Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OWINO AUFYATA MKIA KWA LOGA, AREJESHWA KUIVAA OLJORO JKT

BEKI Joseph Owino amejishusha na kuomba radhi kwa kocha Zdravko Logarusic mbele ya wachezaji wenzake, juu ya tuhuma zake za utovu wa nidhamu na kujiona yuko juu ya wenzake- na bahati nzuri kwake amesamehewa na kurejeshwa kikosini.

Habari kutoka ndani ya Simba SC zimesema kwamba, Owino aliandika barua ya kuomba radhi na baada ya hapo akaitwa kutakiwa kufanya hivyo mbele ya wachezaji wenzake pia, ili waridhie.

Owino alipima kina cha maji kwa Logarusic, akagundua parefu hatimaye ameomba radhi na sasa amerejeshwa kundini

Wachezaji wote wa Simba SC walipokea ombi la Owino kwa mikono miwili na kumkaribisha tena kundini, waendelee kupeperusha bendera nyekundu na nyeupe ya Mtaa wa Msimbazi.

Lakini pamoja na kusamehewa, Owino atakatwa mshahara kwa siku zote ambazo hakuwa kwenye timu.


Mcroatia huyo alikuwa anamtuhumu Owino mambo mawili, kutofuata maelekezo yake na kujiona yuko juu ya wachezaji wenzake na kwa sababu hiyo akaona hafai kuwamo kwenye kikosi chake, hadi akubali kubadilika.

Owino alikorofishana na kocha Loga wiki iliyopita, akidai kutukanwa na mwalimu huyo wa zamani wa Gor Mahia ya Kenya, hivyo kujitoa mazoezini siku mbili kabla ya Simba kucheza mechi ya kwanza ya mzungkuo wa pili wa Ligi Kuu dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora Jumapili.

Na tangu wakati huo, Owino aliendelea kususia mazoezi Simba SC huku akipeleka malalamiko yake kwa uongozi kwamba hapendwi na kocha huyo.
Loga akaipangua hoja ya kutompenda Owino kwa kusema amekuwa akimpanga mchezaji huyo tangu ameanza kazi Msimbazi pamoja na mapungufu yake na kama angekuwa hampendi asingekuwa anampa nafasi.
  
Mganda huyo sasa anatarajiwa kuanza mazoezi leo, tayari kwa mchezo wa mwishoni mwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC