Kocha wa Wydad aula Saudi Arabia

Aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Wydad Casablanca, Josef Zinnbauer amejiunga na klabu ya Al Wahda kuwa kocha mkuu ambayo imeshuka daraja katika Ligi Kuu nchini Saudi Arabia.

Josef alitimuliwa na Wydad Casablanca kutokana na mwenendo mbaya wa timu hiyo kwenye michuano yote ya ndani na nje na kuifanya timu hiyo kumaliza bila taji lolote.

Sasa Wydad imempa mikoba kocha wa zamani wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini Rulani Mokwena


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI