Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, ametangaza kuna uwezekano nyota wa Cameroon, Samuel Eto’o, atasalia katika klabu hicho msimu ujao licha ya habari anakusudia kurejea Uhispania kandarasi yake itakapoisha Juni. Mourinho anakusudia kumhifadhi mshambulizi huyo wa zamani wa Mallorca na Barcelona, 32, lakini anasema uamuzi wa mwisho uko mikononi mwa klabu ama Eto’o musimu utakapo karibia kuyoyoma. Eto’o ameibuka mshambuliaji kigezo wa timu hiyo huku Fernando Torres akiendelea kuuguza jeraha la goti huku kampeni ikizidi kuchacha moto.
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com