Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MENEJA MKUU WA SIMBA SC NI MKUBWA KULIKO KOCHA MKUU

Na Prince Hoza Matua

WATU wanajiuliza nani mkubwa kicheo ndani ya klabu ya Simba SC kati ya Meneja mkuu na kocha mkuu, kwa maana ya Dimitar Pantev na Seleman Matola.

Hiyo yote inatokana na madaraka yao kikazi kugawanywa na Shirikisho la soka nchini, TFF, ambapo Shirikisho hilo halimtambui Pantev kama kocha mkuu na badala yake linamtambua Seleman Matola.

TFF kwa sheria zao linamtambua kocha mwenye leseni ya CAF A kusimama kwenye benchi la timu husika katika mashindano yake kwa maana Ligi Kuu bara, kombe la CRDB na Ngao ya Jamii.

Pantev hakidhi vigezo hivyo klabu ya Simba SC limemtambulisha kama meneja mkuu na badala yake Seleman Matola anahesabika kama kocha mkuu, mashabiki wa Simba SC wale wasioelewa wanachukulia Pantev kama mdogo wa Matola.

Na sasa Matola anaonekana kama kocha mkuu hivyo Simba SC haijafanya kitu chochote baada ya kuondoka Fadlu David's ambaye alikuwa kocha mkuu na Matola alikuwa kocha msaidizi namba tatu.

Fadlu wakati anajiunga na Simba, aliambatana na msaidizi wake, ingawa klabu ya Simba SC ilikuwa na kocha wake msaidizi ambaye ni Matola, Fadlu aliamua kuondoka Simba baada ya kutokuwa na maelewano mazuri na viongozj wa klabu hiyo.

Fadlu aliondokea nchini Botswana wakati Simba ilipoenda kucheza na timu ya Gaborone United mchezo wa Ligi ya mabingwa Afrika raundi ya awali mchezo wa kwanza ambapo Simba ilipata ushindi wa bao 1-0 goli ambalo lilisaidia kuwavusha raundi ya kwanza.

Simba iliingia raundi ya kwanza baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 katika mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, timu ikinolewa na Hemed Morocco kwa muda.

Baada ya hapo uongozi wa Simba SC ulihaha kutafuta kocha mpya, ambapo Dimitar Pantev raia wa Burgalia alichukua mikoba ya Fadlu, Pantev alikuwa Meneja mkuu wa Gaborone United na alisifika kwa kuifundisha vizuri timu hiyo ingawa iliondoshwa na Simba katika raundi ya awali.

Aina ya uchezaji wake mzuri dhidi ya Simba, ilitosha kuwavutia wengi wakiwemo wachambuzi wa soka nchini na kuishauri Simba imchukue haraka baada ya kuondoka Fadlu, katika mchezo dhidi ya Simba na Gaborone, Pantev alifanya kazi kubwa Uwanjani na almanusura aitoe Simba.

Sare ya kufungana bao 1-1 kidogo iwaondoshe Simba katika mashindano, isipokuwa ushindi wa bao 1-0 ugenini iliwabeba Simba na kusonga mbele, kuanzia mechi ya kwanza jijini Gaborone na jijini Dar es Salaam, Pantev alitawala vipindi vyote.

Ilikuwa ngumu Simba kuleta kocha mwingine badala ya Pantev, kwa sababu Pantev alionekana ana uwezo mkubwa na Simba ilihitaji kocha mwenye uwezo mkubwa bila kujali wasifu wake.

Ingawa kwamba Simba ilikuwa na kocha Fadlu aliyeiwezesha timu hiyo kufika fainali ya kombe la Shirikisho Afrika, kiwango cha Simba kilikuwa cha kawaida, lakini kwa ujio wa Pantev, ni dalili kwamba Simba imerejea kwenye kiwango chake.

Pantev ni kocha mzuri na ataweza kuifikisha katika mafanikio, kuhusu ukubwa kati yake na Matola ambaye atahesabika kama kocha mkuu na Pantev meneja mkuu, utofauti wao utabaki pale pale ila Pantev ambaye ni Meneja mkuu atakuwa mkubwa dhidi ya Matola ambaye ni kocha mkuu.

Pantev ana leseni A ya UEFA ambayo inamfanya asimame kama kocha mkuu kwenye michuano ya CAF, lakini kwenye mashindano ya ndani yanayotambuliwa na TFF atampisha Matola na Pantev atakuwa meneja mkuu.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa