Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM YAVULIWA RASMI UBINGWA WA MAPINDUZI.

Mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam FC jana walivuliwa ubingwa baada ya kukubali kipigo cha magoli 3-2 kutoka kwa KCC ya Uganda kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza uliochezwa kwenye uwanja wa Amaan kisiwani hapa.

Azam ndio waliokuwa wa kwanza kupata goli kupitia kwa nyota wa mchezo huo, ‘yoso’ Joseph Kimwaga katika dakika ya 16 akimalizia kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na beki wa pembeni Erasto Nyoni.

Azam waliendelea kuliandama goli la KCC na katika dakika ya 32 kimwaga tena aliipatia Azam goli la pili akimalizia kwa mguu wa kulia pasi ya ‘kupenyeza’ iliyopigwa na Kipre Tchetche baada ya raia huyo wa Ivory Coast kuwachambua mabeki wa KCC kabla ya kutoa pasi hiyo kwa mfungaji.


Hata hivyo dakika tano baadae, KCC walipata goli la kwanza lililofungwa na beki wake Ibrahim Kiiza kwa shuti kali la mguu wa kushoto lililotokana mpira wa faulo uliomshinda mlinda mlango wa Azam Mwadini Ali.

Mpaka timu hizo zinakwenda mapumziko Azam ilikuwa mbele kwa goli 2-1.

Kipindi cha pili cha kilianza kwa kasi huku KCC wakionekana kutafuta goli la mapema ambapo juhudi zao zilizaa matunda dakika sita tu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili ambapo Tony Odur aliisawazishia KCC kwa kufunga goli zuri akimalizia pasi ya mfungaji wa goli la kwanza Kiiza.

Huku ikionekana kama mchezo huo utamalizika kwa sare, KCC waliwashangaza Azam baada ya winga wake wa kushoto William Wadir kuiandikia timu yake goli la tatu na la ushindi baada ya kuwakimbiza kwa kasi mabeki wa Azam kabla ya kuachia shuti kali liloshinda golikipa Mwadini ambaye alikuwa ametoka golini kwenda kumzuia winga huyo.

Baada ya mchezo huo, Kocha msaidizi wa Azam FC, Kally Ongala, alisema kuwa wachezaji wake ‘walitoka mchezoni’ baada ya kufungwa goli la pili.

Alisema kuwa wapinzani wao walitumia makosa hayo na kupata goli la ushindi.

Kwa upande wake, Kocha wa KCC, George Nsimbe, alisema kikosi chake kiliizidi mbinu Azam hasa kipindi cha pili kutokana na uzoefu wa wachezaji wake.

Kwa matokeo hayo, KCC imetinga hatua ya fainali na ilikuwa ikisubiri mshindi wa mchezo wa jana usiku kati ya Simba na URA kuungana kucheza fainali ya mashindano hayo itakayochezwa kesho Jumapili.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC