Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BIN SLUM AICHIMBA MKWARA YANGA, ASISITIZA KIPIGO KIKO PALEPALE MKWAKWANI.

MKURUGENZI wa Ufundi wa Coastal Union ya Tanga, Nassor Bin Slum amesema Yanga SC itakiona cha moto kwa timu yake keshokutwa katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Akizungumza na mtandao huu Bin Slum amesema kwamba vijana wake wapo vizuri kuelekea mchezo huo na hakuna shaka Yanga itaacha pointi zote tatu Uwanja wa Mkwakwani Jumatano.

“Tunakubali msimu huu tumeshindwa kutimiza malengo yetu, siyo kwenye ubingwa tu, bali hata nafasi za nne za juu. Malengo yetu ya sasa ni kumaliza nafasi ya tano,”alisema Bin Slum.


Amesema ili wafanikiwe kumaliza katika nafasi hiyo, lazima wafanye vizuri katika mechi zilizobaki za Ligi Kuu na hawatakubali kuwa ngazi za timu nyingine kuelekea kwenye ubingwa.

“Coastal Union hatutakubali kamwe kufanywa daraja la timu nyingine zenye kutaka ubingwa, na anayetaka kuamini haya Jumatano tunacheza na Yanga, mtawaonea huruma,”alisema.

Coastal Union na Yanga SC ndizo timu pekee za Ligi Kuu zilizoweka kambi nje ya nchi kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi hiyo.

Wakati Yanga walikuwa Uturuki ambako walicheza mechi nne za kirafiki na kushinda mbili na kutoa sare mbili, Coastal walikuwa Oman ambako walicheza mechi nne pia na kushinda mbili, sare moja na kufungwa moja.
  
Katika mechi zao za ufunguzi za mzunguko wa pili Jumamosi, Yanga ilianza vyema kwa kuifunga Ashanti United mabao 2-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Coastal ililazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na JKT Oljoro Mkwakwani.

Yanga SC ambao ndio mabingwa watetezi wa Ligi Kuu, wapo kileleni mwa ligi hiyo kwa pointi zao 31, baada ya kucheza mechi 14, wakifuatiwa na Azam FC na Mbeya City zenye pointi 30 kila moja, wakati Coastal ni ya nane kwa pointi zake 17 baada ya mechi 14 pia.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC