Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BAINES AONGEZA MKATABA WA MIAKA MINNE EVERTON.

Mlinzi wa Everton Leighton Baines amerefusha muda wake wa kukaa katika klabu hiyo baada ya kutia saini mkataba mpya wa miaka minne, klabu hiyo ya Ligi ya Premia ilitangaza Jumatatu.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza alikuwa amesalia na miezi 17 kwenye mkataba wake Goodison Park na licha ya ripoti kwamba alikuwa akitafutwa na meneja wake wa zamani David Moyes akajiunge naye Manchester United, beki huyo wa kushoto wa umri wa miaka 29 aliambia kusalia Goodison Park.

"Hatuwezi kueleza furaha tuliyo nayo kwamba klabu hii imepata miaka bora ya uchezaji wa Leighton Baines," meneja Roberto Martinez aliambia tovuti rasmi ya klabu hiyo (www.evertonfc.com).

"Ni jambo la kutuongeza nguvu sana na la kuleta msisimko kuhusu siku za usoni. Leighton ametimiza tu miaka 29 majuzi na ana kiwango cha ukomavu na ujuzi wa soka katika pahala maalum uwanjani, na kuwepo kwake kwenye kikosi husikika.”


Baines alijiunga na Everton kutoka Wigan mwaka 2007 na amekuwa na kuwa mmoja wa wachezaji wanaotegemewa sana na klabu hiyo ambayo ameichezea zaidi ya mara 260.

Pia ni mwanachama muhimu wa kikosi cha Uingereza chini ya Roy Hodgson na anapigania nafasi ya kuwa wa kwanza kwenye mechi na Ashley Cole wa Chelsea taifa hilo likijiandaa kwa Kombe la Dunia nchini Brazil mwezi Juni.

"Ninajua kwamba kila shabiki atakuwa na furaha kutokana na habari hizi na tuko pamoja katika msisimko huu tukiangalia sehemu iliyosalia ya msimu huu na hata baadake,” Martinez akaongeza.

"Kutokana na mechi muhimu zilizo mbele yetu, itakuwa muhimu sana kuwa na uzoefu wa Leighton kutuwezesha kupigania malengo yetu.”

Everton walianza vyema msimu chini ya Martinez tangu Mhispania huyo achukue pahala pa Moyes mwanzoni mwa msimu na kwa sasa wako nambari sita kwenye Ligi ya Premia, alama moja pekee nyuma ya jirani zao Merseyside Liverpool, ambao wako nambari nne.

Klabu hiyo pia imefuzu kwa raundi ya tano ya Kombe la FA ambapo wameratibiwa kucheza nyumbani dhidi ya Swansea City.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC