Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UNYAMA MTUPU: KIJANA AUAWA MCHANA KWEUPEE, AHUSISHWA NA 'UASI' TABATA.

Na Salum Fikiri Jr

HALI imeanza kuwa mbaya hasa jijini Dar es Salaam na vitongoji vyake, wananchi wenye hasira kali waishio Tabata Mtambani wamempiga mpaka kumuua kijana mmoja anayefahamika kwa jina la Shada Ibada (Pichani) kwa kumuhusisha na kundi l.akiharifu linalofahamika kwa jina la 'Waasi' ambalo kwa sasa limekuwa kero katika maeneo hayo.

Mwandishi wa habari hizi ambaye alikuwa shuhuda wa tukio hilo amedai kuwa marehemu alikuwa akisakwa kwa muda mrefu kutokana na kujihusisha kwake na vitendo vya uharifu, kabla ya kuuawa marehemu alituhumiwa kuiba maeneo ya jirani ndipo alifukuzwa na wananchi wenye hasira na kumshushia kipigo kilichopelekea kifo chake.

Tayari mwili wa marehemu umeshachukuliwa na polisi na kupelekwa hospitali kwa kuhifadhiwa, hivi karibuni kumezuka kwa vikundi vya vijana vinavyojhihusisha na uporaji, ubakaji na kuharibu amani ya watu, wakazi wa Tabata nao wamejikuta wakiishi kwa shida kufuatia kikundi cha 'Waasi' kuanzisha mtindo mchafu wa uporaji na ubakaji.


Kikundi hicho kimekuwa kikifanya uharifu huo kwenye shughuri mbalimbali hasa sherehe ambapo nyakati za usiku hujitokeza na kuanza uporaji wao, watu mbalimbali wamejitokeza kulaani vikali mchezo mchafu unaofanywa na kikundi hicho cha uasi.

Hata hivyo kampeni imeanzishwa na wakazi wa maeneo hayo ya kuwakamata nyumba hadi nyumba vijana wanaojihusisha na mchezo huo,  Jitihada zao zimeungwa mkono na jeshi la polisi ambapo hadi sasa vijana zaidi ya 10 wameshafikishwa polisi huku wengine wakiendelea kusakwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC