Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KAPOMBE KUREJEA SIMBA.

Uongozi wa klabu ya Simba umesema endapo beki, Shomary Kapombe, atashindwa kurejea AS Cannes inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Ufaransa, mchezaji huyo atalazimika kurejea katika klabu hiyo na hayatatokea kama yalivyojitokeza kwa aliyekuwa mshambuliaji wao, Emmanuel Okwi.

Habari zilizopatikana jijini Dar es Salaam jana zimeeleza kwamba Kapombe hataki kurejea Ufaransa licha ya madai yake dhidi ya klabu hiyo kutatuliwa.

Akizungumza na jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alisema kwa sasa Kapombe ni mali ya wakala, Denis Kadito na kama kuna matatizo kati yake

na wakala huyo wanatakiwa kukaa na kuzungumza ili kutimiza makubaliano waliyoingia kabla ya kujiunga na AS Cannes.

Rage alisema wanaamini Kapombe bado ana nafasi ya kupata klabu barani Ulaya na atakapofanikiwa itakuwa ni faida kwa mchezaji husika na nchi pia.


Mwenyekiti huyo, alisema endapo Kapombe ataamua kuikacha AS Cannes atatakiwa kurejea nchini kuitumikia Simba kwa sababu ana mkataba unaomalizika 2016.

“Wala haitatokea kama ilivyokuwa kwa Okwi, hata sisi tunashindwa kuzungumza na Kapombe kwa sababu tunazifahamu kanuni na taratibu za Fifa, sasa hivi mchezaji yule ana wakala na yeyote anayemhitaji anatakiwa kupitia kwa wakala na si kinyume na hapo,” Rage aliongeza.

Alieleza baadhi ya makubaliano yaliyopo kati ya mkataba wa Kapombe na wakala, Simba itapata asilimia 20 mchezaji huyo atakapouzwa katika klabu nyingine au atarejea

kuitumikia Wekundu wa Msimbazi endapo atashindwa kupata timu huko Ulaya.

Kapombe ambaye alisajiliwa na Simba akitokea Polisi Morogoro, mkataba wake wa awali na Simba ulikuwa unatarajiwa kumalizika Aprili mwaka lakini mwaka jana klabu

hiyo ilimuongezea mkataba wa miaka miwili na kumuongezea mshahara wake yeye pamoja na wachezaji wengine waliopandishwa kutoka Simba B.

Beki huyo yuko hapa nchini tangu mwaka jana na habari zaidi zinaeleza kuwa, klabu za Yanga na Azam zinadaiwa kufanya mazungumzo ya awali ya kutaka kumsajili.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...