Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LOGA AIPONDA FOWADI SIMBA, AZIDI KUMUANDAMA MWOMBEKI.

 Baada ya kupata ushindi finyu katika mechi yake ya kwanza katika Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic 'Loga', amesema ligi hiyo ni ngumu na timu ndogo ndizo zimekuwa kikwazo kwa klabu kongwe za hapa nchini, lakini akaweka wazi kuwa washambuliaji wake bado hawajaelewa darasa lake.

Simba juzi iliifunga Rhino Rangers ya mkoani Tabora bao 1-0 lililoiwezesha kufikisha pointi 27, hivyo kuendelea kukaa katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na wapinzani wao Yanga wakifuatiwa na Azam FC na Mbeya City.


Akizungumza juzi baada ya mechi, Loga, alisema mechi yao ilikuwa ngumu na ushindi huo finyu walioupata umethibitisha kwamba hakuna timu ya kuidharau katika ligi.
Loga alisema kikosi chake kilikutana na ushindani na kupoteza nafasi nyingi za kufunga ambazo walitengeneza katika mchezo huo.

"Ligi ina ushindani, ina changamoto na si rahisi, kila timu sasa ni kubwa, leo (juzi) nimethibitisha timu ndogo zinavyoendelea kuzisumbua timu kongwe. Jambo zuri nimefurahi ni kupata ushindi," alieleza kocha huyo raia wa Croatia.

Loga alisikitishwa pia na kitendo cha wachezaji wake kukosa nafasi za kufunga na kueleza kwamba hali hiyo inatokana na kikosi chake kutokuwa na washambuliaji wenye uzoefu.

Alisema anatarajia katika mechi ijayo kuwaanzisha Edward Christopher na Zahor Pazi.
Hata hivyo, wakati Loga akieleza hayo, mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe ndiye anayeongoza katika orodha ya wafungaji kwenye ligi hiyo.

AMCHAMBUA MWOMBEKI


Loga alisema hataweza kuvumilia kuona mchezaji anabaki uwanjani akifanya 'madudu' na si yale aliyoelekezwa katika benchi la ufundi kabla ya kuingia kucheza.

Kocha huyo alisema mchezaji anayecheza kwa kufuata maelekezo ataendelea kumpa nafasi kwa sababu malengo yake kila mechi ni kushinda.

"Sina ujamaa na mtu, wao ni wachezaji na mimi ni kocha, anayefanya vizuri atabaki uwanjani na atakayeharibu nitamtoa nje, hii ni katika kujenga uimara wa kikosi changu kwenye kila idara," Logarusic aliongeza.

Betram Mwombeki aliingia katika dakika ya 65 akichukua nafasi ya Tambwe lakini zikiwa zimebakia dakika nne mchezo kumalizika alimtoa nje kutokana na kuboronga, hivyo kumpisha kiungo, Henry Joseph.

Simba itaanza tena mazoezi leo kwa ajili ya kujiandaa na mechi yake dhidi ya JKT Oljoro itakayofanyika Februari Mosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC