Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2024

Yanga sasa kucheza na bingwa wa Kagame, wiki ya Wananchi

Picha
Klabu ya Yanga imetangaza kwamba watacheza dhidi ya Mabingwa wa Michuano ya KAGAME Cup,Red Arrows kutoka Zambia kwenye Kilele cha Wiki ya Mwananchi kitakachofanyika Agosti 04,2024 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Awali klabu ya Yanga iliwaandikia maombi Wydad Casablanca ili kusudi wakutane nao katika wiki ya Wananchi lakini imeshindikana na sasa watakutana na mabingwa wa kombe la Kagame Cup, Red Arrows ya Zambia

Msimu ujao Yanga itaalikwa Ulaya- Dauda

Picha
Mchambuzi wa michezo Shafih Dauda amesema hatoshangaa msimu ujao klabu ya Yanga ikialikwa barani Ulaya kwenye mechi za pre season na hasa kutokana na kwenda nchini Afrika Kusini. "Nimefuatilia Pre Season ya Yanga kwa maana maandalizi yao ya msimu mpya wakiwa hapa nyumbani na baadae kwenda Afrika Kusini kwa mualiko maalumu na hivi vitu haviji tu ni lazima kuna mbegu unakuwa umeipanda baada ya muda ndio unaona shina na matunda yake , Yanga wamefanikiwa kwenye hilo hasa matokeo ya jumla ya mechi zao" "Hii imefanya wauze sana na sitoshangaa kama msimu ujao watapata mialiko mingi zaidi" amesema Shafih Dauda

Simba yasajili mbadala wa Lakred

Picha
Klabu ya Simba imefikia makubaliano ya kumsajili golikipa wa timu ya Guinea, Moussa Camara mwenye umri wa miaka 25 kutoka Horoya AC ya Guinea. Simba imeamua kumsajili kipa huyo baada ya kipa wake nambari moja Ayoub Lakred kuumia na atakaa nje kwa miezi sita na pia viongozi wa klabu wakishindwa kumuelewa kipa Aishi Manula

Diamond afanya balaa Barcelona

Picha
Msanii Diamond Platnumz amefanya shoo usiku wa kuamkia leo, Julai 29, Diamond alifanya shoo ya kibabe kabisa huko Barcelona, Uhispania kwenye event ya Afrobrunch. Tukio linalojulikana kwa kuadhimisha muziki na tamaduni za Afrobeats..... Sio mchezo, Diamond alipiga mzigo na kuacha mashabiki hoi na vichwa juu!, kwa kuimba nyimbo zake pendwa huku akipata mwitikio mkubwa kutoka kwao. Hii ilikuwa ni show ya pili masaa kadhaa baada ya ku-perform kwenye show ya Afro Land huko Ujerumani, Julai 27

Alikamwe kumpisha Manara Yanga

Picha
Aliyekuwa Meneja wa Mawasiliano wa Klabu ya Yanga,Ally Kamwe baada ya kuhudumu kwa misimu miwili kama Meneja wa idara ya Habari na Mawasiliano Yanga SC,leo ameandika barua ya kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kuitumikia kwa mafanikio. Kamwe alianza kazi Yanga September 25,2022 ,leo July 29 amejiuzulu taarifa rasmi itatolewa muda wowote kuanzia sasa licha ya kuwa kwenye maongezi na Uongozi wa Yanga juu ya kuongeza Mkataba mpya lakini amesitisha rasmi suala hilo.

Kimenya ajiunga Fountain Gate. Soma zaidi

Picha
Nyota wa zamani wa Mbeya City,Mtibwa Sugar na Dodoma Jiji FC,Salum Kihimbwa amejiunga na Fountain gates kama mchezaji huru kwa mkataba wa mwaka mmoja. Fountain Gates imeweka kambi wilayani Babati Mkoa wa Manyara kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu Bara 2024/25

Yammi amtaja Mbosso

Picha
Msanii Yammi ameweka wazi kuwa na mahusiano ya Kimapenzi na Mbosso, Sio siri tena Yammi amemtaja Mpenzi wake akiwa katikati ya mahojiano na waandishi wa habari. Amefunguka hayo pindi alipokutana na surprise ya Msemaji "BabaLevo" ambaye alikuja kufuta kitendawili cha Mwanaume ambaye. Yammi anasema yupo nae kwa sasa akiwa mwenye furaha nzito.... Kwa mujibu wa Baba Levo anadai kuwa Yammi yupo kwenye Penzi zito na Mwanamuziki kutoka WCB "Mbosso".

Ayoub Lakred nje miezi 6

Picha
Golikipa, Ayoub Lakred atakaa nje ya uwanja kwa miezi sita. Simba SC imeshakamilisha usajili wa golikipa mwingine, Moussa Camara kutoka Horoya AC. Ayoub ataondolewa kwenye mfumo wa (CAF) ili kumpisha kipa mpya kwa sababu idadi ya wachezaji wa kigeni itazidi. Aishi Manula hana maelewano mazuri na uongozi wa Simba SC hivyo ni ngumu kurejea kikosini. Anashutumiwa kwa kufungwa bao 5-1 na Young Africans Sports Club.

Gamondi amduwaza Nabi, Yanga ikiichapa Kaizer 4-0

Picha
Yanga SC chini Miguel Gamondi jioni ya leo imeichapa Kaizer Chief inayonolewa na Kocha wa zamani wa Yanga, Nasreddine Nabi mabao 4-0 kwenye uwanja wa Toyota mchezo wa kuwania kombe la Toyota. Prince Dube dakika ya 25 amefungua ameendelea kufunga baada ya kuiandikia bao la Kwanza kabla ya Stephanie Aziz Ki dakika ya 45 kufunga bao la pili. Clement Mzize dakika ya 57 alifunga bao la tatu kabla ya Aziz Ki ambaye leo ameshinda tuzo ya mchezaji bora, Aziz Ki alifunga bao hilo dakika ya 62. Baada ya ushindi huo Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa Toyota Cup

Nina deni na Yanga- Diamond Platinumz

Picha
"Nimepokewa vizuri sana tangu nijiunge Yanga nina raha tangu wakati huo hadi sasa. Kwa raha nilizopata toka niwe MWANANCHI nina zawadi yao, nahisi nina deni nao” "Jezi za Yanga ni tofauti na wengine, unaweza kuvaa sehemu yoyote, hata kwenye show zangu nitavaa" Diamond Platnumz akiongea na Azam TV

Chley Nkose amshukuru Diamond Platinumz

Picha
Msanii kutoka Afrika Kusini Chley Nkosi" ametoa shukrani zake kwa staa wa bongofleva Diamond Platnumz hii ni baada ya Diamond Platnumz kumshirikisha kwenye nyimbo kadhaa . Kupitia ukurasa wake wa Instagram mrembo Chley ametoa shukrani kwenye hilo na ameamua kumshukuru Diamond waziwazi.

Debora amfunika mbaya Ngoma na kutakiwa aondoke kikosini

Picha
Siku za mchezaji wa Simba SC Fabrice Luamba Ngoma raia wa DR Congo zinahesabika kwani tayari kocha wa klabu hiyo Fadlu Davids raia wa Afrika Kusini ameshamkataa na anataka atupiwe virago. Lakini adui wa maisha ya Ngoma aliyesajiliwa kwa madaha msimu uliopita ni kiungo mpya kutoka Angola mwenye uraia wa Congo Brazaville Debora Fernandez Mavambo ambaye amekuwa akikichafua vibaya mno kiasi kwamba kocha anamuona Ngoma kama mzululaji uwanjani

Ahmed Ally abeba tuzo za WAKITA

Picha
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba SC Ahmed Ally ametunukiwa tuzo ya heshima ya matumizi fasaha ya lugha ya kiswahili kutoka kwa Watetezi wa Kiswahili Tanzania (WAKITA). Katika hafla ya utoaji tuzo kwa watetezi wengine wa lugha ya kiswahili, mgeni wa heshima alikuwa Rais mstaafu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Dkt Jakaya Kikwete ambaye pia alimkabidhi tuzo hiyo

Yanga watambulisha jezi za mpya 2024/2025

Picha
Mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga SC leo wametambulisha jezi zao mpya ambazo watazitumia msimu ujao. Agosti 4 mwaka huu Yanga wataadhimisha tamasha lao la Wiki ya Wananchi ambapo mbali ya kutambulisha kikosi chao pia watatambulisha na jezi zao mpya zenye rangi ya njano, kijani na nyeusi

Paul Godfrey Boxer atua Songea United

Picha
Beki wa zamani wa Yanga, Paul Godfrey ‘Boxer’ amejiunga na Songea United (zamani FGA Talents) iliyopo Ligi ya Championship, ili kuongeza nguvu katika kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao.  Uongozi wa timu hiyo umeona kiwango cha Boxer, kitawasaidia kutokana na uzoefu wake alionao baada ya kucheza timu tofauti za Ligi Kuu ambapo msimu ulioisha alikuwa Ihefu (sasa Singida Black Stars).

Mangungu aongoza Ibada ya kuunusuru uongozi Simba usipinduliwe

Picha
Mwenyekiti wa Klabu ya Simba SC Murtaza Mangungu hii leo ameongoza dua ya kuwaombea viongozi wa klabu hiyo pamoja na timu kufanya vizuri kuelekea kwenye msimu mpya wa 2024 - 25 Dua hiyo imefanyika katika uwanja wa Mo Simba Arena, Bunju. Simba imeamua kufanya dua hiyo kutokana na mwenendo wake kuwa mbaya msimu uliopita na kuambulia nafasi ya tatu kwenye Ligi Kuu bara huku ikitolewa Ligi ya mabingwa hatua ya robo fainali

Mzee Magoma azidi kumkalia kooni Injinia Hersi

Picha
Pale Yanga SC kuna makundi ukionekana wewe siasa zako zinaenda kinyume na wao wanakuweka pembeni. Mimi siwezi kuwa mtumwa wao hata siku moja nitaendelea kusimamia kwenye katiba. Kwa sasa siwezi kwenda pale klabuni kwasababu nimeomba serikali inirinde sasa nikienda pale wakati nimeshawasha moto si itaonekana nimejitakia. Mimi nimekataa kutumika kama wengine,hauwezi kuona nimekaa pale nasuburi viongozi wanipe mia mbili, amesema mzee Magoma

Stephanie Aziz Ki aweka rekodi Ligi Kuu bara tangu 2005

Picha
Wafungaji bora Ligi Kuu Tanzania bara tangu mwaka 2004 | 5 hadi sasa (20 yrs) : ◉ 2005 - Abu. Mkangwa ›› Mtibwa - 16 ◉ 2006 - Isse Abshir ›› Simba - 19 ◉ 2007 - Abdallah Juma ›› Mtibwa - 20 ◉ 2008 - M. Katende ›› Kagera - 11 ◉ 2009 - Boni Ambani ›› Yanga - 18 ◉ 2010 - Mussa Mgosi ›› Simba - 18 ◉ 2011 - Mrisho Ngassa ›› Azam - 18 ◉ 2012 - John Bocco ›› Azam - 19 ◉ 2013 - Kipre Tchetche ›› Azam - 17 ◉ 2014 - Amiss Tambwe ›› Simba - 19 ◉ 2015 - Simon Msuva ›› Yanga - 17 ◉ 2016 - Amiss Tambwe ›› Yanga - 21 ◉ 2017 - Msuva & Abdulrahman - 14 ◉ 2018 - Emmanuel Okwi ›› Simba - 20 ◉ 2019 - Meddie Kagere ›› Simba - 23 ◉ 2020 - Meddie Kagere ›› Simba - 22 ◉ 2021 - John Bocco ›› Simba - 16 ◉ 2022 - George Mpole ›› Geita - 17 ◉ 2023 - Mayele & Ntibazonkiza - 17 ◉ 2024 - Stephane Aziz Ki ›› Yanga - 21 ◉ 2025 - ?! Tangu uanzishwe mfumo wa timu (16), hakuna mchezaji aliyefunga magoli mengi ndani ya msimu (1) kuliko Aziz Ki. John Bocco, Simon Msuva, Meddie Kagere na Amissi Tambwe ndio wachezaji

Irene Uwoya aitosa Yanga na kutupia jezi ya Simba

Picha
Mjadala mkubwa umeibuka mitandaoni baada ya mwigizaji wa filamu Irene Uwoya kuonekana akiwa ametupia Jezi ya Simba huku walio wengi wakidai kwamba yeye ni Yanga damu na ushahidi wa video yake ukiwekwa hadharani. Lakini staa huyo wa filamu ameonekana kuvalia jezi mpya ya Simba SC na slipoulizwa kwanini amevaa. Jezi ya Simba wakati yeye ni Yanga akajibu kwamba amepewa azitamgaze kwakuwa yeye ni msanii. *Kazi yangu inaniruhusu kuvaa jezi ya timu yoyote kama nikipewa tenda navaa na kuitangaza, lakini mimi ni Yanga damu", alisema staa huyo aliyewahi kuolewa na Dogo Janja na kubadili dini

Aishi Manula kurejeshwa kikosini Simba SC

Picha
Kinachosubiriwa kwa sasa ni taarifa tu juu ya kurejea kikosini Simba SC na kuendelea na majukumu yake ya kila siku licha ya kukosekana kwa muda katika kipindi hiki cha Pre-season wakati Klabu hiyo ikiwa nchini Misri. Aishi Manula aliachwa Tanzania pasipo kujua sababu yake, Ayoub Lakred ni Majeruhi na atakaa nje ya uwanja kwa zaidi ya mieiz mitatu. Kwa sasa kitu ambacho kimewafanya Viongozi wa Simba kuamua kumrejesha Aishi Manula kikosini na kumfanya kuwa chaguo la Kwanza. Tegemea tena kumuona Aishi Manula Langoni, Siku ya Tarehe 08, August.

Agosti 3 Simba kumtambulisha Mpanzu

Picha
Na Salum Fikiri Jr Klabu ya Simba SC maarufu Wekundu wa Msimbazi Agosti 3 mwaka huu wakati wa tamasha lake la Simba Day inatarajia kumtambulisha winga Elie Mpanzu toka DR Congo kama mchezaji wake mpya. Simba itamkata Willy Onana  baada ya kocha wa Wekundu hao kumkataaa mazima na hivyo mabosi wa timu hiyo wamelazimika kumfuatilia Mpanzu na kuongeza dau analolitaka. Simba ilishaachana na Mpanzu na kuamua kumtumia tiketi ya ndege Onana na kusafiri kuwafuata wenzake waliotangulia Misri, lakini jana Simbaisha kocha wa timu hiyo amemkataa waziwazi Onana na kutaka aletwe fasta mbadala wake ama sivyo timu itayumba kwenye Ligi na michuano ya kimataifa. Jumamosi hii, kama mambo yakienda sawa atatambulishwa kwenye Simba Day, kama wakimpata Mpanzu watakwenda kugombea msimu ujao; Wakongomani wameniambia Mpanzu ni namba 10 ambaye muda mwingine anacheza kama winga kilisema chanzo changu

Kocha Simba amtupia virago Onana

Picha
Wakati jana Mambo Uwanjani Blog ikimnukuu kocha wa Simba Fadlu Davids kwamba hana imani na kikosi chake kilichopo Ismailia, Misri. Leo kocha wa klabu hiyo Fadlu Davids ameuomba uongozi wa Klabu kumtafutia mbadala wa Mchezaji Willy Essomba Onana kwani ameonekana kutokufurahishwa na namna Mchezaji huyo anavyosakata Kabumbu. Na hii inafanya kutimia idadi ya wachezaji watatu waliokataliwa na Kocha Fadlu akiwemo Freddy Michael na Ayoub Lakred kutokana na uzito mkubwa hadi kulazimika kumuanzishia Programu ya pekee yake ili kurudisha utimamu wa mwili iliyomfanya kupata majeraha Kipa huyo.

Simba kurejea Jtano ijayo

Picha
Klabu ya Simba SC ya Tanzania inatarajia kurejea Dar es Salaam Jumatano ya Julai 31 kwaajili ya Simba Day 2024 na kuuanza rasmi msimu wa 2024 - 25. Maadhimisho ya Simba Day yatafanyika Agosti 3 ambspo Wekundu hao wa Msimbazi watashuka dimbani kucheza na APR ya Rwanda. Simba pia itatumia nafasi hiyo kutambulisha wachezaji wake wapya na wa zamani pamoja na Benchi lake la ufundi, mbali ya timu ys wanaume kucheza na APR, timu ya wanawake nayo itacheza mchezo wa kirafiki

Matampi aungana na wenzake Coastal Union

Picha
Mlinda mlango wa Coastal Union,Ley Matampi [kulia] tayari amerejea nchini na atajiunga na wachezaji wenzake ambao tayari wameingia kambini kujiandaa na msimu mpya. Msimu uliopita Ley alifanikiwa kupata cleansheet 15 Ligi Kuu na kuwapiku walinda milango wengine wote ndani ya jumba la ladha na hekaheka.

Simba wasimng' ang' anie Kibu- Rage

Picha
Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amewaomba viongozi wa Simba SC kutomng'ang'ania winga, Kibu Denis. "Kibu Denis ameonyesha kutokuwa mwaminifu na huenda akawa sehemu ya wahujumu Simba SC msimu unaofuata. Viongozi wa Simba hawapaswi kumng'ang'ania na nawasihi viongozi wa Simba wasimkomoe mchezaji bali atakaporejea wazungumze naye ili kila upande unufaike kulingana na makubaliano lakini wamruhusu aende zake." "Mimi niliwahi kukutana na kesi kama hiyo nilipokua katika harakati za kumsajili Mbuyu Twite ambaye licha ya kumpatia dola elfu (40) lakini akasaini pia na Yanga SC ambapo ili kuepusha mgogoro tulimueleza arudishe pesa tulizompa na kuongezea dola elfu tano" alisema Rage

Hii ndio timu iliyomteka Kibu Denis toka Simba SC

Picha
Klabu ya Kristiansund BK ya Norway imempa mualiko maalumu Kibu Denis ili kufanya majaribio. Akifuzu watamsajili. Atafanya majaribio hadi tarehe 8/8/2024. Timu hiyo imegharamia safari,Chakula na malazi,Pia ipo tayari kumgharamia kwa jambo lolote. Atafanya mazoezi na timu hiyo,na kucheza kwenye michezo ya kirafiki itakayokuwepo kwenye timu hiyo.

Kocha Simba aingia shaka na kikosi chake

Picha
Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba SC Tanzania inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC Premier League na Kombe la Shirikisho Barani Afrika, Davids Fadlu amesema kwa sasa anahitaji na timu iliyokamilika. Kwasasa Fadlu anahitaji awe na timu iliyotimamu kwa ajili ya kukabiliana na michezo mbalimbali katika michuano ambayo Simba Inashiriki "Itakapofika Siku ya Simba Day tutakuwa na wiki ya 4 na nusu ya pre season,na bado hatupo Fit kucheza dakika 90 za mchezo wa mpira wa miguu kwa sababu bado pia tunaunda Patterns mpya ndani ya timu "Itafikia Mpaka Wiki ya 6 ambapo tutakuwa tunaanza mchezo wetu wa kwanza wa Ligi Kuu NBC. Ni lazima tujipe muda kwa vile timu ni mpya kabisa,bado tunaunda timu kwa hivyo itatulazimu kufanya makosa kwa sababu tunatengeneza kitu kipya,tunahitaji kuwa na subira tu kwa sasa na tuende katika utaratibu mzuri alisema Fadlu

Makambo apata timu Ujerumani

Picha
Mshambuliaji aliyewika na Mtibwa Sugar Under- 20 ambaye baadae alijiunga na Mashujaa FC ya Kigoma, Athumani Makambo amesajiliwa na klabu ya Darmstadt ya daraja la pili Ujerumani. Makambo amesaini mkataba wa miaka mitatu, mshambuliaji huyo alionesha kiwango kikubwa na ilitabiriwa angefika mbali jambo ambalo limetimia

Rais Samia geukia na mchezo wa riadha, unaipeperusha vema bendera ya Tanzania

Picha
Na Prince Hoza #TupoNaMama katika upande wa michezo kwani mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya vizuri katika kipindi chake kifupi cha duru la kwanza la Urais wake wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania. Rais Samia amechukua Urais kutoka kwa mtangulizi wake Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki mwaka 2021, sio siri tangu alipochukua kijiti amefanya mambo mazuri ya kuendeleza miradi ya maenceleo aliyoikuta ikiwemo ujenzi wa barabara, reli na bwawa la Nyerere. Usafiri wa reli ya kisasa ya SGR imeanza kazi ambapo safari za Dar, Moro na Dodoma zimeanza huku umeme wa bwawa la Nyerere pia unatumika na barabara za mwendokasi nazo zinaendelea kujengwa. Bila shaka Rais Samia anafanya vema itakuwa dhambi hatutamsifia kwa hilo kwani mtangulizi wake hayati Magufuli alisifiwa sana na Watanzania kutokana na kuanzisha miradi hiyo mikubwa kabla ya kufariki ikiwa miradi haijakamilika, kitendo cha mama Samia kuikamilisha anahitaji sifa kemkem. Sifa nyingine anayostahili mama yetu Samia Suluhu Hassan ni

House girl wangu alinipa wazo la kujenga- Wolper

Picha
"Mimi wazo la kujenga nyumba nililipata kwa house girl wangu, nilikuwa namlipa mshahara kumbe alikuwa anatunza hadi siku aliyokuja kuniambia "Dada nashukuru kwa msaada wako mimi nimejenga nyumba kupitia mshahara wako" Hapo ndipo akili ikanijia kuwa kumbe hata mimi naweza kujenga nyumba kwa kusevu pesa kidogo kidogo" "Tangu hapo nilianza kusevu pesa kwa ajili ya nyumba na hatimae nikafanikiwa kujenga nyumba kubwa, nzuri ambayo thamani yake huenda ni zaidi ya shilingi milioni 500 za Tanzania ingawa bado haijaisha vizuri. Namshukuru house girl wangu kwa kunipa wazo" - Jacqueline Wolper, mwigizaji maarufu Tanzania pia mfanyabiashara

Kocha wa Wydad aula Saudi Arabia

Picha
Aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Wydad Casablanca, Josef Zinnbauer amejiunga na klabu ya Al Wahda kuwa kocha mkuu ambayo imeshuka daraja katika Ligi Kuu nchini Saudi Arabia. Josef alitimuliwa na Wydad Casablanca kutokana na mwenendo mbaya wa timu hiyo kwenye michuano yote ya ndani na nje na kuifanya timu hiyo kumaliza bila taji lolote. Sasa Wydad imempa mikoba kocha wa zamani wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini Rulani Mokwena

Dube afungua akaunti ya mabao Yanga ikiichapa TS Galaxy

Picha
Timu ya Yanga SC ya Tanzania jioni ya leo imeifunga timu ya TS Galaxy ya Afrika Kusini bao 1-0 katika uwanja wa Kalamazane katika mchezo wa michuano ya Mpumalanga Primier. Bao pekee la Yanga limefungwa na mshambuliaji wake mpya Prince Dube dakika ya 55, huo ni mchezo wake wa pili baada ya mechi ya kwanza kufungwa mabao 2-1 na Ausburg ya Ujerumani. Yanga itashuka tena uwanjani siku ya Jumapili ikichuana na Kaizer Chief pia ya Afrika Kusini kuwania kombe la Toyota

Mapya, Kibu Denis arudisha pesa zote za Simba

Picha
Kibu Denis amerudisha pesa zote za signing fee alizopewa na Simba SC kupitia Bank ya MMB kwenye account ya Simba,Kibu Denis yuko Norway kwa ajili ya mapumziko. "Sisi tunamtambua Kibu Denis kuwa bado ni mchezaji wetu, mchezaji wetu mtoro"

Simba yazindua jezi, neno Sanda laleta balaa

Picha
Klabu ya Simba SC leo imetambulisha jezi mpya watakazozitumia msimu ujao wa 2024/2025, lakini jezi hizo zimeleta tafrani baada ya neno la mbele kuandikwa "Sanda" jambo ambalo limewagawa mashabiki. Simba leo imezindua wiki ya Simba Day kwenye mbuga ya wanyama ya Mikumi mkoani Morogoro, hata hivyo jezi za msimu huu ni bora kuliko za misimu yote iliyopita ila neno Sanda limeleta tafrani