Kocha Simba amtupia virago Onana

Wakati jana Mambo Uwanjani Blog ikimnukuu kocha wa Simba Fadlu Davids kwamba hana imani na kikosi chake kilichopo Ismailia, Misri.

Leo kocha wa klabu hiyo Fadlu Davids ameuomba uongozi wa Klabu kumtafutia mbadala wa Mchezaji Willy Essomba Onana kwani ameonekana kutokufurahishwa na namna Mchezaji huyo anavyosakata Kabumbu.

Na hii inafanya kutimia idadi ya wachezaji watatu waliokataliwa na Kocha Fadlu akiwemo Freddy Michael na Ayoub Lakred kutokana na uzito mkubwa hadi kulazimika kumuanzishia Programu ya pekee yake ili kurudisha utimamu wa mwili iliyomfanya kupata majeraha Kipa huyo.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI