Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YAITEKETEZA RHINO RANGERS, YAIPIGIA HESABU OLJORO JKT.

SIMBA SC imeanza vyema mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo, unaifanya Simba SC itimize pointi 27 baada ya kucheza mechi 14, ikibaki nafasi ya nne nyuma ya Yanga yenye pointi 31, Azam na Mbeya City pointi 30 kila moja.

Hadi mapumziko, tayari Simba SC walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na mshambuliaji Ramadhani Yahya Singano ‘Messi’ dakika ya 14.

Messi alifunga bao hilo, baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa Rhino na ndipo akaupitia mpira na kufumua shuti kali lililoipa ushindi huo Simba SC.


Pamoja na kufungwa, Rhino walicheza vizuri na kuonyesha upinzani kwa Simba SC ambao katika mechi ya mzunguko wa kwanza walitoka nayo sare ya 2-2 Uwanja wa Ally Hassan Mwinyhi Tabora.

Simba SC ingeweza kuondoka na ushindi mnene zaidi kama si refa Andrew Shamba wa Pwani kukataa mabao mawili ya Amisi Tambwe moja kila kipindi na Messi kukosa penalti dakika ya 70.

Penalti hiyo ilitolewa baada ya Haroun Chanongo kumnawisha mpira beki wa Rhino, Ladislaus Mbogo kwenye eneo la hatari. Messi pia alikosa mabao ya wazi mawili kipindi cha pili.

Kikosi cha Simba SC leo kilikuwa; Ivo Mapunda, Haruna Shamte, Idrisa Rashid, Gilbert Kaze, Donald Mosoti, Awadh Juma, Haruna Chanongo, Amri Kiemba, Ali Badru/Said Ndemla dk, Amisi Tambwe/Betram Mombeki dk65/Henry Joseph dk85 na Ramadhani Singano ‘Messi’.

Rhino Rangers; Charles Mpinuki, Julius Masunga, Amani Juma, Ladislaus Mbogo, Laban Kambole, Hamisi Msafiri, Salum Kamana, Hussein Abdallah, Darlingtn Enyinna, Suleiman Jingo/Salum Majid dk84 na Shijja Mongo.
Fundi wa mpira; Ramadhan Singano 'Messi' akimiliki mpira mbele ya beki wa Rhino

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC