Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OSCAR AIBEBA CHELSEA IKIIADHIBU STOKE.

Bao maridadi kutoka Oscar liliiongoza Chelsea kuwalaza Stoke City 1-0 katika raundi ya nne ya kombe la FA jana Jumapili.

Kiungo huyo wa Brazil ambaye alichukua nafasi ya Juan Mata, aliyesajiliwa na Manchester United, kama kielelezo cha mashambulizi, alitia kimiani kutokana na mkwaju wa adhabu.

Ubora wa bao lake nyota huyo lilidhihirisha sababu iliyomfanya meneja Jose Mourinho kuekeza imani naye na kumruhusu Mata kuondoka Stamford Bridge siku mbili zilizopita.


Chelsea walipoteza nafasi kadhaa za kuadhibu Stoke huku wakipata ulingo wa lango mara mbili lakini hatimaye, wageni wao hawakutishia kulazimisha wenyeji mechi ya marudiano.

“Bao moja kwa bila haitoshi kuonesha jinsi tulivyocheza na kumiliki mechi. La muhimu ni kushinda na kuepuka mchuano wa marudio kwani hatuhitaji mechi ya ziada,” Mourinho aliambia runinga ya ITV.

Meneja wa Stoke, Mark Hughes, alilalamikia uamuzi wa mkwaju wa adhabu dhidi ya Erik Pieters baada ya kukabiliana na straika, Samuel Eto’o, ambao Oscar alifunika wavuni lakini aliinuliwa moya na jinsi vijana wake walivyo cheza.

“Hatukubuni nafasi wazi. Ilikuwa ngumu kwetu lakini ninafurahia yale tuliyoyafanya. Hatukuzama nah ii ni ishara ya mazuri,” aliendelea.

Wachezaji wenye uzoefu miongoni mwao nahodha John Terry na kipa Petr Cech walipumzishwa ingawa Eto’o alipewa nafasi ya kuanza na Mourinho huku Demba Ba, aliyetarajiwa kuorodheshwa akibaki kwenye benchi.

Ni bidii za nyota huyo wa Cameroon aliyefunga matatu dhidi ya United wiki iliyopita ambazo zilifungua ngome ya Stoke na kumruhusu Oscar kuibuka shujaa katika dakika ya 27 pale alipochezewa vibaya na Pietersen.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC