Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JESHI LA YANGA NOMA UTURUKI.

Mabingwa wa soka nchini, Yanga, jana walianza rasmi mazoezi wakiwa nchini Uturuki walipokwenda kuweka kambi ya wiki mbili kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu na mashindano ya kimataifa.

Kikosi cha Yanga jana asubuhi kilifanya mazoezi kwenye uwanja uliopo ndani ya Hoteli waliyofikia ya Sueno Beach mjini Antalya.

Akizungumza kwa njia ya simu, Kocha wa timu hiyo, Charles Mkwasa aliyeambatana na timu hiyo alisema kuwa programu yake rasmi ya mazoezi anaianza leo Jumamosi.


Yanga iliondoka nchini juzi Alhamisi ambapo ikiwa huko inatarajiwa kucheza michezo mitatu ya kirafiki dhidi ya timu za huko.

Mkwasa alisema mechi hizo zitawasaidia wachezaji wake kujiweka imara kabla ya ligi kuanza na pia kupata uzoefu wa michezo ya kimataifa.

“Mbali na ligi kuu, pia Yanga inakabiliwa na mashindano ya kimataifa hivyo kambi ya huku itaisaidia sana na nimepewa taarifa kuwa tutacheza michezo mitatu ya kirafiki ambayo kwangu naona ni ya umuhimu sana kwenye maandalizi yetu haya,” alisema Mkwasa.

Mkwasa alisema amefurahi kikosi hicho kupata safari hiyo ambayo itawasaidia kufanya mazoezi ya kutosha na timu kutoka nchi nyingine tofauti na za Afrika.

Alisema wachezaji wote wako imara na wapo kwenye harui nzuri hivyo wana nafasi ya kuzingatia zaidi mazoezi wakiwa huko.

Mkwasa ambaye anaiongoza timu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Ernest Brandts na msaidizi wake Frerd Felix ‘Minziro’ alisema mazoezi ya jana asubuhi yalikuwa mepesi kwa ajili ya kuweka mwili vizuri na programu yake itaanza rasmi leo.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu wa klabu hiyo Beno Njovu alisema mchakato wa kumpata kocha mkuu bado zinaendelea.

Akizungumza jana alisema wanatarajia kumtangaza kocha wiki ijayo na si jana kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari.

Alisema wao kama viongozi bado wako katika harakati za kutafuta kocha mkuu ambaye atasaidiana na kocha Mkwasa katika kukinoa kikosi hicho cha wanajangwani hao ambacho kwa sasa kipo nchini Uturuki.

Hata hivyo habari kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema baada ya majina mengi yaliyokuwa yameomba kzi hiyo, uongozi umebekisha majina ya makocha wawili raia wa Serbia na Uholanzi ambapo mmoja wapo atatangazwa kocha wa Yanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC