Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Rais Samia geukia na mchezo wa riadha, unaipeperusha vema bendera ya Tanzania

Na Prince Hoza

#TupoNaMama katika upande wa michezo kwani mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya vizuri katika kipindi chake kifupi cha duru la kwanza la Urais wake wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Rais Samia amechukua Urais kutoka kwa mtangulizi wake Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki mwaka 2021, sio siri tangu alipochukua kijiti amefanya mambo mazuri ya kuendeleza miradi ya maenceleo aliyoikuta ikiwemo ujenzi wa barabara, reli na bwawa la Nyerere.

Usafiri wa reli ya kisasa ya SGR imeanza kazi ambapo safari za Dar, Moro na Dodoma zimeanza huku umeme wa bwawa la Nyerere pia unatumika na barabara za mwendokasi nazo zinaendelea kujengwa.

Bila shaka Rais Samia anafanya vema itakuwa dhambi hatutamsifia kwa hilo kwani mtangulizi wake hayati Magufuli alisifiwa sana na Watanzania kutokana na kuanzisha miradi hiyo mikubwa kabla ya kufariki ikiwa miradi haijakamilika, kitendo cha mama Samia kuikamilisha anahitaji sifa kemkem.

Sifa nyingine anayostahili mama yetu Samia Suluhu Hassan ni kwenye upande wa michezo, kiongozi huyo mkuu wa nchi alipojngia madarakani aligeukia upande wa michezo hasa mchezo wa soka ambapo alianzisha kampeni yake iitwayo "goli la mama" kwa timu za Simba, Yanga na Taifa Stars.

Rais Samia aliingilia kati na kutoa tsh milioni 5 mpaka 10 kwa kila goli moja kwa wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika au kombe la Shirikisho kwa timu hizo za Simba na Yanga na baadaye timu ya taifa.

Tumeshuhudia Taifa Stars ikifuzu fainali za mataifa Afrika zilizofanyika nchini Ivory Coast, wakati Yanga ikifanikiwa kuingia fainali ya kombe la Shirikisho Afrika msimu juzi na pia iliingia robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika msimu jana.

Lakini pia Simba ikafanikiwa kuingia robo fainali mara mbili ya Ligi ya mabingwa Afrika, mchango mkubwa umetolewa na Rais Samia hivyo hatuna budi kumpongeza, Rais Samia pia alizisaidia timu za taifa mpira wa magongo na ya wanawake.

Timu ya taifa ya mpira wa magongo Tembo Worriers ilifanikiwa kufuzu fainali za kombe la dunia, pia timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Girls, timu zote hizo zilifuzu fainali za kombe la dunia ikiwa ni kwa mara ya kwanza tangu nchi ipate Uhuru.

Kwenye kiwanda cha michezo hasa soka Tanzania imepiga hatua kubwa sana, Ligi Kuu Tanzania bara kwa sasa inashika nafasi ya sita kwa ubora barani Afrika na tayari TFF na Bodi ya Ligi imeamua kuleta VAR ili kusaidia kuendesha ligi vizuri huku timu zikicheza bila kulalamikia maamuzi.

Lakini Rais Samia anatakiwa kuugeukia mchezo wa riadha, mchezo huo umesahaulika tena sana, ikumbukwe kuwa mchezo wa riadhaa ndio pekee ulioiletea heshima kubwa nchi ya Tanzania kuliko michezo yoyote ile.

Hata mchezo wa soka wenyewe bado haujaifikia riadha, kwani riadha imeleta medali ya shaba tena mara mbili, mashindano ya Olimpiki ambayo ni makubwa zaidi duniani yameleta medali mbili za shaba zilizoletwa na wanariadha Seleman Nyambui na Filbert Bayi.

Nakuomba Rais Samia ugeukie mchezo wa riadha kwani unasuasua, chama cha mchezo huo RT nawaona wanasuasua katika kupata fedha za maandalizi ya kuwaandaa Filbert Bayi wa baadaye huku kamati ya Olimpiki Tanzania inasuasua pia na inafikia kulumbana na RT.

Timu za Simba, Yanga na Taifa Stars bado hazijapeperusha bendera ya Tanzania kama ilivyo kwa Bayi na Nyambui, fainali za Olimpiki zinafanana na za fainali za kombe la dunia, lakini fainali za Olimpiki zinashirikisha michezo yote.

Kwenye mchezo wa soka Tanzania haijawahi kushinda medali yoyote hata ya bati, lakini riadha pekee imeitangaza vema Tanzania, lakini kuanguka kwa Tanzania kwenye mashindano ya riadha kiasi kwamba majirani zetu Kenya wakichukua nafasi yetu na kutamba kwenye mbio mbalimbali.

Mkombozi wa riadha hapa Tanzania kwasasa ni Rais Samia, binafsi naamini Rais Samia anaweza kuisaidia riadha na kuivusha juu ili iweze kuipeperusha bendera ya Tanzania, riadha wanaweza endapo wakiwezeshwa tu kama wanavyowezeshwa Simba, Yanga na Taifa Stars.

ALAMSIKI





Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC