Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SHOMARI KAPOMBE HATIHATI KUTUA YANGA AU AZAM.

Beki wa zamani wa Simba ya jijini Dar es Salaam, Shomary Kapombe, amesema yeye sasa ni mchezaji huru na yuko tayari kufanya mazungumzo na klabu yoyote ya ndani na nje ya nchi ambayo itahitaji huduma yake.

Kapombe ambaye kwa sasa yuko hapa nchini, alikuwa akilelewa kisoka Ufaransa katika Klabu ya AS Cannes akiichezea kwa mkopo kwa lengo la kutumia nafasi hiyo kupata uzoefu wa ligi ya nchi hiyo kabla ya kutafutiwa soko.

Simba ilimtoa beki huyo na kumpeleka Ufaransa kupitia wakala wa mchezaji huyo.

Akizungumza juzi jijini, Kapombe, alisema baada ya Klabu ya AS Cannes kusitisha malipo yake ya mshahara na posho, aliamua kuikacha na kutorejea huko kuendelea na timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la nne.


Kapombe alisema bado ndoto zake za kucheza Ulaya hazijapotea lakini ataangalia maslahi kwanza endapo atapata timu yoyote ya kuichezea hapa nchini. "Mimi niko huru, nilikuwa kwetu Morogoro mzima wala siumwi," alisema beki huyo wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) juzi mara baada ya mechi ya kirafiki kati ya Simba na Mtibwa Sugar iliyochezwa Uwanja wa Taifa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope, alisema hivi karibuni kuwa Kapombe ni mali ya wakala na wakala huyo ndiye anawajibika kwa matatizo yoyote yatakayomkuta mchezaji huyo.

Hanspope alisema wao walichokubaliana na wakala huyo ambaye ni raia wa Ufaransa ni kuhakikisha Kapombe anapata timu ya kucheza huko Ulaya itakayomlipa vizuri na endapo atauzwa rasmi, klabu hiyo ya Msimbazi itapokea malipo ya asilimia 40. Tayari habari ambazo viongozi wa Yanga na Azam wamekataa kuthibitisha ni kwamba wanamhitaji beki huyo ambaye anacheza zaidi ya namba tatu uwanjani.

Mwaka jana Simba ilishuhudia mshambuliaji wake raia wa Uganda, Emmanuel Okwi, akijiunga na wapinzani wao Yanga kiulaini huku wao wakiendelea kuidai timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia Dola za Marekani 300,000.

Kama ilivyokuwa kwa Okwi, Kapombe kabla ya kuondoka alikuwa na mkataba na Simba hivyo klabu hiyo ilihitajika kulipwa kabla ya nyota huyo kuingia mkataba na klabu hiyo ya Ufaransa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC