Ruka hadi kwenye maudhui makuu

VAN PERSIE AMTABIRIA MAKUBWA MOYES.

Robin van Persie amesema ana imani kwamba meneja wa Manchester United anayekabiliwa na shinikizo David Moyes atafana Old Trafford.

Moyes amekumbana na mwanzo mbaya wa ufanyakazi wake United kwani timu hiyo imehangaika katika juhudi zake za kutetea taji la Ligi ya Premia na pia ilibanduliwa kutoka kwa Kombe la FA raundi ya tatu.

United wako alama 11 nyuma ya viongozi Arsenal na wanakabiliwa na mlima katika juhudi zao za kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao.

Kumekuwa na uvumi kwamba Moyes ameshindwa kupata imani kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa United.

Na mahangaiko ya klabu hiyo katika juhudi zake za kudumisha viwango vya miaka ya Alex yamepelekea kushuka kwa thamani ya hisa za klabu katika Soko la Hisa la New York.


Lakini straika wa United Van Persie, ambaye amekosa sehemu kubwa ya msimu huu kutokana na jeraha la paja, ana imani kwamba Moyes atafanikiwa akipewa muda.

“Ninafikiri kwamba anahitaji muda sawa na watu wengine wote, hasa ukiwa mgeni katika klabu kubwa,” Van Persie aliambia gazeti la Guardian.

"Na kwa kweli, sidhani kwamba watu hawaelewi kwamba wanahitaji kumpa muda zaidi, na naongea kuhusu mashabiki na hata sisi.

“Atapata muda huo na kila mmoja anajua kwamba tutabadilisha mambo karibuni.

“Tulipoteza alama nyingi msimu huu, nyingi sana, lakini ikiwa unataka kupigania mataji yote, ni lazima ucheze vyema na ushinde mechi nyingi – lakini tunafanya kila tuwezalo kubadilisha hilo.

"Meneja ndiye kiongozi wetu katika hilo na anajaribu kadiri awezavyo na ninafikiri atabadilisha mambo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC