Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LIGI KUU BARA KIVUMBI LEO, YANGA VS ASHANTI, MTIBWA, AZAM HAPATOSHI CHAMANZI.

Baada ya kuwa katika mapumziko ya takribani miezi mitatu, Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo inaingia katika mzunguko wa pili wa lala salama, ambapo nyasi za viwanja vinne zitahitaji maji ili kuzima moto wa timu nane zitakazoshuka dimbani kukwaana.

Viwanja vitakavyowaka moto leo ni Uwanja wa Taifa na Azam Complex vya jijini Dar es Salaam, Uwanja wa Mkwakwani,Tanga na Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Kwenye Uwanja wa Taifa, vinara na Mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga watakabiliana na Ashanti United, wakati Azam wataikaribisha Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Azam Complex huku Coastal Union ikiwa mwenyeji wa JKT Oljoro itakayopimana nayo ubavu kwenye Uwanja wa Mkwakwani.


Kagera Sugar wenyewe watatoana jasho na Mbeya City katika pambano litakalopigwa kwenye Uwanja wa Kaitaba.

Yanga yenye pointi 28, watazindua kampeni zake za mzunguko wa pili wakiwa na mwonekano mpya katika benchi la ufundi ambalo kwa mara ya kwanza litaongozwa na kocha mpya wa timu hiyo, Mdachi Hans Van Der Pluijm na Msaidizi wake Charles Mkwassa.

Lakini muhimu zaidi, Yanga itaingia uwanjani huku ikibeba kumbukumbu nzuri ya matokeo ya ushindi mnono wa mabao 5-1 dhidi ya Ashanti katika pambano la mzunguko wa kwanza.

Hata hivyo, hiyo haiwezi kuwa silaha tosha ya kuishinda Ashanti iliyoko nafasi ya 11, kwani hivi sasa imemwajiri kocha Abdallah Kibadeni ‘King’.

Pluijm akizungumzia maandalizi ya timu yake alisema, “Nina muda mfupi tangu nimekabidhiwa hii timu, lakini ninaweza kusema wachezaji wangu wameelewa mafunzo niliyowapa, naamini tutakuwa na mwenendo mzuri.”

Naye Kibadeni alisema,”Nina timu yenye wachezaji wenye uzoefu ambao wapo tayari kupambana, jambo zuri ni kwamba mpira unachezwa sehemu ya wazi.”

Kwa upande wake kocha wa Azam, Mcameroon Marius Omog ambaye kikosi chake kinakamata nafasi ya pili kikiwa na pointi 27 na leo kinaumana na Mtibwa alisema,”Mashindano ya Kombe la Mapinduzi yalinisaidia kuwajua vizuri wachezaji wangu, nina kikosi cha kuwania ubingwa.”

Lakini mpinzani wake, Mecky Mexime ambaye ni kocha wa Mtibwa Sugar amejinadi kuwa amekipika vizuri kikosi chake akilenga kuhakikisha anavuna pointi zote tatu bila kujali anacheza na nani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC