwa mara nyingi wa michuano hiyo, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini wenye mataji mawili wamepangwa Kundi A pamoja na wenyeji, FC Masar, AS FAR Rabat ya Morocco, Primiero de Agosto ya Angola na US FAS Bamako ya Mali. Michuano hiyo ya tano ya Ligi ya Mabingwa ya Wanawake Afrika inatarajiwa kufanyika nchini Misri kuanzia Novemba 8 hadi 21 mwaka huu ikishirikisha timu hizo nane zilizogawanywa katika makundi mawili.

Police FC ya Kenya yakata rufaa CAF na wapewe ushindi licha ya kufungwa

Timu ya Ettiene Ndayiragije ya Polisi FC ya nchini Kenya imefungua malalamiko kwenye Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) wakidai kuwa Al Hilal kwenye mchezo wa pili uliochezwa Benghazi nchini Libya na kupasuka mabao matatu kwa moja walichezesha wachezaji watatu ambao hawakusajiliwa na Shirikisho la Soka nchini Sudan (SFA) Polisi Kenya walitolewa kwa jumla ya mabao manne kwa moja baada ya kufungwa bao moja wakiwa nyumbani kabla ya kuchakazwa chuma tatu kule nchini Libya.

Timu ya Mtanzania Arzebaijan yalazimishwa sare 0-0 Ligi Kuu

Nyota wa Tanzania Alphonce Mabula na timu yake ya Samaxi FC wamepata sare ya 0-0 dhidi ya Qarabag katika mchezo wa Ligi Kuu ya Azerbaijan 

Simba yashikwa, lakini yatinga makundi Ligi ya mabingwa

TIMU ya Simba SC imefanikiwa kuingia Hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika licha ya sare ya 0-0 na Nsingizini Hotspur ya Eswatini katika mchezo wa marudiano Raundi ya Pili Ligi ya Mabingwa Afrika jioni ya leo Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Simba inanufaika na ushindi wa 3-0 dhidi ya Nsingizini Hotspur kwenye mchezo wa kwanza mabao ya beki mpya, Wilson Edwin Nangu dakika ya 45’+1 na kiungo mshambuliaji, Kibu Dennis Prosper mawili dakika ya 82 na 90’+1 Oktoba 19 Uwanja wa Taifa wa Somhlolo nchini Eswatini. Simba SC inaungana na watani wao wa jadi, Yanga SC kutinga hatua hiyo ya makundi inayoshirikisha timu 16 – wakati katika Kombe la Shirikisho pia timu zote mbili za Tanzania zimeingia hatua ya makundi pia, Azam FC na Singida Black Stars. Droo ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kwa pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika itapangwa Jumatatu ya Novemba 3 katika studio za SuperSport Jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambao ni washirika wa Matangazo wa Shirikisho l...

Naina D anamtaka mpenzi aliye- serious

Na Mwandishi Wetu MSANII wa kike wa muziki wa kizaxi kipya anayejulikana kwa jina la Naina D, ambaye pia anatamba na wimbo wake uitwao "Nipe tamu", ametambulisha wimbo wake mpya uitwao Serious. Akizungumza na Mambo Uwanjani Blog, Naina D amedai kwamba wimbo wake mpya aliourekodi kwa njia ya audio, unaelimisha jamii na kuburudisha. "Wimbo ni wa mapenzi na unalenga kumpata mtu aliye- serious na si wa kupotezeana muda", alisema na kuongeza. Wimbo huo ameutambulisha kwenye mitandao ya kijamii, ikiwemo youtube, facebook, TikTok, pia atautambulisha kwenye stesheni za redio. Naina D

Bondia mrembo kupanda ulingoni Desemba mwaka huu

Bondia mrembo Debora Mwenda  amepata nafasi nyingine ya kupigana Disemba kwa promoter Seleman Semunyu wa kampuni ya Peak Time Media. Akizungumza na mtandao huu, bondia mrembo amesema, "Nimepata nafasi  ya kuwaonesha kua niliamua kuufanya mchezo wa ngumi kwa sababu nina imani ninao uwezo wa kuufanya vizuri mchezo huo, ukiachilia mitazamo mbalimbali ya watu. Tarajieni mazuri kutoka kwangu. Leo nitawambia maana ya bondia mrembo,  urembo  unapimwa kwa ujasiri, nidhamu na nguvu ninazo ziweka kila ninapo panda ulingoni na kila ninavyoishi ishi maisha yangu ya kila siku,maandalizi nk. Urembo wangu ni katika  moyo wa kupambana na kutokata tamaa. Kila jasho ni hatua moja karibu na ndoto yangu. Nafanya boxing kwa moyo. Dunia itanikumbuka kama bondia bora wa kike, aliyeinua mchezo kwa nidhamu na mapenzi.

Masikini Clement Mzize, aumia tena

Hii inaweza kuwa taarifa mbaya kwa mashabiki wa Yanga, baada ya mshambuliaji wa kikosi hicho, Clement Mzize, juzi kujitonesha jeraha la goti. . Taarifa kutoka kwa Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema Mzize amewatia hofu tena kwani juzi jioni katika mazoezi ya mwisho kuelekea kuikabili Silver Strikers, alijitonesha jeraha lake la goti ambalo awali ilielezwa amepona . Kamwe amesema kwa Sasa kilichosalia ni Mzize kufanyiwa Vipimo Kisha kujua ukubwa wa Majeraha yake.

Rasmi Yanga yamtambulisha kocha mpya, ni Mreno Pedro Goncalves

Klabu ya Yanga Sc imetangaza kumteua aliyekuwa kocha wa Timu ya Taifa ya Angola, Pedro Gonçalves kuwa kocha mkuu mpya klabuni hapo akichukua mikoba ya Roman Folz aliyetupiwa virago. Gonçalves (49) raia wa Ureno amewahi pia kufanya kazi kama kocha wa kikosi cha vijana wa klabu ya Sporting Lisbon ya Ureno.

Singida Black Stars haoo makundi kombe la Shirikisho Afrika

Timu ya Singida Black Stars ya Tanzania bara imefanikiwa kutinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho Afrika baada ya kuiondosha Flambeau du Centre Bujumbura ya Burundi kwa mabao 3-1. Mchezo huo uliofanyika uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam, wageni Flambeau walitangulia kupata bao kupitia kwa David Irishura dakika ya 26 kabla ya Muaku kuisawazishia Singida Black Stars dakika ya 55 na baadaye Clatous Chama kuongeza bao la pili dakika ya 67 wakati dakika ya 72 Idrissa Diomande kufunga bao la tatu. Jumla Singida Black Stars inatinga makundi kwa mabao 4-2.

Ahadi ya bilioni 1 zawatokea puani Vipers, yatupwa nje na Power Dynamos

Licha ya kuahidiwa Tsh  Billion 1.7 iwapo wataiondoa Power Dynamos  na kutinga hatua ya Makundi CAF Champions League Vipers SC wameshindwa kufua dafu mbele ya wababe hao wa soka nchini Zambia. Rasmi Vipers SC Wameondoshwa kwenye Mashindano kwa Jumla ya Aggregate (3-2) ambapo mchezo wa leo umetamatika kwa Sare ya  (1-1).

Injinia Hersi atamba leo kutambulisha kocha mkubwa duniani

Rais wa klabu ya Yanga Sc Eng.Hersi Said amethibitidha usiku wa leo klabu yao itamtambulisha kocha mkuu kutoka Ulaya  ambaye ana uwezo na uzoefu mkubwa  Hersi Said “Tumefanya maamuzi sahihi na usiku wa leo yanga itatambulisha kocha bora kutoka Ulaya tutatambulisha kocha mwenye Ubora, Experience Kubwa, kocha atakayetuvusha kwenye mashindano haya kwenda hatua inayofuata”. “Habari hii Nzuri inakuja kwenu wananchi na Leo tutamtambulisha usiku huu kama Zawadi kwenu kwa kutuunga mkono”.

Minziro hatihati BigMan

Fred Minziro amekuwa na mwanzo mbaya akiwa na kikosi cha BigMan ambapo mpaka sasa amepoteza michezo 3 mfululizo ambayo ameiongoza timu hiyo huku timu wakiwa hawajafunga goli lolote. Timu hiyo ya Minziro imepoteza dhidi ya TMA 1-0, Mbuni 2-0 na Kagera Sugar 1-0, michezo ya BigMan inayofuata ni dhidi ya Barberian,  Polisi Tanzania, Songea United  na Kengold

Yanga kwa mbinde yatinga makundi Ligi ya mabingwa Afrika

TIMU ya Yanga imefanikiwa kwenda Hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Silver Strikers ya Malawi jioni hii Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga SC leo yamefungwa na beki Dickson Nickson Job dakika ya sita na kiungo Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua dakika ya 34. Kwa matokeo hayo, Yanga wanatinga hatua ya makundi kwa ushindi wa jumla wa 2-1 kufuatia kufungwa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Jumamosi iliyopita katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Pili Uwanja wa Taifa wa Bingu Jijini Lilongwe nchini Malawi. Bao pekee la Silver Strikers siku hiyo lililoizamisha Yanga lilifungwa na kiungo mshambuliaji Andulu Yosefe dakika ya 76 akimalizia kazi nzuri ya kiungo Uchizi Vunga. Droo ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kwa pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika itapangwa Jumatatu ya Novemba 3 katika studio za SuperSport Jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambao ni washirika wa Matangazo wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuanzia...

Pedro Goncalves kocha mkuu Yanga SC

Yanga SC wamemuajiri kocha wa zamani wa vilabu vya Sporting Lisbon, De Agosto na timu ya taifa ya Angola,Pedro Valdemar Soares Gonçalves (49). Kama nilivyoripoti jana kwamba Pira Ureno linakuja Jangwani,now nathibitisha kwamba Pedro Valdemar Soares Gonçalves ni kocha mpya wa Yanga. Ikumbukwe kocha huyo aliifikisha Angola hatua ya robo fainali kwenye AFCON iliyopita.

Mike Tyson aitembelea DR Congo na kudai alikotoka babu yake

NGULI wa Masumbwi, Mike Tyson amezungumzia safari yake ya hivi karibuni nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Nchi ambayo ameitaja kama asili ya mababu zake alipowasili Nchini humo kushiriki maadhimisho ya miaka 50 ya pambano la kihistoria “Rumble in the Jungle”, lililowakutanisha mabondia maarufu Muhammad Ali na George Foreman mwaka 1974. Katika chapisho lake rasmi la leo Oktoba 24, 2025 kwenye mitandao ya kijamii, Tyson ameweka picha kadhaa akiwa Jijini Kinshasa, ambako pia alialikwa kwa shughuli maalum za kitaifa na kitamaduni na kukutana na Rais wa DRC, President Félix Tshisekedi huku akielezea ziara hiyo kama uzoefu wa kubadilisha maisha akionyesha kupendezwa sana na nchi hiyo na watu wake na kuahidi kurejea tena Nchini humo. Ujio wa bingwa huyo wa zamani wa uzito wa juu nchini DRC ulijumuisha ziara za kitamaduni na ushirikiano yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa michezo na burudani kati ya nchi hiyo na watu mashuhuri duniani. Mkutano wake na Rais Tshisekedi katika ikulu ya K...

Paul Peter Kasunda ameanza msimu wa ligi ya NBC vizuri, kapachika mabao matatu sasa

Mshambuliaji Paul Peter Kasunda ameanza vizuri NBC Premier League 2025/26.. Amefunga magoli matatu kwenye mechi tano alizocheza akiwa na JKT Tanzania.. Anatupa muendelezo wa kile alichokifanya msimu wa 2024/25 akiwa na Dodoma Jiji alimaliza na magoli 8. Kwa jinsi JKT Tanzania wanavyocheza na kutengeneza nafasi huwenda @kasunda51 atafunga magoli mengi zaidi ya yale ya msimu uliopita. Kwenye orodha ya washambuliaji hatari zaidi wa kizawa kwasasa jina la Paul Peter Kasunda lipo.

Azam FC yatinga makundi kombe la Shirikisho kwa kipigo cha mbwa mwizi

TIMU ya Azam FC imetaka tiketi ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya KMKM ya Zanzibar katika mchezo wa marudiano wa Hatua ya 32 Bora leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Azam FC inakwenda Hatua ya makundi inayoshirikisha timu 16 kwa ushindi wa jumla wa 9-0 kufuatia ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza Oktoba 18 Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Mabao ya Azam FC yamefungwa na winga Iddi Suleiman Ali ‘Nado’, mawili dakika ya 23 na 43, mshambuliaji Mkongo, Bola Jephte Kitambala mawili pia dakika ya 27 na 30, beki Paschal gaudence Msindo dakika ya 48 na Abdul Khamis Suleiman ‘Sopu’ mawili pia dakika ya 54 na 57. Watoto wa Bilionea, Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa – Abubakar Bakhresa na wadogo zake, Omar Bakhresa na Yussuf Bakhresa wamiliki wa Azam FC wote walikuwepo uwanjani kushuhudia mchezo timu ikiweka rekodi mpya katika historia yake. Droo ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho kwa pamoja na Ligi ya Mab...

Karabaka ainusuru JKT Tanzania kulala mbele ya Mbeya City

BAO la kiungo mshambuliaji, Saleh Karabaka dakika ya 90’+4 limeisaidia JKT Tanzania kupata sare ya 2-2 na Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar e Salaam. Ilikuwa mechi tamu ya funga nikufunge, Mbeya City wakitangulia kwa bao la Hamad Majimengi dakika ya 15, kabla ya Paul Peter kuisawazishia JKT Tanzania – lakini Vitalis Mayanga akaifungia timu kutoka mkoa wa Mbeya bao la pili dakika ya 75 kabla ya Karabaka kusawazisha. Kwa matoke ohayo, Mbeya City inafikisha point inane katika mchezo wa sita na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi moja zaidi ya JKT Tanzania ambayo pia ina mechi moja mkononi. 

Yanga itashambulia mwanzo mwisho- Mabedi

Kaimu kocha mkuu wa Yanga SC, Patrick Mabedi amesema katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Silver Strickers, watashambulia mwanzo mwisho-. "Kesho tunatakiwa kushambulia tu hatutakiwi kukaa nyuma. Tayari wapinzani wetu wako mbele kwa goli moja na tunatakiwa kuhakikisha tunashinda mchezo wa kesho ili tusonge mbele na huo ndo ukweli na wala hakuna njia nyingine", "Kwenye mpira kila mchezo una presha na sisi tunaishi kwenye hiyo presha na tunajua kuna presha kubwa hasa kwa mashabiki wetu lakini jambo la muhimu kwenye mchezo wa kesho nikufanya vizuri na kusonga mbele ili kuondoa hiyo presha na Wachezaji wote wamejiandaa vizuri na wako tayari kuipambannia nembo ya Klabu yetu” Tulianza kambi yetu Jumanne baada ya mchezo wetu wa kwanza dhidi ya Silver Strikers, Malawi. Wachezaji wamejiandaa vizuri na kuna nguvu kubwa, hamasa na ari baina yao kuelekea mchezo huu muhimu wa kesho", Amesema Kaimu kocha mkuu wa Yanga SC, Patrick Mabedi

Kocha KMKM awaonya Azam FC

Kocha mkuu wa KMKM ya Zanzibar Hababuu Omar ameoneshwa kuhuzunishwa na tabia za mashabiki wa Tanzania hususani upande wa Zanzibar kua hawapendi timu zao za Zanzibar hali inayopelekea wachezaji kucheza bila support ya mashabiki  Pia amesema amezungumza na makocha zaidi ya wanne kutokea Zanzibar ambao nao wamekili kua hua wanafurahia zaidi kucheza nje ya Zanzibar kuliko ndani ya Zanzibar Katika hatua nyingine kocha huyo amesema wanajiona kama wapo nyumbani na watatoa ushindani mkubwa kwa Azam FC baadaye leo.

Silver Strickers yawasili Dar es Salaam kuikanda Yanga

Kikosi cha Wachezaji wa Silver Strikers wamewasili nchini kujiandaa na mchezo wa marudiano ya mchezo wa awali wa kufuzu hatua ya makundi dhidi ya Yanga SC. . Silver Strikers wametanguliza mguu mmoja mbele baada ya kushinda mchezo qa kwanza kwa bao 1-0 huko nchini Malawi 

Hakim Zeyich atambulishwa Wydad Casablanca

Klabu ya Wydad Casablanca imemtambulisha Kiungo Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Hakim Ziyech  ambaye amejiunga na Klabu hiyo kwa Mkataba wa Mwaka mmoja. Ziyech ameonesha kufurahishwa na kujiunga na miamba hiyo baada ya kukaa nje ya Uwanja kwa mda wa miezi minne na leo ataanza mazoezi rasmi na Wydad. . Safu ya Ushambuliaji ya Wydad huenda ikabadilika kutokana na ujio wa Supa Staa huyo ambapo inaweza kuongozwa na Amrabat, Lorch, Aziz Ki na Hakim Ziyech 

Kocha Nsingizini Hotspurs asema walicheza vizuri kuliko Simba

Kocha wa timu ya Nsingizini Hotspurs ya Eswatini, Mandela Qhogi amesema kwamba katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya Simba na kufungwa mabao 3-0, walicheza vizuri zaidi ya Simba ila walichezewa rafu nyingi. "Tulicheza vizuri kuliko Simba SC, wao muda mwingi walicheza mchezo mchafu kujidondosha kuua moments zetu za kushambulia" "Naamini ni mbinu wataitumia mchezo wa marudiano kupaki basi na kujidondosha ila tutashambulia kupindua matokeo" -Mandla Qhogi, kocha mkuu wa klabu ya Nsingizini Hotsupers FC

Mota Maria kuchukua nafasi ya Folz, Yanga SC

Mota Maria ni kocha mwenye uzoefu barani Afrika na Asia, ambapo amewahi kuzinoa timu kama Al Hilal Omdurman ya Sudan na Al Hussein SC ya Jordan. Anatambulika kwa mbinu ya kucheza soka la pasi chini (ground football), akisisitiza umiliki wa mpira na nidhamu ya kiufundi uwanjani. Mota Maria alizaliwa Septemba 16, 1966, na aliwahi kucheza kama beki. Alipitia katika vikosi vya vijana vya FC Barreirense na Sporting CP. Alistaafu soka mwaka 2000. Mfumo wake pendwa kiwanjani ni 4 - 2 - 3 - 1 mfumo ambao hata Yanga wameutumia kwa miaka mitano mfululizo  Kwa sasa, anahudumu kama kocha wa Saham Club nchini Oman. Wakati huu anahusishwa kujiunga na Young Africans Sports Club kuja kuziba nafasi ya Romain Folz

RC Amos Makalla ataka Arusha kuwa na timu ya Ligi Kuu, akubali kuwa mlezi wa Mbuni

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA. Amos Gabriel Makalla, rasmi amekubali kuwa Mlezi wa Timu ya mpira wa Miguu ya Mbuni FC yenye Makao yake Makuu Mkoani humo, kufuatia ombi lililowasilishwa kwake na JWTZ Brigedi ya Kanda ya Kaskazini.  CPA. Makalla ameanza ulezi huo rasmi leo Oktoba 23,2025, alipokutana na kuzungumza na Menejimenti na Wachezaji wa timu hiyo na kutoa shilingi milioni 13.5 kwa ajili ya posho na motisha kwa wachezaji huku akiwataka kuanza safari ya kuipandisha timu hiyo ili kucheza Ligi kuu, kama sehemu ya kukuza utalii wa Michezo Arusha. Aidha, CPA Makalla ametoa vyakula  na televisheni kwaajili ya kambi ya timu hiyo huku Uongozi wa Timu hiyo ukimshukuru kwa motisha na kukubali kuwa mlezi wa timu hiyo, na kuahidi ushindi kwa michezo ijayo. Awali, CPA Makalla ameitaka timu hiyo kuweka malengo  ya kushinda mechi zote za nyumbani, na kusisitiza kuwa Serikali ya awamu ya sita inajenga viwanja vya michezo pamoja na uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu, ikiwa ni maand...

Silver Strickers haoo kuwavaa Yanga SC Jmosi

Kikosi cha wachezaji 23 cha Silver Strikers kimeondoka nchini Malawi hii leo kuja Jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya mchezo wa pili wa mtoano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Yanga SC katika Uwanja wa Benjamin Mkapa. Silver Strickers walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga katika mchezo wa kwanza ambapo inahitaji sare yoyote Ili kutinga makundi.

Mecky Mexime kumrithi Mayanga, Mashujaa FC. soma zaidi

Mecky Mexime ndiye anatajwa kurithi mikoba ya Salum Mayanga ndani ya kikosi cha Mashujaa FC ,Ikumbukwe kuwa Kwa sasa Mexime hana timu anayofundisha baada ya kuachana na Kagera Sugar msimu uliopita. Mecky ni kocha mwenye uzoefu mkubwa na soka la Tanzania akiwa amewahi kufundisha kwenye Vilabu vya Mtibwa Sugar ,Kagera Sugar,Ihefu pamoja na Dodoma Jiji.

MENEJA MKUU WA SIMBA SC NI MKUBWA KULIKO KOCHA MKUU

Na Prince Hoza Matua WATU wanajiuliza nani mkubwa kicheo ndani ya klabu ya Simba SC kati ya Meneja mkuu na kocha mkuu, kwa maana ya Dimitar Pantev na Seleman Matola. Hiyo yote inatokana na madaraka yao kikazi kugawanywa na Shirikisho la soka nchini, TFF, ambapo Shirikisho hilo halimtambui Pantev kama kocha mkuu na badala yake linamtambua Seleman Matola. TFF kwa sheria zao linamtambua kocha mwenye leseni ya CAF A kusimama kwenye benchi la timu husika katika mashindano yake kwa maana Ligi Kuu bara, kombe la CRDB na Ngao ya Jamii. Pantev hakidhi vigezo hivyo klabu ya Simba SC limemtambulisha kama meneja mkuu na badala yake Seleman Matola anahesabika kama kocha mkuu, mashabiki wa Simba SC wale wasioelewa wanachukulia Pantev kama mdogo wa Matola. Na sasa Matola anaonekana kama kocha mkuu hivyo Simba SC haijafanya kitu chochote baada ya kuondoka Fadlu David's ambaye alikuwa kocha mkuu na Matola alikuwa kocha msaidizi namba tatu. Fadlu wakati anajiunga na Simba, aliambatana na msaidizi wa...