Katika michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya leo kuna kivumbi kingine ambapo CSKA Moscow itakuwa na kibarua kigumu pale watakapowakaribisha Bayern Munich. Wakati huo huo Man City waliopigwa bao moja na Bayern Munich watakutana na AC Roma iliyowapiga CSKA Moscow mabao matano katika mechi iliyopita. Paris St G ya Ufaransa wao wanakutana uso kwa uso na Barcelona Ukumbumbuke katika mechi ya wikendi iliyopita Paris St G walitoka sare na Ajax bao moja kwa moja. Ajax inakutana leo na Apoel Nic ambayo ilipigwa na Barcelona bao moja katika mechi ya awali.
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com