Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA KUTUPA KARATA NYINGINE LEO UTURUKI, KUCHEZA NA TIMU YA LIGI KUU.

Mabingwa wa soka nchini, Yanga wanaendelea na mandalizi yao kwa ajili ya ligi kuu na mashindano ya kimataifa na leo wanacheza mchezo wa tatu wa kirafiki dhidi ya KS Flamurtari Vlore inayoshiriki ligi kuu nchini  Albania.

Yanga ipo nchini Uturuki ilipokwenda kuweka kambi na itacheza na timu hiyo ambayo nayo ipo nchini humo kwa ziara ya mafunzo.

Akizungumza kwa njia ya simu, Afisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto, alisema kuwa mchezo huo wa leo ni sehemu ya mafunzo yao na kocha mpya wa timu hiyo, Johanes Franciscus 'Hans' van der Pluijm anataka kutumia michezo ya kirafiki nchini humo kukifahamu vizuri kikosi chake.


"Mwalimu anatumia michezo hii kuwaona wachezaji wake kama unavyojua ameungana na timu hivi karibuni tu, hii ni nfasi yake ya kuangaliwa wachezaji wake ili ajue anaanzia wapi," alisema Kiziguto.

Alisema timu hiyo ilifanya mazoezi ya nguvu juzi asubuhi chini ya kocha mpya na wako tayari kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki.

Alisema kuwa baadea ya mchezo wa leo watacheza mchezo mwingine wa kirafiki katikati ya wiki ambao utakuwa wa msiho kabla ya kuanza safari ya kurejea nchini.

Aidha, alisema kuwa kambi ya timu hiyo aina majeruhi zaidi ya kiungo, Hassan Dilunga ambaye anasumbuliwa na malaria.

"Dilunga anasumbuliwa na malaria lakini tayari ameanza dozi na anatibiwa na daktari wa timu Suphian.., zaidi ya huyo hakuna majeruhi mwingine," alisema kiziguto.

Alisema kuwa kambi ya nchini humo imewasaidia zaidi wachezaji wake ambao sasa wapo tayari kwa ajili ya mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara.

Ikiwa nchini humo tayari Yanga imecheza michezo miwili ya kirafiki na zote kuibuka na ushindi

Awali ilianza kucheza na Ankara Sekerspor na kushinda magoli  3-0 na baadae kucheza na Altay Sk na kuibuka na ushindi wa magoli 2-0.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC