Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUPO TAYARI KWA LIGI KUU-LOGARUSIC

Kocha wa klabu ya Simba Zdravko Logarusic 'Loga' amesema kuwa hana shaka na kikosi chake na kwa sasa timu yake ipo tayari kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara.

Akizungumza jana, Loga, alisema kuwa michezo ya kombe la mapinduzi imewaimarisha zaidi wachezaji wake na kwa sasa wanasubiri mzunguko wa pili wa ligi kuu.

Alisema kuwa wachezaji watakaopata nafasi kwenye mzunguko wa pili wa ligi ku ni wale watakaoonyesha uwezo.

"Mechi tulizocheza Zanzibar zimetumarisha zaidi ni maandalizi mazuri kwa ajili ya ligi..., sina shaka na timu yangu kwa sasa tupo tayari kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi kuu," alisema Loga.


Alisema kuwa lengo lake ni kuhakikisha Simba inachukua ubingwa msimu huu na kusisitiza kuwa uwezo wa kufanya hivyo wanao.

"Nina wachezaji wenye uwezo mkubwa... kila mchezaji akitimiza majukumu yake nina uhakika wa ubingwa mwisho wa msimu," aliongezea kusema Loga.

Alisema kuwa kwake yeye kila mchezaji anauwezo mkubwa lakini navutiwa zaidi na mchezaji Ramdahani Singano 'Messi'.

"nataka wachezaji wajitume kama anavyofanya yeye (Singano), amekuwa mfano wa kuigwa najituma na anajua kazi yake," aliongezea kusema Loga.

Aidha, Kocha huyo aliema mchezo wa kirafiki wa leo dhidi ya Mtibwa Sugar angependa uwe wa mwisho na wajipange kwa ajili ya mzunguko wa pili.

Simba leo inacheza na Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa kirafiki ikiwa ni sehemu maandalizi ya timu hizo kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi kuu uliopangwa kuanza Januari 25.

Simba inacheza na Mtibwa huku ikiwa imetoka kushiriki mashindano ya kombe la mapinduzi ambapo wamefanikiwa kushika nafasi ya pili baada ya kufungwa goli 1-0 kwenye mchezo wa fainali na KCCA ya Uganda.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC